Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Friday, December 31, 2010

2011

Chekazone inawatakia wadau wake wote heri ya mwaka mpya na fanaka tele. Mungu awajaalie heri katika maisha yenu ya kila siku.

Wanandoa wakigombana

Wanandoa wawili baada ya majibizano yaliyogharimu takribani nusu saa yaliishia hivi:
Mwanamke: Nilikua mpumbavu kukubali kuolewa na wewe.
Mwanaume: Nili-fall in love ndio maana sikuliona hilo.

Mbwa

Mtoto mmoja alimuuliza baba yake, "baba hivi kwa nini huyu mbwa wetu hapa nyumbani anapenda saaana kufukuza gari huku akibwaka kama avile anataka kuling'ata?"
Baba mtu akamjibu mwanae kwa kicheko "hehehe mwanagu unajua nini? Huyu mbwa anadhani atapewa gari aendeshe"

Apointiment

Dereva mmoja alikua akitafuta pa kupaki gari yake bila mafanikio,
Ikafika hatua akabandika kikaratasi kimeandikwa "nimezunguka jengo kwa dk 20 sijapata pa kuegesha gari. Hivyo nimeamua kuliegesha hapa nina apointment vinginevyo ntapoteza kazi yangu" akakiweka kwenye kioo na kukishikizia na wiper.

Aliporudi akakuta na yeye kikaratasi cha mkatisha ticket za parking kimeandikwa "nimefanya kazi hii kwa miaka 20 na hii ndio mara ya kwanza siwezi kukuachia vinginevyo ntapoteza kazi yangu"

Maua

Ndugu mmoja alimtembelea ndugu yake anaeishi mjini. Ikawa kila siku alfajiri anajituma kumuagilia maua ya ndugu yake mwenye nyumba mjini.

Siku moja akamuuliza ndugu yake ''nimekua nkimwagilia sana maua yako ya nje na ndani ila ya ndani sioni mabadiliko si uyatoe nje yakue vizuri?''

Ndipo ndugu yake akamjibu, ''ooh pole sana haya ya ndani ni ya plastik sio maua halisi''

Wednesday, December 29, 2010

Maji

Siku moja familia moja ilienda mikumi kuangalia wanyama. Sasa wakati wanaangalia angalia wakaona pundamilia wakiwa pembezoni mwa mto wakinywa maji.

Mtoto akamuuliza baba yake, ''sasa baba hawa pundamilia maji yao yamechemshwa kweli?''

Monday, December 27, 2010

Alarm system

Jamaa mmoja alibahatika kununua gari, sasa kwa vile mpaka anainunua gari yake mpaka inakaa barabarani akawa kama ameshaishiwa hela. na akihitaji kweli kuweka alarm system mapema awezavyo. Akapata wazo la ziada la kusogeza siku, si akallipaka pilipili gari lote. Halafu kichwani akiwaza "dah hapa itakua sijamkomesha mwizi ataejitokeza hasa kama ni mhindi"

Foleni ya magari

Siku moja jamaa wawili walikua wakitwanga stori za hapa na pale zikaingia mpaka zihusuzo foleni za barabarani. Jamaa mmoja akasema "dah foleni za dar bwana, jumapili zinaafadhali kidogo"

Mwenzake akadakia na kujibu "weeweee! Kitu ubungoooo. Pale foleni ni compulsory"
Yaani akimaanisha ni laziiimaa!

Kucha za kubandika

Mtoto mmoja alimuuliza mama yake mzazi "mama mi nna swali"
Mama yake akamuambia "uliza tu mwanangu"
Ndipo mtoto akauliza "hivi kucha za kubandika ukikata zinakua?"

Saturday, December 25, 2010

Spea tairi

Mtoto mmoja akimuuliza baba yake "baba, hivi spea tairi huwa inapataga pancha?"

Xmas

Mtoto mmoja alimsumbua sana baba yake kuhusu sherehe za xmas!
Ilikua baba ninunulie hiki, baba ninunulie kie.
Baba yake akashindwa kuvumilia akamuambia
"Mwanangu mpenzi xmas imeahirishwa mpaka mwakani"

Friday, December 17, 2010

Sh 200

Jamaa mmoja alienda kununua sigara packti zima.
Alipofika akajikuta ata pungufu ya shilingi mia mbili. Muuza duka akakomaa bila mia mbili hatoi kitu. Jamaa akaenda nyumbani na kumchukua mwanae wa miaka minne na kumpa muuza duka.

Muuza duka akauliza, ''sasa huyu mtoto ndio wa nini mie?''
Jamaa akamjibu, ''ile mia mbili anayo huyo mtoto aliimeza ichukue''

Thursday, December 16, 2010

Mgonjwa kulazwa

Mgonjwa mmoja wa malaria alipoenda hospitali akaambiwa alazwe kulingana na hali aliyokua nayo. Bahati mbaya akaambiwa wodi na vitanda vyoote vimejaa, jamaa (mgonjwa) akadakia na kusema ''ina maana hata mochuari nako kumejaa? Nipelekeni huko''

Tuesday, December 14, 2010

Saprizi

Mwanamke mmoja aliporudi nyumbani mumewe akamfunika nakitambaa usoni.

Akampeleka mpaka kwenye meza ya chakula, sasa mkewe alikua anasumbuliwa na tumbo. Akawa anajinyanyua upande mmoja akijamba mara kama tatu.

Mumewe alipomfungua kile kitambaa ili akutane na hiyo sapraizi. Hamadi meza ya chakula imejaa wakwe wa pande zote mbili...

Malengo

Watoto wawili mapacha wakiwa bado tumboni mwa mama yao wakiongea:
Mtoto wa kwanza: Mimi nikitoka humu ndani lazima niwe fundi umeme, kwa sababu ya hili giza.

Mtoto wa pili: Mimi lazima niwe muwindaji.
mwenzake akamuuliza. ''Kwa nini?''
Akajibu: We humuoni yule nyoka anaeingia humu mara kwa mara.

Monday, December 13, 2010

Kigugumizi

Vijana watatu walikuwa wanasafiri toka Dar kwenda Morogoro na gari ndogo. Ghafla maeneoo ya kimara akakatisha jamaa na guta/mkokoteni wakamkosa kosa. Yule mwenye kigugumizi akawa anatukana sasa kile kigugumizi akaanza tangu eneo la tukio mpaka anafika Kibaha ndio akalipata tusi alilokilitamka...

Sunday, December 12, 2010

kutojua matumizi

Mtoto mmoja alikua hajui jeneza ni kitu gani siku moja akamfuata baba yake na kumuambia ''baba... baba... Ninunulie jeneza la kuchezeaa''

Dereva

Dereva mmoja alikamatwa na askari wa usalama barabarani akawa anaulizwa na kijibu kama ifuatavyo:
Trafiki: Una stika ya usalama barabarani?
Dereva: Ndio.
Trafiki: Fire Extinguisher?
Dereva: Ndio. Ila sina leseni tu...

Saturday, December 11, 2010

Mgao wa umeme

Jamaa mmoja wakati yupo kijiweni anatwanga stori na wenzake, mmoja akasema ''dah huu mgao wa umeme kero sana Dar, na hili joto mh''
Ndipo mwenzake akanena, ''ooohh ndio maana nyumbani nasikiaga kitu kama jenereta, kumbe kuna mgao siku hizi?''

Friday, December 10, 2010

Network

Jamaa mmoja alimuona dereva wa lori moja limechoka choka hivi likiwa barabarani. Akamuona dereva wa lori anaongea na simu huku akiendesha. Akamuuliza yule dereva ''samahani, hivi kumbe na humo network inapatikana?''

Thursday, December 9, 2010

Akili za darasani

Mtoto mmoja alimuuliza baba yake ''eti baba inawezekana kukopa?''
Baba hakuelewa akamuuliza, ''sijakuelewa mwanangu''
Mtoto: Kesho kutwa kuna mtihani nataka nimkopeshe Raymond akili zake maana sijasoma kabisa''

Kuopoa bar

Jamaa mmoja alienda Bar, akamuona mrembo mmoja akamuomba wakae nae meza moja.
Wakati wanapiga stori. Jamaa akawa anamuambia yule mwanamke, ''onja basi bia kidogo''

M-dada akajibu ''ooh mimi sinywi bia kabisa''
Jamaa akasisitiza zaidi ''jaribu tu si kidogo tu''
Mwanamke, ''nna dozi bwana leo''
Jamaa: Yaani kidogo tu, dozi gani hiyo bwana?''
Mwanamke: Nipo kwenye dozi ya ARV kaka....

Wednesday, December 8, 2010

Dude

Wakina dada wawili wlimuona mmasai kakaa vibaya wa kiume! Wakawa wanamuona maeneo nyeti! Mmasai alipowashtukia akawaambia ''nyie mnaishangaa hii? Nnazo zingine tatu nyumbani''

Saturday, December 4, 2010

Umeme

Jamaa mmoja akimuuliza mwenzake, ''jana nlikuona na mrembo pale kibarazani''
Jamaa aliekua na mrembo, ''ndio bwana nilikua namtongoza''
Jamaa wa kwanza, ''enhe sasa ikawaje?''
Akajibu, ''nilishindwa kuongea''
Jamaa akamuuliza ''kwa nini ulishindwa?''
Aliekitongoza akajibu ''umeme ulikatika sikuweza kusoma kikaratasi maneno ya kuongea''

Kagera

Jamaa wakiongelea kazi, mmoja akamuuliza mwenzake, ''aisee hivi ulisema wamekupagia wapi kazi?''
Jamaa yake akamjibu, ''dah si Kagera ndugu yangu'' mwenzake akajibu ''duh! Si kuna kutekwa tekwa njiani kule?''
Jamaa akajibu, ''we acha tu, sijui ndio wamenitoa kafara au ndio wananipeleka mafunzoni''

Thursday, December 2, 2010

Kuendesha usiku

Dada mmoja akimuambia mpenzi wake amfuate alipoenda kwenye sherehe. ''Mpenzi wangu najua hupendi kuendesha gari usiku ila leo naomba uje kunichukua sherehe ikiisha''

Mchumba na akamjibu, ''mpenzi ntakuja kukufuata ila si unajua kuna mgao wa umeme, naogopa pia wasije kata umeme kwenye gari bure.''

Mlevi akiongea

Mlevi mmoja akiongea
''nikopeshe hela ndugu yangu, ntakulipa wiki ijayo nimekwama kwa kweli mwenzangu. Naahidi kesho tu ntakurudishia pesa yako.''
Akii-a-mbia ATM''

Mvua

Jamaa mmoja alimpigia simu jamaa yake simu na kumuuliza, ''aisee za masiku? Mvua vipi huko inanyesha?''
Jamaa ake akajibu ''nzuri tu, ila mvua ndio inanyesha!''
Alieuliza mwanzo akanena, ''dah! Hadi mvua ya mgao mbona huku hainyeshi!!?''

Tuesday, November 30, 2010

Gari kutoa moshi

Mtoto mmoja aliporudi nyumbani toka shuleni akawa anamsimulia baba yake, ''baba leo tumepelekwa jumba la makumbusho tumejifunza mengi''

Baba akanena, ''safi sana mwanangu.''
Mtoto: Pia nimewaambia waje nyumbani kukuona.
Baba: Enh??!! Kuniona? Akina nani?
Mtoto: Si watu wa makumbusho:

Baba: Mimi wananifuata ili iweje.
Mtoto: Nimewaambia baba angu ana gari la zamani na linatoa sana moshi, na wao wanataka gari la zamani linalotoa moshi mwing kama lako.

Afrika kusini

Mama: Mume wangu safari bado haijaiva.
Baba: Najipanga mke wangu, South Africa maisha yapo juu kidogo.
Mtoto: Mhh! Baba, we si ulisema unaenda Afrika Kusini? Mbona mama unamdanganya unamuambia unaenda South Africa?

Maneno

Mwanaume mmoja alifuatwa na jirani mwema na kumuambia ''baba nanihi nimemuona mke wako yupo na mwanaume mwingine muda huu huu.''

Mwanaume aliefuatwa akajibu, ''ooh bora mwanaume maana nlishamkataza kukaa na wanawake umbea mwingi.''

Monday, November 29, 2010

Mke na mume

Mwanamke mmoja alikua amekaa sebuleni na mwanae, punde akachukua simu na kumpigia mumewe huku simu ikiwa katika sauti kubwa (loud speaker) ''mume wangu upo wapi? Mbona unachelewa kujibu''

Mume akawa anajibu kupitia simu, ''naja punde mke wangu nipo kwenye jam''
Kale katoto kakaenda jikoni na kurudi huku kakimuambia mama yake ''mama...mama... Baba muongo mbona hayupo humu kwenye chupa ya Jam'' (mithili ya siagi)

Unataka kusoma nini

Baba mmoja alikaa kibarazani na mwanae wa miaka minne akiongea nae, akamuuliza swali ''mwanangu ukikua mkubwa ungependa kusoma nini?''

Mtoto nae bila hiyana akamjibu Dad yake, ''mimi baba? Nikikua nataka nisome magazeti''

Mavituzi

Mwanamke mmoja wa kipemba alikuja Dar, siku moja akaopolewa na kidume. Alipewa malavidavi moto moto ikiwa kunyonywa kona zote.

Siku aliporudi kwa mumewe zanzibar wakati yupo na mumewe wakati wa malavidavi akamuambia ''mume wangu, Dar yaliwa hiyo''

Dogo

Dogo mmoja akimuambia ama kumuuliza baba yake, ''baba... nyumba ina dirisha, gari lina dirisha, ndege ina dirisha sasa mbona hamna dirisha kwenye baiskeli?''

Sunday, November 28, 2010

Chai time

Jamaa mmoja alikua anapita sehemu karibu na mgahawa, akaona mini-bus aina ya Coaster ina jeneza imepaki ikiashiria wasindikiza maiti wanapata kifungua kinywa.

Akamuita dereva wa ile bus na kumuuliza:
Jamaa: Samahani we ndi dereva?
Dereva: Ndio kaka, kulikoni?
Jamaa: Mbona mmesimama hapa?
Dereva: Mkuu tunapata chai kidogo safari ndefu.
Jamaa: Sasa mwenzenu kwenye jeneza mbona hamjamnunulia hata andazi?

Friday, November 26, 2010

Ajali kusimulia

Dogo mmoja akiwasimulia wenzake ''dah, baba angu si kapata ajali?''
Dogo wa pili, ''kagongwa na gari?''
Dogo wa kwanza, ''ndio! Yaani bora kagongwa na benz kuliko ingekuwa corolla''

Taratiibu

Jamaa mmoja alikua na mpenzi wake chumbani, alipotoka bafuni mchumba wake akamuambia ''ee chupi yako saafi''

Jamaa alipofika kitandani akawa anakaa taratiiiibu saaana, mpenziwe akamuuliza ''vipi misuli imekushika?''

Jamaa akajibu, ''naogopa ntaichafua chupi''

Mimba

Baba mmoja akifanya ishara kadha wa kadha mbele ya tumbo la mkewe ambae ni mjamzito.
Mkewe alimuangaliaa mwisho akashindwa vumilia akamuuliza ''kwani mbona sikuelewi mwenzangu?''

Mumewe bila hiyana akamjibu, ''we huoni kuwa namfundisha mwanangu tangu akiwa tumboni akitoka awe trafiki polisi?''

Kuonja

Mtoto: Mama hiyo unayotengeneza ni nini?
Mama: Natengeneza sumu nimuwekee baba yako ananiudhi sana.
Baada ya masaa kadhaa.
Mtoto: Mama nimeionja ile sumu taamu, baba atafaidi kweli leo.

Mtoto akisimulia jambo

Mtoto: Mama nikuambie kitu?
Mama: Niambie tu mwanangu.
Mtoto: Haya, kwani baba muoga eenhe?
Mama: Mh!! Kwa nini mwanangu?
Mtoto: Maana ukisafiri huwa anaogopa kulalia godoro anamlaliaga dada wa kazi tuuu.

Wednesday, November 24, 2010

TV

Mtoto mmoja alizoea kuona TV za kisasa tangu amezaliwa. Siku moja akaenda kutembelea ndugu zao alipofika akaona TV zile zenye kichogo nyuma akamuita baba yake na kumuuliza ''baba hii nini nyuma ya TV?''

Kwa dokta

Dokta mmoja wa kiume akimhudumia mama mjamzito.
Dokta: Hii ni mimba yako ya kwanza?
Mjamzito: Ndio, hivi huwa inauma wkati wa kujifungua?
Dokta akajibu, ''mimi mbona nlijifungua bila maumivu''

Bata

Kibosile mmoja alienda kuangalia sarakasi, mwanasakasi mmoja akawa amemuweka bata chini ya beseni amemfunika juu chini huku akiruka ruka na kucheza.

Yule kibosile akaongea na jamaa mpaka akamunua yule bata. Siku chache mbele akampigia simu yule aliemuuzia, ''halo... Mbona bata hachezi kama siku ile?

Jamaa akamjibu, ''ulikumbuka kumuwashia mshumaa?''

Tuesday, November 23, 2010

Hela iko wapi?

Mama akimuuliza mama yake.
Mama: Jesca mwanagu ile pesa yangu pale mezani ipo wapi?
Mtoto: Ooh! Nimeitumia mama ila niliitoa photocopy nimekuachia kopi.

Friday, November 19, 2010

Mtoto na mama yake

Mtoto mmoja akimuambia mama yake mjamzito alipomuona anakoroga chai. ''wee mama weewee! Shauri yako, utamuunguza mtoto tumboni''

Pesa bank

Jamaa mmoja alianza kuangua kiliobaada ya kusikia taharifa ya habari, kuulizwa kulikoni akajibu ''nimesikia kwenye taharifa ya habari bank ya cbn imeibiwa milioni mia tawi la mjini''

Jamaa akawa hajamuelewa, ''sasa wewe unalia nini?''
Anaelia akajibu, ''si jana tu nimeweka milioni mia tawi lile lilee'' (huku akifuta machozi)
Msimuliwaji alicheka mpaka akakaa chini na kumuambia ''hehehe imeibiwa bank au wewe? Hahahaha!''

Kituo cha polisi

Jamaa mmoja alienda mpaka kituo cha polisi akafika na kuuliza, ''nna tatizo nyumbani kwangu''
Polisi akamuuliza: Tatizo gani hilo lililokuleta?
Jamaa akajibu: Kuku wangu wawili wameibiwa na mbwa wenu.
Polisi: Mbwa wetu?
Jamaa: Si yule mbwa anaitwa polisi kwani sio wenu?

Wednesday, November 17, 2010

Siku ya kwanza shuleni

Mama alimuuliza mwanae baada ya kurudi kutoka shule siku ya kwanza, ''enhe mwanangu umejifunza nini leo shuleni?''
Mtoto akamjibu mama yake ''bado sijajifunza vya kutosha itabidi nirudi tena kesho''

Kojoleo

Mtoto mmoja wa kike alimuambia baba yake ''baba na mimi ninunulie kojoleo kama la dereva''

Tuesday, November 16, 2010

Dawa ya usingizi

Jamaa: Dokta zile dawa ulizonipa jana mbona ni za usingizi?
Dokta: Ndio, si ndio ulizotaka nikupatie?
Jamaa: aah mi nlitaka za kulala sio za usingizi.

Teja

Teja moja (bwia unga) alikuwa kituo cha daladala akiitia/piga debe daladala ''tandika tandika gari...'' huku anasinzia na ule ulevi wao wa kubwia unga.
Kuja kuhamaki ''kumbe daladala ishatimua kitaambo kama dakika tano zilizopita''

Sunday, November 14, 2010

Moto

Mtoto mmoja akimuambia baba yake kwenye simu wakati nyumba yao inaungua moto, ''baba... baba... Heee wahi uone nyumba yetu inaungua kaaama kwenye sinema ya James Bond vile gadi raha''

Mswaki

Jamaa mmoja alienda kwa rafiki yake na kumuambia nna bidhaa nauza ikiwemo miswaki!
Jamaa anae uziwa akanunua.

Kesho yake jamaa akapita tena ''aisee mswaki ulioniuzia mzuri nimeupenda sana.''
Jamaa akamjibu ''asante sana ipo mingine kama unataka yote used kama nliokuuzia''

Saturday, November 13, 2010

Maongezi ya vijana

Vijana watatu wa kiume na msichana mmoja wakiongea mara akapita msichana mrembo mmoja kati ya wale vijana akasema ''dah mrembo yule mtamu'' mwingine akasema ''si mchezo''

Ikafika muda wa yule dada kati ya vijana watatu akamuuliza kijana mmoja wa tatu ''Iddi wewe je?''
Iddi akajibu ''aanh mimi niko period''

Kipofu kwa daktari

Kipofu alipelekwa hospitali na ndugu yake kufika hospitali nesi akawaambia ''kumuona daktari ni shilingi elfu kumi''

Yule aliempeleka hospitali kipofu akajibu, ''tumekuelewa ila huyu mwenzangu ni kipofu hawezi kumuona daktari''

Friday, November 12, 2010

Mmassai na mzigo

Mmasai mmoja alipewa lifti kwenye kenta alikuwa amejibebesha mzigo kichwani. Alipopanda kwenye kenta akawa bado mzigo wake upo kichwani. Wakamuambia aushushe tu si yupo kwenye gari mmasai yule akakataa katu katu.

Thursday, November 11, 2010

Headphone

Jamaa mmoja alimuuliza mwenzake swali lifuatalo, ''kwani hizi headphones ni za kupitishia sauti?''
Mwenzake akamjibu ''ndio maana ake''
Akauliza tena ''hazichakachui unachokisikia kweli?''

Jiografia

Mtoto: Mama nikuulize swali?
Mama: Enhe mwanangu uliza tu.
Mtoto: Hivi Arusha na Tanzania ipi kubwa?

Treni

Mtoto mmoja wa kiarabu alipelekwa kusoma Ujerumani. Siku moja akamuandikia barua baba yake kama ifuatavyo:

Dear Dad,
Huku Berlin-German hali ya hewa nzuri!
Wanafunzi na walimu wananishangaa mimi nakuja na Ferrari shule wengine wote wanakuja na treni.
Wako Mwanao.

Baba nae akajibu,
Dear Son,
Nimefurahi kupata barua yako, kuhusu ferrari usijali basi na mimi ntakununulia Treni ya kwako.
Mimi baba yako.

Samaki wa kukaanga

Siku moja mtoto mmoja alienda kuogelea, aliporudi nyumbani akakuta wamepika ugali na samaki. Papo hapo akatamka ''hee!! Mama huyu samaki sio ameletwa na mzee idrisa?''

Mama akajibu ''ndio mwanangu, kwani vipo''
Mtoto akajibu tena, ''basi kama ndie aliemleta nilimuona huyu samaki alikuwa ana mimba''

Wednesday, November 10, 2010

Rubani wa ndege

Rubani mmoja wakati yupo angani baada ya muda mrefu hewani akamuita mhudumu na kumuambia ''tafuta mtu kati ya abiria akazibe pancha tairi moja kabla hatujatua...''

Gari

Jamaa wawili wakipiga stori zao za kawaida tu, mmoja akamuambia mwenzake ''ebwana si James kanunua gari bwana''
Mwenzake akanena ''aah gari yenyewe inatoa moshi utadhani inatumia kuni... Sio ishu''

Mgeni

Mtoto: Mama... Maaama!
Mama: Abee mwanangu unasemaje?
Mtoto: Eti mama, kwani baba amekuwa mgenisiku hizi?
Mama: Hapana kwani vipi mwanangu?
Mtoto: Si jana na leo memuona anaingia na mdada nyumba ya kulala wageni.

Tuesday, November 9, 2010

Ki-ndege

Jamaa alienda kuangakia sinema, alipoomba kukata ticket mbili za kuingia akaambiwa hawaruhusu kuingia na wanyama au ndege.

Akaenda pembeni akamfiche yule ndege kwenye suruali, kisha akafanikiwa kuingia ndani kuangalia sinema! Kwa vile joto lilizidi akafungua zipu ili kale kandege kapunge upepo. Humo sinema pana kigiza giza......

Dada mmoja akamnong'oneza mwenzake ''hii dudu ya huyu jamaa pembeni yangu inakula popcorn zangu''

Kukujoa hadharani

Jamaa mmoja alikua anakujoa kwenye eneo la wazi, ghafla polisi akatokea na kumuuliza '' wewe kwa nini unakojoa hadharani? Hebu fungazipo yako utoke hapo''

Yule jamaa akaanza kucheka sana baada ya kupandisha zipi yake, polisi akamuuliza ''kulikoni tena?''
Jamaa akajibu ''nimefunga zipu ila bado naendelea kukojoa ndani ya suruali.''

Sunday, November 7, 2010

Kifo cha mgonjwa

Jamaa walikua na mgonjwa wao aliekuwa amelazwa na hali mbaya! Wakaamua kumuita mchungaji aje kumuombea!

Yule mgonjwa akaomba peni na karatasi kwa vitendo, akaandika kitu akampa mchungaji. Mchungaji akakichukua na kukiweka mfukoni.

Alipokufa mgonjwa, baada ya kuzika akakumbuka ana kile kikaratasi, akakitoa na kukisoma mbele ya watu wasikie marehemu alichoandika kama ifuatavyo ''mchungaji umekanyaga paipu yangu ninayovutia oxygen''

Mjane

Mjane mmoja tajiri alibandika tangazo limeandikwa hivi ''nahitaji mwanaume mwenye sifa zifuatazo:
1. Asinipige
2. Asinikimbie
3. Awe mzima kitandani

Baada ya kupata maombi mengi siku moja akagongewa na mwanaume hana mikono wala mguu. Akamuuliza ''enhe sasa wewe ndio....''

Mwanaume akajibu, ''si unaona sina mikono so siwezi kukupiga, sina miguu siwezi kimbia''
Mjane: Na je kitandani je?
Mwanaume: We unadhani kengele nimegongaje?

Friday, November 5, 2010

Kipimo

Jamaa mmoja mlevi alienda kuomba kazi kiwanda cha wine wakam-test kwa kumpa mvinyi (wine)aonje na kufafanua ni kinywaji gani nk nk
Akapewa wine ya kwanza akaionja na kujibu, ''hii ina miaka 10, kilevi......'' nk nk
Akapewa ya pili pia akapatia vyema kabisa.

Wakaona kweli anafaa wakamuekea mkojo kwenye glass, yule jamaa alipoonja akajibu ''mkojo wa mtu mwenya miaka 21, na mjamzito wa miezi mitatu, na kama hamnipia kazi ntawatajia na baba wa huyo mtoto.''

Wednesday, November 3, 2010

Hotelini

Mr. na Mrs. Walienda hotel moja kusherekea miaka yao 50 ya ndoa. Punde kidogo wakarudi reception na mume akaanza kubwata ''hatukitaki kile chumba, hakina kiti, meza, dirisha wala choo''

Mzee wa watu akazidi bwatuka ''yaani mmetuona sie ndio wakuja sio, niitie meneja wenu haiwezekani kabisa.....''

Mhudumu akawa anajaribu kumkatisha mpaka akafanikiwa ''Mzee... Mzee... Mzee hile ni lift sio chumba mlichopewa''

Kununiana mke na mume

Mke na mume wakiwa safarini kwenye gari yao, takribani tangu waanze safari hamna alieongea neno na mwenzie. Baada ya muda mbele wakamuona nguruwe, mume akauliza ''huyo ni ndugu yenu upande gani?''

Mke nae bila hiyana akajibu, ''ndio ndugu yetu upande wa wakwe zangu.''

Neno mbadala

Mwanaume mmoja shule yake iliishia darasa la saba alienda kwa daktari na maongezi yao yakawa hivi:
M'ume: Dokta, mke wangu ni mvivu sana, nimekuja unisaidie.
Dokta: Enhe nikusaidiaje?
M'ume: Nataka unipe neno la kidaktari la kumaanisha kuwa yeye ni mvivu mnoo. Maana nkimuambia kavukavu atanijeruhi leo.

Utani huu

Mfanyakazi mmoja akiongea mbele ya wenzake chuo fulani, ''aisee mmemuona Mkuu wetu mpya alivyo na sura mbaya kama anang'oa jino?''

Mwanamke mmoja pale pembeni akadakia, ''unajua mimi ni nani?''
Mfanyakazi akajibu, ''hapana, we ni nani?''
mwanamke akajibu, ''mimi ni mke wa huyo unaemzungumzia''

Mfanyakazi: Ooh, na mimi unanifahamu ni nani?
Mwanamke akajibu: Hapana.
Mfanyakazi akanena, ''Ooh vizuri kumbe kibarua changu kipo salama.''

Monday, November 1, 2010

Kelele kwa mtoto

Mama mmoja mjamzito alipokuwa akiongea na kucheka kwa sauti na shoga yake ghafla mwanae mmoja wa miaka mitano akaja na kumuambia, ''mama usipige kelele utamwamsha mtoto tumboni.''

Kahawa

Dokta nna tatizo, kila nkinywa kahawa baada ya muda nasikia kama maumivu hivi kwenye koo.
Dokta baada ya kumfanyia X-ray nakadhalika akamuambia ''siku ingine kabla hujanywa chai hakikisha umetoa kijiko cha sukari kwenye kikombe kwanza.''

Jicho

Marafiki wawili wakiongea, mmoja akimuambia mwenzake jambo linalomsumbua!
Rashid: Ebwana mi jicho langu lanisumbua.
Ima: Linafanyaje kwani?
Rashid: Linakua kama lina kidoti hivi kwa mbele nakiona ona.
Ima: Umemuona Daktari?
Rashid: Hapana nakiona kidoti tu nlichokuambia.

Sunday, October 31, 2010

Kung'oa jino

Dokta wa meno: Nimeliona jino linalokusumbua.
Mgonjwa: Utanichaji shilingi ngapi?
Dokta: Elfu 20 tu.
Mgonjwa: Khaa yaani kwa dakika chache tu hela yote hiyo?
Dokta: Usijali, basi ntakung'oa taratiiibu mpaka mwenyewe utafurahi:

Friday, October 29, 2010

Pichu Nyeupe

Vijana wawili wakati wakiwa kwenye maongezi yao binafsi:
Daudi: naona umetoka kuoga bado kunukia sasa!
Frank: Anha kawaida yangu si unajua tena.
Daudi: Na kweli, naona umeamua kutinga chupi nyeupe kabisa.
Frank: Hehehe ukiona hivyo leo nna ki-date na mtoto mzuuri.
Dauidi: Hee! kumbe.

Thursday, October 28, 2010

Elfu tano

Mtoto: Mama naomba shilingi elfu tano.
Mama: Hapana sina mwanangu leo.
Mtoto: Basi sikuambii baba alichomuambia dada (housegirl).
Mama akatoa hela na kumpa elfu tano.
Mama: Enhe! Alimuambia nini?
Mtoto: Alimuambia asisahau kumfulia sox zake kesho.

Kuzaliwa

Mtoto: Mama kwani mimi nimezaliwaje?
Mama: Ooh, mwanangu wewe uliletwa na malaika.
Mtoto: Na je wewe na baba?
Mama: Pia sie hivyo hivyo.
Mtoto: Na Babu na bibi je?
Mama: Pia na wao.
Mtoto: Ah! Hii ripoti ntashindwa iandika maana katika familia yetu vizazi vitatu vyoote hamna kilichozaliwa.

Baloon

Mzee mmoja alipanda baloon (puto kuubwa la kuelea hewani), baada ya kuwa hewani kwa dakika kadhaa akawa hajui yupo wapi.

Akalishusha kidogo toka hewani, kicha akamuuliza kijana mmoja ''samahani eti hapa nipo wapi?''
Kijana akajibu ''ooh! Upo kwenye baloon, mita chache toka kwenye ardhi!''

Wednesday, October 27, 2010

Jambazi

Jambazi mmoja mkuu akiwauliza wenzake "nani yupo tayari kuvuna pesa?"
Wale majambazi wadogo wakajibu "sisii"
Akawauliza tena, "Je mpo tayari kwa kazi hiyo?"
Wakajibu "ndio"
Akawauliza tena "mpo tayari kufa?"
Wakajibu "ndiooo"
Mmoja wa wale wadogo akauliza "samahani uliza swali la mwisho tena?"

Pesa bank

Mmasai mmoja alienda bank kuweka hela, alipofika baada ya kuweka akasema "siweki tena pesa yangu bank" Jamaa mmoja akamuuliza "kwa nini?." Mmasai akajibu "metoka weka pesa bank mtu mwingine kazichukua, eti wanasema pesa yangu imebaki kwa karatasi."

Tuesday, October 26, 2010

Andunje

Kulikua na vijana wawili wafupi mno (emolo/andunje). Wakapata warembo kila mmoja wapo.
Wakaenda guest house.
Ilipofika asubuhi wakawa wanaulizana:

Andunje wa kwanza: Vipi mwenzangu jana ilikuwaje?
Andunje wa pili: Ilikuwa aibu sikuweza mfikia vizuri, enhe na wewe ilikuwaje?
Andunje wa kwanza: Bora wewe mie hata kitandani nlishindwa panda.

Idiot

Kwenye darasa moja la shule moja ya kizungu:
Mwalimu: Any one who is idiot asimame.
Darasa loote likakaa kimya.
Mwanafunzi mmoja akaanyoosha mkona.

Mwalimu: Enhe! Tell me what is it.
Mwanafunzi: Nashangaa wewe ndio uliesimama peke yako.

Monday, October 25, 2010

Kiwembe

''Dokta mwanangu amemeza kiwembe naomba msaada wako'' Baba akiongea kwenye simu.
Dokta ''okey nakuja, umechukua hatua gani mpaka sasa?''
Baba, ''nimeamua kunyoa kwa kutumia mashine ya umeme badala yake''

Chupi mpya

Demu: honey ninunulie chupi mpya. Unajua wanaume wenzio wananishangaa chupi zangu za kizamani!

Saturday, October 23, 2010

Kuokota

Jamaa wawili wakisimuliana jambo:
Kijana wa kwanza: Jana nlikua natembea njiani nkaokota wallet ila bahati mbaya ndani ilikuwa empty!
Kijana wa pili: Mimi pia jana hiyo hiyo nliokota sidiria ya mwanamke ila bahati mbaya ilikuwa empty pia ndani.

Mtoto kuua inzi

Mtoto: Mama, leo nimeua inzi watatu madume na wawili majike.
Mama: Enhe!? We umewajuaje?
Mtoto: Kwa sababu inzi watatu walikua kwenye chupa ya bia, na wawili walikuwa kwenye kioo cha dressng table.

Kipofu

Kipofu mmoja alikuwa ameshika gazeti amelifunua, jamaa mmoja akamfuata na kumuuliza ''kaka wewe si kipofu unawezaje kusoma gazeti?''

Kipofu nae akamjibu ''hapana sisomi gazeti naangalia picha tu''

Vichaa

Vichaa walipelekwa kwenye bwawa la kuogelea lisilo na maji wakaambiwa waingie waogelee! Woote wakaingia isipokuwa wawili, wakaulizwa mbona nyie hamuingii kuogelea?

Wa kwanza akajibu ''ntaingiaje wakati hamjanipa chupi ya kuogelea.''
Wa pili akajibu ''mimi mpaka mkinipa boya la kuelea ndo ntaingia.''

Friday, October 22, 2010

Chakula

Jamaa alipakua chakula, wakati anaenda kula mwenzake akamuuliza ''mbona humsubiri mwenzako?'' (kisa amepakua kingi)

Tuesday, October 19, 2010

Somo la Historia

Mwalimu mmoja wakati anafundisha somo la historia darasani akatamka ''natamani ningekuwa nimeishi miaka 1000 iliyopita''

Mwalimu akamuuliza, ''kwa nini?''
Mwanafunzi akajibu ''nisingekua nalisoma hili somo sasa?''

Jeneza

Siku moja tajiri mmoja alikufa na kutengenezewa jeneza la ukweli (thamani sana). Alipozikwa tu usiku wake kibaka akajitosa kufukua na kutoka nalo na kumzika bila jeneza.

Nje kwenye geti akakutana na askari waliokua doria.

Askari: Wewe unafanya nini huku? Unazika watu usiku? Na hilo Jeneza umelibeba kwa nini?
Kibaka: Nimewaambia ndugu zangu nataka kuzikwa Ilala wao wamenizika Kinondoni, nimeamua kwenda mwenyewe kutoka.
Polisi walilala mbele (walikimbia wote).

Monday, October 18, 2010

Ndege imeelemewa!

Ndege moja angani ilielemewa, wakapunguza mizigo kwa kuitupa bado haikusaidia. Ikabidi wapunguze abiria, rubani akasema ''tutaita ALPHABETICALLY''

All Africans... Watu kimya!
All blacks... Watu kiimya!
All Caribean... Watu kimya!

Mtoto akamuuliza baba yake ''baba kwani sisi sio waafrica?'' Baba akajibu, ''shhh kuanzia sasa sisi ni Zanzibarians''

Sunday, October 17, 2010

Sigara

Kijana mmoja alienda duka moja na kuuliza:
Kijana: Samahani unauza sigara moja moja?
Muuzaji: Hapana ni kwa pakti tu.

Jamaa akaondoka, kesho yake na kesho kutwa akaja tena. Siku ya mbele yake akaamua kujiandaa!
Alipofika muuzaji akamjibu:

Kijana: Samahani unauza sigara moja moja?
Muuzaji: Ndio.
Kijana: Shilingi ngapi?
Akatajiwa na jamaa akafungua pakti moja na kumuuliza.

Muuzaji: Unataka ngapi?
Kijana: Nataka 20.
(pakti moja inabeba sigara 20)

Ajali

Dereva mmoja alimgonga mwanamke mmoja barabarani. Wakati anaulizwa hali ikawa hivi:
Raia wa kawaida: Sasa hapa nani mwenye makosa?
Dereva akajibu: Mwanamke.
Raia: Kwa nini unasema mwanamke ndio ana makosa?
Dereva: Kwanini amekuja barabarani badala ya kuwa joikoni?

Mkate

Mteja: Habari? Nipatie mkate.
Dukani: Unataka upi? Mweupe au Wa brown?
Mteja: We nipe wowote nae mnunulia ni kipofu.

Mtoto na babu!

Mtoto alikua amekaa kibarazani na babu yake.
Mtoto: Babu nikuulize swali la kizushi?
Babu: Uliza mjukuu wangu.
Mtoto: Unaikumbuka siku ya kwanza uliyo-kiss?
Babu: Mjukuu wangu hiyo ya mwisho tu siikumbuki sembuse ya kwanza!!

Saturday, October 16, 2010

Miguu ya chura

Jamaa aliingia kwenye restaurant ya wachina akamuita mhudumu na kumuuliza, ''aisee una miguu ya chura?''
Mhudumu akajibu ''ndio mkuu''
Mteja: Okey basi ruka mara moja hapo mtaa wa pili ukanichukulie sigara tatu.

Toilet paper

Jamaa alienda nunua toilet paper, mkewa akamuuliza ''sasa mbona umenunua nyeupe tuu mi nilitaka za rangi?''
Mume akajibu: Za rangi ni gharama kidogo ntazipaka rangiz hizi hizi nyeupe usiwe na wasiwasi.

Watalii

Mtalii mmoja alitekwa bahati mbaya na watu porini asiowajua, akaulizwa ''what is your name?''
Mzungu yule mtalii akanena na yeye ''kwa nini mnataka kujua jina yangu?''
Mmoja wa watekaji akajibu ''ni kwa ajili ya menu ya leo''

Kuibiwa

Jamaa mmoja aliamka usiku mkubwa akaenda sebuleni kuchukua betri aweke kwenye tochi.
Alipoweka tu na kuwasha akakutana na kibaka ndani ya nyumba yake.
Kibaka: Nimekuja kukuibia kaa kimya...
Mwenye Nyumba: Oh! Okey mi nazima tochi naenda kulala ukipata kitu chenye thamani niamshe nkusaidie kubeba!

Mapenzi

Mwanamke akiwa dakika za mwisho hoi hospitalini akimuambia mumewe.
Mwanamke: Mume wangu niahidi utatafuta mwanamke mwingine nikifa.
Mwanaume: Nakuahidi mke wangu.
Mwanamke: Utampa jaketi langu alivae uwe unanikumbuka?
Mwanaume: Mhh! Mbona lile jacket halimtoshi ye mnene kidogo.

Kutoroka

Wafungwa wawili walipanga njama za kutoroka:
mfungwa wa kwanza: Tufanye hivi tukifika pale getini si kuna ukuta? Halafu tunapanda na kuruka.
Mfungwa wa pili: Anha! Tuchimbe chini kwa chini ndio.......!

Wakaamua wachukua choice one, walipofika eneo la geti kubwa mmoja kati yao akasema ''shenzi kumbe hamna ukuta!!''

Ugonjwa wa kusahau

Mwanamke: Dokta nimekuja nna tatizo, mume wangu ana tatizo la kusahau sana.
Dokta: Ooh! Nini dalili za hilo tatizo alilo nalo?
Mwanamke: Akiona mwanamke mzuri tu anasahau kua ameshaoa!

Kununua maua

Jamaa mmoja alikua akienda duka la maua kila siku ya ijumaa kununua ua/maua!
Muuza maua: Unayapenda maua yetu eenhe?
Alimuuliza jamaa kwa ujio wake.
Jamaa: Hii ndio mara ya mwisho nanunua maua hapa.
Muuzaji: Kwa nini tena?
Jamaa: Kwa sababu kuanzia kesho ntakua nimeshaoa!

Hii tamu

Jamaa mkewe alijifungua mapacha!
Jamaa: Ebwana mke wangu si kajifungua mapacha bwana!
Rafiki: Mbona jambo la kawaida ndugu yangu.
Jamaa: La kawaida ndio lakini swali sijajua yule pacha mwingine ni mtoto wa nani?

Thursday, October 14, 2010

Jani

Mtoto mmoja alienda na mama yake kwenye makumbusho ya picha na sanamu mbalimbali. Punde akaona Sanamu moja ikiwa uchi kasoro sehemu nyeti ikiwa imefunikwa na jani la sanamu na lenyewe, mama yake akamuuliza ''mbona hautokia hapo?''

Mtoto akajibu, ''nasubiri hili jani lianguke''

Kuku wadogo

Dogo mmoja alienda restaurant na kuagize kuku!
Akamuambia mhudumu ''aisee nletee kuku sio mkubwa mwili wangu sio mkubwa, nataka kuku mdogo tuu''

Mhudumu akaenda andaa mlo na alipomletea akamletea mayai mawili kwa kigezo cha kuku wadogo.

Wednesday, October 13, 2010

Vichaa watatu

Vichaa watatu walitoroka hospitali ya vichaa:
Wakaanxa ulizana wakati wapo nje
Wa kwamza: Eti saa hizi mchana au usiku
Wa pili: Itakuwa usiku kwani lile jua au mwezi?
Wakamuuliza mwenzao ''eti we unaonaje maswali yetu?''
Akawajibu ''mie sio mwenyeji hapa''

Tuesday, October 12, 2010

Kupima macho

Jamaa mmojaalienda kupima macho, wakati yupo kwa daktari akavishwa lenzi ili aweze kusoma maandishi madogo yaliopo kwenye ubao:

Dokta: Haya soma haya maandishi yaliyopo kwenye huu ubao.
Mgonjwa: Ubao gani dokta?

Mzigo umevuka

Kulikuwa na jamaa mmoja alikuwa tall kweli kweli kiasi kwamba vitanda vya shule ya bording miguu inavuka kitanda.

Siku moja wanafunzi wenzake wakamfunga kitambaa chekundu miguuni eti mzigo umevuka body ya gari/lori. (mithili ya lori inavyokuwaga).

Sunday, October 10, 2010

Volks Wagen

Mama mmoja alisimamishwa na traffic police kwa kosa la kupita njia ambayo hairuhusiwi akiwa na gari aina ya Volks Wagen (mgongo wa chura) akajibu, ''traffic jaman gari lenyewe dogo halijui kitu''

Riadha

Daah! Aisee nimekimbia mita 500 kwa sekunde thelathini. Jamaa mmoja akimuambia mwenzake. Mwenzake nae akamjibu ''haiwezekani kwani hata mwanariadha wa dunia hawezi hiyo kitu''

Jamaa akamjibu: Si nimegumdua shortcut way.

Friday, October 8, 2010

Mboga

Wasukuma walienda kumtembelea mkwe wao, wakaletewa viazi nyama. Maongezi yao yakawa hivi:
Msukuma wa kwanza: Tumeenda kwa mke wa K si akaturetea mboga tupu.
Jamaa anaesimuliwa akanena: Kwa nini?
Msukuma akajibu: Si hatukuona ugari.

Kitambi

Mtoto akimuuliza mama yake, ''mama... mama... Kwani mimba ya baba nani kampa?''
Akimaanisha kitambi.

Thursday, October 7, 2010

Hii nayo...

Mtoto: Mama eti mtoto anazaliwa pale baba anapoingizaga dudu yake.
Mama: Ndio mwanangu.
Mtoto wa kike mae akadakia, ''sasa meno je hawezi yang'oa kweli?''

Kaka na Dada

Kaka ma dada wakiangalia tv, kaka akawa ma hamu ya kufanya mapenzi akamuambia dada yake.
Dada akajibu, ''wewe mi si dada yako?''
Kaka akanena, ''so what?''

Kaka akazidi bembeleza mpaka waka-do.
Walipomaliza kaka akamuuliza vipi ume-enjoy?
Dada akajibu ''sio tamu kama nikiwa na babu yeye zaidi''

Sukuma gari

Mtoto: Mama kwa nini tunaisukuma gari ya baba tu tuwashe tuondoke.
Mama: Shhh... Utamuamsha baba yako.

Tuesday, October 5, 2010

Annivessary

Mume alimnunulia tiket ya ndege kwenda Peru siku yao ya annivessary, mke akamuuliza mumewe ''enhe mume wangu annivessary ijayo utaninunulia nini?''

Mume nae akamjibu: Ntakununulia ticket ya kurudi (return ticket).

Pombe bwana

Jamaa mmoja alirudi kwake, alipofika sebuleni akawa analigonga gonga lile bwawa dogo la kioo la kufugia samaki. Mkewe akamuuliza ''unafanya niniz?'' Jamaa akajibu ''nawazuia hawa samaki wasinibwakie (kama mbwa)''

Sunday, October 3, 2010

Kumuona daktari

Jamaa alienda zahanati moja alikuwa anaumwa, akaambiwa kumuona daktari ni shilingi elfu mbili.
Jamaa akadakia na kujibu ''sina hiyo elfu mbili ntafumba macho nsimuone ili insilipe.

Friday, October 1, 2010

Wizi

Mama mmoja aliambiwa mwanae ameuwawa kwa sababu ya wizi akajibu hivi, "maskini Tarimo alikua anafanya kazi ya ujambazi akiniletea pesa za kuishi, sasa hiyo kazi ya wizi ameanza lini tena?"

Kipofu

Jamaa mmoja alikuwa amekaa sehemu na rafiki yake kipofu, sasa wakati wanatwanga stories yule kipofu akamuuliza mwenzake asiye kipofu, "hivi umeiona movie mpya ya Kanumba? Aisee kali acha."

Godoro

Jamaa alikua anamfukuza mtu alietoka na godora lake kwake. Mfukuzwaji alipoona jamaa bado anamfukuza akaingia kituo cha polisi.
Polisi: Wewe vipi na godoro?
Jamaa: Kuna mtu ananifukuza mi mwizi wake.

Mwenye godoro akafika, "samahani polisi huyu ni ndugu yangu ana matatizo ya akili kidogo naomba niondoke nae tafadhali."

Jamaa: Hapana jamani mimi mwizi wake nimemuibia hili godoro.....

Wednesday, September 29, 2010

Mende

Kuna jamaa mmoja alienda kula kwa mama ntilie, kumega tu tonge la kwanza akakuta mende maongezi yao yakawa hivi:
Jamaa: Ebo nimekula mende kwenye chakula changu.
Mama ntilie: usijali, tutakutoza tu pesa ya chakula, huyo mende ni bure

Saturday, September 25, 2010

Eskot

Jamaa alienda kuomba escort ya polisi. Akaulizwa "umebeba billion ngapi au umetishiwa life?"
Akajibu "No napita na kitimoto msikitini".

Wednesday, September 22, 2010

Talaka

Mwanaume: Rafiki yangu mi nataka mpatia mke wangu talaka.
Rafiki: Kwa nini tena?
Mwanaume: Kila nkirudi nyumbani nakuta kaficha mwanaume kwenye kabati la nguo.
Rafiki: Oh! Hiyo mbaya sana.
Mwanaume: Yaani nakosa nafasi ya kutundika nguo zangu kabisa.

Kwenda ulaya

Mtoto: Mama mi niliwaomba tangu mdogo kwenda ulaya.
Mama: Usijali mwanangu ngoja ngoja kidogo.
Mtoto: Ningoje mpaka lini? Sa ivi tangu mdogo ningekua nimeshakaribia kwa kutembea kwa mguu.

Tuesday, September 21, 2010

Kichekesho

Mtoto akimuambia mama yake, "mama nikusimulie kichekesho ucheke?
Mama: Ndio mwanangu nisimulie nasikiliza.
Mtoto: Haya anza kucheka kwanza.

Airport

Rubani mmoja wa ndege alipotua ndege na kumuuliza mwenzake, "leo tumetua kiwanja gani mbona tambarare kubwa na hata nyasi hamna...?"

Rubani wa pili akamjibu, "kwa sababu tumetua juu ya bahari."

Airport

Rubani mmoja wa ndege alipotua ndege na kumuuliza mwenzake, "leo tumetua kiwanja gani mbona tambarare kubwa na hata nyasi hamna...?"

Rubani wa pili akamjibu, "kwa sababu tumetua juu ya bahari."

Picha ya thamani

Wakili mmoja alimfuata kingunge mmoja na kumuambia.
Wakili: Mzee nna habari nzuri na mbaya za kukupa.
Kingunge: Oh! Okey, anza na nzuri.
Wakili: Mke wako amepata picha yenye thamani ya milioni 10.
Kingunge: Oh! Safi sana. So nini tatizo?
Wakili: Ni picha yako upo na secretary.

Mchumba

Kijana mmoja alienda soma nje miaka mitano. Akaoa huko huko, siku aliyorudi Tanzania akaja na mkewe akamtambulishe kwa wazazi wake.

Siku aliyoenda alikuwa na rafiki zake watatu, wawili kati yao wasichana.
Akamuambia mama yake ajaribu mtambua yupi ndio mkwewe.

Mama akamnyooshe mlengwa.
Jamaa akauliza, "hee! Mama umemjuaje kama ndie huyu?"
Mama: Nimechukia tangu nlipomuona.

Adhabu!

Mtoto wa miaka mitano siku moja alimuona mama yake akiwa na baba yake kwenye majamboz, mtoto akamwambia mama yake "aanha! Kumbe mimi unaniadhibugi kwa kukinyonya kidole gumba changu."

Ngazi

Mama na mtoto wakipandisha ngazi kwenda ghorofa ya kumi kwenye apartment yao, lift ilikuwa mbovu siku hiyo.
Mtoto: Mama nikuambie kitu...
Mama: Embu nyamaza.
Mara ya pili ivoivo akajibu.
Ghorofa ya 10 huku wakiwa hoi kwa kuhema.
Mama: Enhe ulikuwa unasemaje?
Mtoto: Nlikua nataka kukuambia nimesahau ufunguo kwenye gari wa mlango.

Ujauzito

Mtoto mmoja alimuuliza mama yake mjamzito "mama... mama... Asa we unafanyaje huyo mtoto tumboni akianza kulia?"

Kuhesabu.

Watoto wakihesabu mpaka kwa kidhungu mpaka 10.
Wa 1: Akishia 4.
Wa 2: Akafikia 6.
Wa 3: Akahesabu mpaka 10. Alipoona watu wanamuangalia kwa uwezo wake mzuri akaendelea ...prince, queen, king... Nk

Mtoto wa kike

Mtoto alikutana uso kwa uso na wazazi wake waki-do, baba akamwambia "oh! Mwanangu, tunamtengeneza mdogo wako wa kike"

Siku moja baba alirudi home na kukuta mwanae akilia akamuuliza, "unalia nini?"
Mtoto: Yule mdogo wangu uliekimtengeneza jirani yetu memuona akimla.

Sumu!

Jamaa alipiga simu kwa daktari:
Jamaa: Dokta mke wangu amekunywa sumu yangu yote halafu anajidai amelala, nisaidie nifamnyeje aamke?

Mooo!

Ng'ombe wakiongea.
Ng'ombe 1: Ng'ombe wenzako wote tunalia mooo! Wewe mwenzetu unalia meee!
Ng'ombe 2: Nlisahau waambia, najifunza lugha mpya.

Toothpick

Mteja kaingia bar.
Mteja: Mhudumu njoo. Habari yako?
Mhudumu: Nzuri tu karibu.
Mteja: Mna toothpick?
Mhudumu: Unataka ya baridi au moto?
Mteja: Namaana vijiti.

Vichaa ndegeni.

Ndege moja ilibeba vichaa, sasa walikuwa na kelele. Baada ya muda kidogo msimamizi wao akatokea kwa rubani na kumuuliza mmoja.
Msimamizi/mwangalizi: Wewe! Wenzako wakwapi?
Kichaa akajibu, wanakelele sana wapo hapo nje nimewatoa kidogo.

Monday, September 20, 2010

Ajali

Ilitokea ajali, jamaa mmoja alikatika mkono akawa analia.
Mwingine akasema, "we mkono tu unalia, mbona huya aliekatika shingo halii?"

Mjusi

Mjusi mmoja alikuwa amesimama kwenye siling board. Ghafla akapiga chafya... Punde akapiga chafya... Alipokaribia kupiga ya tatu si akaacha kujishika azibe pua, akaanguka.

Jino na ganzi!

Jamaa alienda kung'oa jino, sasa ganzi haikuingia vzuri.
Wakati daktari anamng'oa si jamaa na yeye ananyanyuka nalo. Mchezo ulikuwa huo bwana mpaka kumaliza hoi.

Sunday, September 19, 2010

Kama siafu

Mental mmoja alikua ghorofa ya 50, chini kulikua na mwanamke mnene. Alikua akimuona mdogo kama siafu.
Akashuka ghorofa kadhaa kwa awamu uku akizidi muona mkubwa. Alipofika chini akaenda mkumbatia.
Mdada mnene: We ni nani?
Mental: Nimekufahamu tangu mdogo kama siafu.

Ze fumanizi

Mwarabu mmoja alimfumania mke wake aki-do na mkewe.
Rafiki: Sasa ukamfanya nini?
Mwarabu: Sa ningefanya nini na sijui english.

Sumu

Mume alienda pharmacy.
Mume: Mke wangu anataka kujiua.
Pharmacy: Vipi nikuitie ambulance?
Mume: Nahitaji sumu nkampatie.

Mke|Ajali

Dokta: Mkeo ameumia sana kwa ajali, itabidi umlishe, umuogeshe, msalani.
Mume: Maskiini.
Dokta: Usijali, nkikutania. Amesha kufa

Mapacha bar

Mapacha wawili walienda bar, pembeni kulikuwa na mlevi kalewa akasema alipowaangalia "holly shit i think i see everthing double!"

Ku-do

Wanandoa wawili walisahau funga mlango wakati wana-do. Mtoto wao akaingia, baba akasema "oh, mwanangu najaza upepo kwenye mapafu ya mama yako"

Mtoto akajibu, "haja jana yule mbaba jirani alisahau kufunga wakati anamjaza upepo mama mdomoni."

Inzi

Inzi karibu kumi walikuwa wamekizonga kinyesi cha mbwa. Ghafla mmoja akajamba, mwingine akasema "we huoni ka tunakula hapa?"

Jogoo mfupi

Jamaa: Dokta nimekuja, Jogoo wangu mfupi, kwa nini hafiki mpaka miguuni.
Siku iliyofuata akaamka akajikuta hana miguu.

Kuungama

Kijana alipoenda kwa Padre, "nimekuja kumuungamia dhambi rafiki yangu."
Padiri akauliza, "kwa nini asije mwenyewe?
Kijana akajibu, "aah Rashidi ni muislamu."

Kuungama

Kijana alipoenda kwa Padre, "nimekuja kumuungamia dhambi rafiki yangu."
Padiri akauliza, "kwa nini asije mwenyewe?
Kijana akajibu, "aah Rashidi ni muislamu."

Dokta.

Fundi bomba alikuja tatua tatizo moja kwenye nyumba moja.
Fundi: Shughuli nzima itagharibu laki mbili.
Mama: Haa! Mume wangu tu ni dokta hatengenezi hiyo pesa kwa saa.
Fundi: hata mimi nlikuwa napata kidogo wakati nlipokuwa dokta pia.

Boxing

Jamaa mmoja alienda kuangalia boxing (ndondi). Alikaa pembeni mwa kocha mmoja wa ndondi, kocha akamuambia jamaa "unaonaje ukijiunga na boxing? Utatengeneza pesa nzuri sana."

Jamaa akajibu, "haina shida, umejuaje kama mi ni dokta wa meno?"

Pikipiki | Gari

Mmiliki gari: Natumia pesa mingi kwa ajili ya mafuta ya gari. Wewe je mwenzangu?
Mmiliki pikpik: Natumia pesa mingi ku-repear kati ya mimi au pikpik.

Alama barabarani.

Traffick polisi alimsimamisha dereva alievuka kibao cha kuonye asimame.
Polisi: Hujakiona kile kibao usimame?
Dereva: Nilikiona, isipokuwa sikukuona wewe.

Nimesahau bukta

Jamaa mmoja alienda nyumba moja kugonga. Mlango ulipofunguliwa akaulizwa na mwanaume aliemfungulia mlango, "nikusaidie nini kijana?"

Kijana akajibu, "samahani kwa usumbufu ila nimekuja nimesahau bukta yangu ya ndani chumbani kwa mkeo?"

Saturday, September 18, 2010

Bado mna?

Frank: James hivi bado unam-date Lily?
James: Hapana.
Frank: Oh! Nlitaka nkuambiage zamani bora umemuacha maana ni mbaya hana mpango kabisa.
James: Hatu-date tena kwani nimemuoa tayari.

Inzi

Jamaa alishikwa na hasira alipokuta inzi kwenye supu yake akamuita mhudumu.
Mteja: Unaona nini hii?
Mhudumu: Oh! Usijali ameshakufa nimewapulizia dawa wote jikoni.

Siafu

Kwenye ndege kwa mara ya kwanza alipanda. Akaangalia nje.
Ima: Ona ona binadamu wadogo kama siafu.
Doto: Wee hao ni siafu kweli bado hatujapaa

Funga mkanda

True story:
Siku moja traffic polisi alipewa lift. Lilipofika suala la kufunga mkanda sasa... Mara aupitishe nyuma ya shingo, mara mgongo... Ilihitajika msaada maana ni aibu.
Kumbe wapo wasiojua kazi kuagiza/kuuliza tu.

Na bibi.

Baba mmoja karudi home kakuta mwanae anafanya mapenzi na bibi yake, "we mtoto umekosa adabu kabisa..."
Mtoto: Kumbe inauma enhe! We unavyofanyaga na mama yangu je?"

Toothpick

Jamaa mmoja restaurant baada ya kumaliza mlo. Akatafuta toothpick atoe nyama kwenye meno, hakufanikiwa. Meza ya pili jamaa alikuwa anacho kimoja anatakitumia akamuambia "kaka samahani ukimaliza hicho niazime pia"

Mimba

Mtoto alimuuliza mama yake?
Mtoto: Eti mama, kwani baba atajifungua lini?
Mama: Kwa nini umeuliza mwanangu?
Mtoto: We huoni tumbo lake kama hili la kwako?

Fumanizi

Jamaa alimuuliza rafiki yake, "utafanya nini ukimfumania mkeo na njemba?"
Jamaa akajibu, "ntamnyoa kwa chupa, na kuivunja vioo ile gari yake nyekundu."

Maiti

Ndege ilikuwa inasafirisha maiti. Bahati mbaya ilianguka na waliomo ndani wote wakafa. Jamaa mmoja kwa masikitiko aliposikia hiyo taharifa akasema, "maskiini, sasa maiti si imekufa tena?"

Kuchelewa kazini

Bosi: Imekuwaje leo unafika muda huu kazini? Umechelewa sana! Ni nini foleni au?
Mwajiriwa: Bosi nisame, yule jogoo anaewika kila siku alfajiri ameuzwa.

Friday, September 17, 2010

Ya leo ndogo

Mtalii alienda restaurant, meza ya jirani akaona jamaa anakula mlo akauli ile nini akajibiwa ni korodani za ng'ombe.

Akaomba aletewe akaambiwa ziliwepo hizo mpaki wiki ijayo kwenye mashindano ya ng'ombe dume na binadamu.

Siku ikafika mtalii akaenda ili awahi oda yake, alipoletewa akauliza "mbona za leo ndogo sio kama za siku ile?"
Mhudumu akajibu, "leo ng'ombe dume ndio kashinda."

Tafuta mke

Jamaa wawili waligongana supamaketi bahati mbaya.
Wa1: Samahani kaka.
Wa2: Bila samahani, namtafuta mke wangu!
Wa1: Mimi pia vivyo hivyo.

Wa2: Mke wako yupoje?
Wa1: Mwembamba, mrefu hivi. Wa kwako je?
Wa2: Agh! Tuache tu, tumtafute wako kwanza.

Spidi ndogo na kubwa

Gari moja ilikuwa spidi ya 50kph, ingine ikapita kwa spidi ya 150kph. Mwisho wa siku wote wakajikuta Majerui hospitali.
Wa 50kph: Vipi tena?
Wa 150kph: Ajali bwana. Je, wewe si ulikuwa slow mbona upo hapa!?
Wa 50kph: Ulivopita nkajua injini yangu imezima nkashuka nkaangalie kumbe inatembea.

Ndege itilafu

Ndege angani ilianza sumbua | itilafu, ma-pilot (Rubani) wakavaa parashuti kujiandaa kuruka wakawaambia abiria "tunakuja tunaenda omba msaada kidogo."

Swali

Josh: Rafiki yangu nna swali nataka kukuuliza!
Sam: Uliza tu mi na wewe tena.
Josh: Hivi lile kovu kwenye paja la mkeo aliumiaga?

Mvuto

Aliingia bar mwanamke mzuri. Jamaa mmoja akamuambia mwenzake "aisee nimemfuatilia yule dada mwaka sasa na zaidi"

Mwenzake akajibu "mh" lakini wewe si ni shoga?"
Akamjibu tena "ndio najua, nataka aniunganishie kaka yake."

Wednesday, September 15, 2010

Baba!

Mtoto: Mama eti ni kweli Mungu ndio anatupatia maji na chakula?
Mama: Ndio mwanangu.
Mtoto: Sasa baba wa nini tena?

Gari usiku

Juma: Mi nashangaa watu wanawezaje endesha gari usiku.
George: Unamaana gani?
Juma: Najiuliza wanawezaje kujua|kuingiza gia kwenye giza?

Mapenzi

Mume: Mke wangu leo tujaribu kitu mupya.
Mke: Kweli mume wangu, twende kwenye garden park leo tuka-do.

Mume akakubali, walipofika eneo polisi nae akatokea kabla hata hawajaanza. Polisi akawadai faini Mume laki moja, mke laki tatu.

Mume: Haiwezekani, kwa nini mke wangu adaiwe zaidi?
Polisi: Kwa sababu huyu mwanamke ni mara ya tatu namnasa hapa akifanya ngono.

Tuesday, September 14, 2010

Museum

Mwanamke mmoja alienda museum, punde akaona taswira siyo. Akamuita mhusika wa pale "kaka haiwezekani, unataka kuniambia hii art?"

Mwanamke: Mbona hata hamna mvuto.
Mtu wa museum akajibu kwa upole, "mama hiki kinaitwa kioo"

Mke kupotea

Mtu na mchumba walienda kariako, punde jamaa akawa hamuoni mchumba wake. Akajaribu mtafuta bila kumpata.

Akamfuata mdada mwingine mrembo, "dada unaweza ukaongea na mimi kidogo?"
Dada akajibu "hapana, kwanini?"

Jamaa: Namtafuta mchumba wangu, akiniona naongea na msichana mzuri kama wewe atakuja tu."

Mapacha

Mwanamke mmoja alipanda daladala na watoto wawili.
Dereva: Hawa ni mapacha?
Mwanamke: Hapana, kwa nini?
Dereva: Siamini tu kama hujatumia condom mara mbili.

Mapacha

Mwanamke mmoja alipanda daladala na watoto wawili.
Dereva: Hawa ni mapacha?
Mwanamke: Hapana, kwa nini?
Dereva: Siamini tu kama hujatumia condom mara mbili.

Monday, September 13, 2010

Jino

Jamaa alienda kwa dokta, "dokta nimekuja na jino la ng'ombe u-replace pale uliponing'oa jana."

Sunday, September 12, 2010

Pikipiki

Idd: Kaka nimenunua pikipiki jana bwana.
Ali: Oh hongera sana. Je ni left hand au right hand?

Supu

Mzee mmoja alienda pata mlo restaurant.
Mzee: Hii supu mbona sio nzuri kama ya jana.
Mhudumu: Mh! Muongo mbona ndio ile ile ilobaki jana?

Muokoaji

Meli moja ya watalii moja wakati inapita walimuo mtu anahangaika kwenye maji yenye kina. Kila mtu akawa anaogopa kujitosa akamuokoe.

Ghafla jamaa mmoja akajitosa na boya la kuogelea akamuokoa.
Walipopandishwa kwenye meli akapewa kipaza sauti aongee kwa ujasiri alioufanya. Akashika kipaza sauti na kusema "namtaka alienisukumia kwenye maji"

Mwizi

Mwizi: Dokta malaria bado nnayo.
Dokta: Dawa nlizokupa ulimeza zote?
Mwizi: Zile ulizonipa nimeziiba, labda unipe zingine.

Karata

Wacheza karata:
Wa 1: Mambo gani ya kulowesha lowesha karata na mimate sasa. wa 2: Si umenipa jokeri ukasema nilambe karata tano!

Saturday, September 11, 2010

Chai

Jamaa mmoja mgahawani akinywa chai ghafla akaja jamaa mbabe mmoja na kuinywa chai yake, akanena "kaka sio vizuri hivyo."

Kisha akaendelea kusema, "leo nimefukuzwa kazi, wiki iliyopita mama yangu kafa, nimemfumania mke wangu na mwanaume, leo nataka kujiua umekunywa sumu yangu kwenye chai."

Vibonge

Kulikuwa na vibonge wakiongea.
Kibonge 1: Unene wangu mpaka mlangoni nashindwa kupita.
Kibonge 2: Unene wangu mpaka nashindwa panda daladala.
Kibongo 3: Unene wangu nilikuwa naanika chupi jirani yangu akaniuliza "unaanika tent?"

Walevi|Simba

Walevi wakitoka kulewa huko kijijini walimuona simba, mmoja akapanda mti. Wa pili akauzunguka mara kadhaa halafu akamuambia mwenzake "usiogope nipo mbali sana nshauzungu mti mara 6 nipo mbali sasa hawezi nifikia."

Zawadi ya besdei

Mke alimletea mumewe chuka kama zawadi kwenye birthday yake.
Mume akaduwaa, hii nini sasa...
Mke akamuambia "usishangae mume wangu hiyo ni zawadi nzuri sana"

Usiku wakati amelala akastuka akakuta chura nanyonya kwa ustadi naniliu ya jamaa.

Asubuhi alipoenda jikoni huku amemshikilia chura mkono mmoja, mkono wa pili kitabu cha mapishi. Mke akamuuliza, "enhe imekuwaje usiku? Zawadi nzuri?"

Mume akajibu, "namfundisha chura jinsi ya kupika, wewe paki nguo zako uondoke"

Picha ukutani.

Jamaa mmoja alikuwa chumbani kwake akitafuta pa kuweka picha ukutani. Alipopata wakati ana-drill ukuta ghafla akasikia kelele toka kwa jirani yao.

Akamtuma mwanae akaangalie kuna nini. Aliporudi akamuuliza mwanae, "enhe kuna nini?"
Mtoto: Umemtoboa mkono.

Goroli

Jamaa mmoja alienda kwa dokta:

Jamaa: Dokta golori yangu moja kubwa ingine ndogo mpaka marafiki zangu wanicheka.
Dokta: Ebu tuone.
Jamaa akashusha zipu kusha suruali...
Golori ya jamaa moja ikagusa mpaka chini.
Dokta akaanza kucheeka mpaka akagalagala.

Jamaa akamuambia dokta "sasa dokta hapo hujaiona kubwa yake"

Ombaomba

Omba omba mmoja alimuomba hela jamaa njiani.
Jamaa: Samahani huwa sitoagi hela mitaani.
Ombaomba akajibu, "sasa nifanyeje? Nifungue ofisi?"

Kadi ya ATM

Jamaa alipoteza atm kadi: "Nimepoteza ATM kadi yangu, kizuri ni kwamba huyo mwizi hatotumia pesa nyingi kama mke wangu."

Wallet

Restaurant
Ali: Jamani nimedondosha wallet ina laki tatu. Atakaeiona ntampatia elfu hamsini.
Jamaa mwingine humo humo restaurant akasema, "Yeyote atakaeileta kwangu ntampa laki moja."

Vidonda vya tumbo

Dokta: Mama inaonekana una vidonda vya tumbo.
Mume: Sasa dokta tusaidie, je plasta tutabandikaje? Au atakiwa aimeze?

Pipi utaoza meno

Chumba cha kupanga kimoja:
Mama: Mwanangu usile pipi meno yataoza.
Mtoto: Mbona mama we usiku unamnyonyaga baba mpaka anatoa gundi, huogopi?

Friday, September 10, 2010

Kipofu

Kipofu mmoja aliingia supermarket na fimbo ya kumuongozea. Mule supermarket kulikuwa na tangazo kubwa limeandikwa '50% OFF'
Kipofu akasema "mbona lile tangazo mmebandika ndani sasa, halafu maandishi yake yanaumiza macho?"

Furaha

Mwanajeshi mmoja alipoze mkono mmoja vitani. Akawa anataka jiua. Wakati yupo tayari akaona mtu mwingine ana mkono mmoja akiruka ruka...

Akaenda muuliza, "mbona kama una mkono mmoja unaruka ruka kwa furaha?"
Jamaa akajibu "nani kakuambia nna furaha? Ni nyuki kaning'ata tako."

Zima moto

Askari mmoja wa zima moto alienda nyumbani kwake na kumuambia mkewe "mke wangu tuwashe moto nyumba yetu nifanye mazoezi ya kuzima moto, siku nyingi sijazima moto."

Kuogelea

Mtu na msichana wake walikuwa beach.
Mwanamke: Njoo tuogelee mpenzi.
Mwanaume: Nibebe na condom?

Mwandishi wa habari

Mwandishi mmoja wa habari alikwama kwenye foleni kubwa iliyosababisha hiyo foleni. Akaamua atumie muda huo kushuka akachukue habari ya kuifanyia kazi...

Basi akapenya penya kwenye umati wa watu ili aone na kufanya kazi ya uandishi akakuta aliegongwa ni ng'ombe.

Paka!

Jamaa mmoja alisikia mlango ukigongwa, alipofungua akakuta jamaa amembeba paka.
Akamueka chini, paka akawa anaruka ruka huku na huko akaangusha whisky na glass. Mwenye nyumba akamfuata jamaa aliekua akiondoka akamuambia "siku ingine usije na paka kwangu"

Jamaa akajibu, "sio wangu mi nimemkuta mlangoni kwako akitaka kuingia nkajua wako."

Thursday, September 9, 2010

Kisima

Mgeni rasmi alipoenda zindua kisima si akachungulia kisimani kisha akauliza, "hee mmeshaanza kufuga na mamba humu?"
Kumbe kajiona sura yake.

Kisima

Mgeni rasmi alipoenda zindua kisima si akachungulia kisimani kisha akauliza, "hee mmeshaanza kufuga na mamba humu?"
Kumbe kajiona sura yake.

Tofauti kati ya...

Mtoto aliulizwa, "tofauti kati ya baba na mama ni nini?"
Mtoto akajibu "baba ni mlevi mama ni mpole."

Wednesday, September 8, 2010

Funguo ya pingu

Mtoto mmoja baba yake askari magereza, alienda na kumuambia baba yake, "baba naomba ufunguo wa pingu?"
Baba kwa mshangao akauliza "enhe! Za nini?"
Mtoto akajibu, "si kuna wafungwa wawili wapo nje wametoroka jela."

Funguo ya pingu

Mtoto mmoja baba yake askari magereza, alienda na kumuambia baba yake, "baba naomba ufunguo wa pingu?"
Baba kwa mshangao akauliza "enhe! Za nini?"
Mtoto akajibu, "si kuna wafungwa wawili wapo nje wametoroka jela."

Open roof

Traffic mpya kazini siku moja aliona gari kwa mbaali inakuja akaisimamisha. Gari husika ilikuwa open-roof... Kwa vile ilikuwa mara ya kwanza kuliona akamuuliza dereva "...hii gari yako mbona imeng'oka paa?"

Tuesday, September 7, 2010

Jino

Jamaa alienda kwa mtaalamu wa meno, alipofika akafungua zipu ya suruali na kutoa naniliu... Dokta akasema "e-e-e! Mimi sio... Mimi ni dokta wa meno."
Jamaa akajibu, "najua, kuna jino limenasia kwenye naniliu yangu"

Juisi ya papai

Josh: Dokta kaniambia ninywe juisi ya papai baada ya maji ya moto ya kuoga.
Fred: Je imekusaidia?
Josh: Hata sijui, siwezi maliza maji ya moto ya kuoga aliyosema kwanza.

Mama na mtoto

Mtoto: Mama kwani dada wa kazi hajakua tu?
Mama: Kwa nini mwanangu?
Mtoto: Ananyonya mpaka leo!
Mama: Mhh! Mwanaaangu...
Mtoto: Kweli mama, mi nlimuona kapiga magoti huku baba anamnyonyesha.

Headphones II

Jamaa alifika duka la vyombo vya mziki akaona headphones, akaulizia kazi yake akajibiwa. Kisha akauliza "inachukua mda gani mziki kufika masikioni?"

Headphones

Jamaa alinunua discman kwa mara ya kwanza, sasa wakati ameweka headphones masikioni akisikiliza mziki, rafiki yake akawa anaushika waya wa headphones huku akisema "hee! Huu waya wake mzuri"

Jamaa mwenye discman akamuambia kwa ukali "wee usiushike utazuia mziki usifike masikioni"

Gazeti

Mtoto katumwa gazeti la tarehe 10. Alipokosa na kurudi... "baba nimekosa gazeti la tarehe 10. Nimenunua ya tarehe 5 mawili"

Kikaoni

Mtendaji mmoja kwenye kikao alimuuliza mwenzake.
Mtendaji: Ndugu yangu mbona hatuonani?
Mtendaji ii akajibu "samahani mkuu, hatuonani wapi?"

Monday, September 6, 2010

Jirani mpya

"mama nikuambie yule dada jirani yetu anaitwa nani?" mtoto akimuuliza mama yake.
Mama akauliza, "we umejuaje mwanangu?"
Mtoto: Si baba alimuita nkasikia.
Mama: Enhe alimuitaje?
Mtoto: Si Honey! Tena ukiondokaga baaba muoogaa peke yake basi anaendaga kulala kwa huyo dada.

Watoto je?

Jamaa mmoja akiongea na rafiki yake "mke wangu hapendagi kabisa nimguse miaka yote tangu tumeoana."
Rafiki yake akanena "sasa hao watoto mmewapataje?"

Don't drink & Drive

Jamaa mmoja alirudi kwake, mkewe akamuuliza "vipi mume wangu mbona... Kwa miguu?"
Mume akajibu "nimekuta kibao kimeandikwa don't drink and drive ivo nlipokunywa tu maji nkaiacha pale pale gari"

Njoo nje

Katoto kamoja ka-kiume kalirudi ndani mbio mbio huku kakimuambia mama yake "mama mama njoo haraka haraka umuone mama frank kasimama pale nje sketi yake inapeperuka na upepo... njoo umuone kavaa ya blue kama yako"

Watoto wa mtaani

Bibi mmoja kasikika akilalama, ''kila siku wanasema watoto wa mitaani wanaongezeka! Si wamfundishe huyo mitaani uzazi wa mpango?"

Sunday, September 5, 2010

Thermos

Jamaa aliona kifaa dukani, akauliza "hii nini?"
akajibiwa "hii ni thermos, kazi yake kufanya cha moto kubaki moto na baridi kuwa baridi."

Siku yupo kazini boss akamuuliza nae akamjibu kama alivyojibiwa.
Boss akauliza tena, "sasa umeweka nini ndani?"
Jamaa akajibu, "chai na maji ya baridi ya kunywa baadae."

Kuchelewa

Jamaa aliamka haraka haraka akiwa amechelewa. Mbio mbio akiwahi anapoenda.
Baada ya mda akarudi.
Mama: Vipi mbona umerudi?
Jamaa: Nimechelewa mekuta mlango washafunga kanisani.
Mama: We umeenda kanisa gani?
Jamaa: Hapo konani karibu na...
Mama: Khaa! Pale msikitini jamani kanisa lipo kwa mbele zaidi.

Mwanga wa tochi

Kaka mmoja na mchumba wake walienda tembea kwenye garden. Kaka akavuka daraja la mbao, alipomaliza likavunjika.

Mchumba wake akasema, "ntavukaje sasa?"
Kaka akajibu, "subiri giza liingie, ntawasha tochi kisha utavuka kupitia juu ya mwanga wa tochi."
Mchumba: "Haa! Hapana nkifika katikati ya mto we utazima tochi halafu ntaanguka."

Punguza uzito

Dokta alimshauri jamaa akimbie kwa siku 30 ili apungue uzito.
Siku 30 baadae jamaa kwenye simu, "dokta asante sana nimepungua, ila sasa ntarudije nipo mile 300 toka nyumbani?"

Punguza uzito

Dokta alimshauri jamaa akimbie kwa siku 30 ili apungue uzito.
Siku 30 baadae jamaa kwenye simu, "dokta asante sana nimepungua, ila sasa ntarudije nipo mile 300 toka nyumbani?"

Hii nini?

Mtoto alimuliza mamake.
Mtoto: Hiki nini?
Mama: Mapulizo (matiti)
Mtoto: Nilimuona baba jikoni akiyapuliza ya dada mfanyakazi

Kanisani

Jamaa alikutana na wenzake wanatoka kanisani akawauliza, "leo sijaja kanisani, vipi wameita majina?"

Mtekanyara

Jamaa mmoja alimteka mtoto wa tajiri akaandika barua "nimemteka mwanenu, nataka dola elfu5. Nimemruhusu mara 1 tu aje achukue nguo za kuvaa kesho."

Mtekanyara

Jamaa mmoja alimteka mtoto wa tajiri akaandika barua "nimemteka mwanenu, nataka dola elfu5. Nimemruhusu mara 1 tu aje achukue nguo za kuvaa kesho."

Soda | 500

Mmasai kaenda dukani kauliza "soda bei gani?" Kaambiwa "mia 5."
Katoa kibuyu, "weka ya mia nampa mtoto."

Ibada

Jamaa alikua anaangalia ibada kwenye tv sebuleni. Punde akajibu sms iliyoingia "siwezi chat now padre ataniona"

Makaburini

Dogo mmoja na wenzake wawili walipita njia moja karibu na makaburi. Sasa wakawa wanaona wengine wamekufa na umri mkubwa mfano 95, 101 nk nk.
Aliporudi nyumbani akamuambia mama yake, "mama mi nikifa niandikeni nimeishi miaka 200"

Mama kwa mshangao akauliza, "hee! We mtoto nani uliwahi msikia...?"
Mtoto: We niandikieni ivo ivo?
Mama: Kwa nini wasema hivyo mwanangu?
Mtoto: Nataka niwashinde wote waliokufa.

Makunyanzi

Mtoto mmoja alimuona bibi yake walioenda kijijini. Baada ya kuona ngozi ya bibi yake ina makunyanzi ya uzee sana akamnong'oneza mama yake, "mama... kwani bibi si aipige pasi tu ngozi yake imejikunja sana!?"

Mnyama gani?

Siku moja mama mmoja alienda mbuga za wanyama na mwanae mdogo wa miaka miwili. Wakati wakiangalia wanyama yule mtoto akaona tembo akamuulima mama yake "mama huyu mnyama gani? Mbona ana mkia mbele na nyuma?"

Friday, September 3, 2010

Msiba

Dada mmoja alipata taharifa kafiwa na mama yake. Boss akamuambia aende tu nyumbani. Dada akasihi aendelee wepo eneo la kazi.

Baadae boss akaenda muangalia akakuta analia akamuuliza "vipi tena kulikoni?"
Dada akajibu "dada yangu anaenifuata amenipigia na yeye amefiwa na mama yake."

Kuchelewa rudi

Jamaa alinunua gari akaenda chalinze. Wakati anarudi mkewe akamuuliza "mbona umechelewa rudi?"
Mume "hii gari wameeka gia 4 kwenda mbele tu, kurudi nyuma eti 1 tu"
(alirudi kinyume nyume)

Mapacha

Mwanaume mmoja alienda hospitali, akakuta mkewe kajifungua mapacha akamuliza mkewe "huyu mtoto mwingine wa nani?"

Risasi

Mama mjamzito wa mapacha watatu alienda supermarket akapigwa risasi 3 tumboni.
Alipoenda kwa daktari akaambiwa "...usiwe na wasi wasi risasi zitatoka zenyewe"

Baada ya miaka 16 wale mapacha baada ya kuzaliwa siku moja ikawa hivi.
Wa kwanza: Mama.. Mama.. Nilienda chooni risasi ikatoka.
Wa pili nae siku moja akamuambia hivyo hivyo.

Wa tatu kabla hajasema mama akadakia "enh na wewe risasi imetoka?"
Mwanae akajibu "ndio imetoka wakati na... Ikampata baba kaanguka"

Thursday, September 2, 2010

Kutabiri mbele

Mwalimu aliuliza darasani, "inawezekana kutabiri jambo la mbele?"
Mtoto mmoja akajibu, "ndio! Mama huwa akiangalia daftari langu la hesabu huniambia, subiri baba yako arudi uone."

Wednesday, September 1, 2010

Makumbusho

Jamaa mmoja akipiga simu ofisi ya Makumbusho ya Taifa: "Haloo, hapo ni Makumbusho ya Taifa?"
OFISI: "Ndio, tukusaidie nini?"
JAMAA: "Ok, naomba mnikumbushe mwaka juzi saa yangu niliipoteza wapi?"
OFISI: "Pumbavu! Hiyo sio kazi yetu..!"
JAMAA: "Sasa makumbusho mnakumbusha nini?" OFISI: "Tunahifadhi mambo ya zamani." JAMAA: "Ahaa... kumbe saa yangu mtakuwa nayo..!"

Tuesday, August 31, 2010

Dish|Kutu

Jamaa mmoja alinunua dish la tv. Baada ya kulitumia kwa muda mrefu likawa limetengeneza kutu karibu loote.

Siku moja akalipaka rangi iliuiepuka ile kutu. Baada ya hapo hakukamata hata channel moja tena.

Monday, August 30, 2010

Naumwa

Marafiki wawili walikaa sehemu wakiongea. Mmoja akamuambia mwenzake, "naumwa leo kichwa."

Mwenzake akamjibu, "we unaumwa? Nenda pale mapokezi Muhimbili uone wagonjwa."

Mchaga.

Mchaga alipata ajali alipozinduka pale hospitali akauliza "nipo wapi hapa?"

Nesi akajibu,"umepata ajali, hapa upo hospitali. Bahati mbaya umekatika mkono."
Mgonjwa: Na je saa yangu ipo wapi ya Rolex?
Ipo mzee, nesi alijibu.

Nesi: Mkeo na watoto wapo hapa kukufariji.
Mgonjwa: Yeuwi... Wamefunga duka?

Sunday, August 29, 2010

Maneno mengi

Wakati jamaa mmoja anakula akawa anamsimulia mwenzake, "nimekutana na huyu mmoja asubuhi hii, mara moja alianza nitukana na kunitishia nk nk"

Msimuliwaji akauliza, "kwani mmekutanaje na huyo mtu?"
Akajibiwa "nimekutana nae kwenye ajali, nilimgonga na gari bahati mbaya"

Afande

Afande: Pw Conso yuko wapi?
Kuruta: Kaenda Air-port afande.
Afande: Pumbafu si ni nimerituma uwanja wa ndege Air-port rimeenda kufanya nini, rikija ni fatiki tu.

Vifaranga

Jamaa mmoja alienda kudai vifaranga kwa jirani, kisa jogoo wake ndio baba wa vifaranga.

Kidole gumba

Jamaa kidole gumba kilikua kinamsumbua, akaenda kwa dokta. Alipofika nesi akamuambia avue nguo kisha aingie chumba cha kusubiria kumuona daktari.

Jamaa akasema "yani kidole gumba tu ndo nivue nguo zote?"
Nesi akajibu, "hiyo ndio sera ya hospitali yetu."

Jamaa chumba cha pili akadakia, "hiyo sio kitu mi nimekuja kutengeneza simu."

Tongoza

Mwanaume mmoja akimtongoza Mwanamke.
Mwanaume: Nipo tayari ku-share kila kitu nawe...
Mwanamke: Tuanze na bank akaunti yako.

Saturday, August 28, 2010

Kijiti

Kwenye sherehe moja ya kuwapongeza maharusi, bwana harusi alitangaza kumkabidhi kijiti rafiki yake mmoja nae aoe siku za usoni.

Jamaa mmoja toka kwa washiriki wa sherehe hiyo akatamka "atakipoteza huyo."

Talaka

Mke na mume walienda mahakamani kuomba sheria iwasaidie watengane, jaji akawauliza "sasa mtagawanaje? Mna watoto watatu"

Mume mtu akajibu "ohh basi tutakuja tena mwakani"

Polisi

Polisi mkuu: Umefanikiwa mkamata mtuhumiwa?
Polisi mdogo: Hapana, ila ameniachia alama za kumtafuta...
Polisi mkuu: Nini?
Polisi mdogo: Alama za vidole.
Polisi mkuu: Wapi?
Polisi mdogo: Kwenye mashavu yangu.

Meli kuzama

Meli moja ilikuwa inazama, watu wakaanza kupiga kelele "meli inazama... meli inazama..."
Jamaa mmoja akasema "kwani ni umbali gani toka hapa mpaka kwenye ardhi?"

Akajibiwa, "kilomita 2"
Jamaa akasema, "sasa hao wanapiga kelele za nini kumbe ni hapo tu?"
Akajitosa kuanza kuogelea kidogo akauliza huku akiwa kwenye maji, "ni upande gani ilipo ardhi?"

Akajibiwa, "kwenda chini" (chini ya maji).

ATM|Password

Dada mmoja wakati anatoa hela kwenye ATM, wa nyuma yake akasema "hahaha nimeiona password yako ina nne-nne. Jamaa akajibu "haha umekosea, ni 1382."

Bia ya mwisho

Mume: Tufanye tuondoke.
Mke: Mume wangu niongezee bia moja ya mwisho.
Mume: Hapana utakojoa kitandani usiku.

Dokta | Mifugo

Jamaa mmoja alimpeleka ndama wa ng'ombe wake kwa dokta. Dokta akamuuliza ana shida gani?
Akajibu "mekuja umpime ndama wangu DNA nijue kama ni wa kwangu!"

Lini besdei

"Mama... Mama... Kwani birthday yangu mbona haifiki tu?"
Mama: Kwani unaijua tarehe?
Mtoto: Ndio si tarehe 32 Mei?

Mwanamziki kwenye TV

Jamaa mmoja alimuona mwanamziki kwenye tv moja akiimba. Baada ya masaa kadhaa akatoka na rafiki yake wakaenda kumtembelea mtu.

Walipofika kwenye tv channel ingine tofauti na home kwake akamuona mwanamziki yule yule akamuuliza mwenzake kwa kunong'ona "huyu mwanamziki huku kafika saa ngapi? Me si nlimuacha kwenye tv ya home."

Besdei

Mke siku moja akimuambia mumewe kwenye simu, "mume wangu usije sema sijakukumbusha, kesho ni birthday yangu."

Mume akamjibu, "sidanganyiiiki."

Mimba

Siku moja mama mmoja akimuasa mwanae wa kike pekee na dunia ya leo. "mwanangu Jesca, usiongee na mwanaume utapata mimba na mengineyo kama ukimwi nk"

Baadae usiku baba yake aliporudi akawa anamsalimia mwanae huyo wa kike, mtoto nae akajibu "mama kaniambia nisiongee na mwanaume ntapata mimba"

Viagra

Siku moja mzee mmoja alimpigia simu daktari wake, mambo yakawa hivi... "dokta... dokta... Mke wangu kameza viagra zangu nifanyeje?"

Tanzanite

Marafiki wawili wakiongea.
J: Hatujaonana siku nyingi sana.
H: Kweli kabisa, unashughulika wapi siku hizi?
J: Nipo na mradi wa Tanzanite. Wewe je?
Mwenzake ili aonekane yupo juu kimaisha akajibu.
H: Ooh! Mimi nipo kwenye mradi wa Mbeyanite.

English only

Shule moja ya dotcom mwanafunzi mmoja alikuwa amejiegesha kitandani na mwenzake, sasa huyo mwenzake anaitwa Kassim akawa anauvutia kwake mto.

Jamaa ikawa inamkera sasa kizungu kwake kidogo shida ikabidi amuambie "katelefone katelefone pliz don't smoke my river"

Tafsiri: Kassim Kassim acha kuvuta mto wangu.

Sinema

Mzee mmoja aliulizwa, "mzee ni sinema gani unaipenda sana?"
Mzee akakaa kimya sekunde kadhaa huku akivuta kumbukumbu kisha akajibu "ile ya kipaimara ya mjukuu wangu"

Namba ya simu

Juma: Jamaa amekupa namba?
Ali: Ndio na nsham-beep.
Juma: Hebu ni hiyo namba.
Baada ya kupewa akanena.
Juma: Wee! Ume-beep landline?

Dawa

House girl mmoja aliulizwa "umempa dawa mtoto?"
Akajibu "amekataa kumeza, nimemsaidia kuzimeza mimi ili zisipotee bure"

Friday, August 27, 2010

Mkia

Mdada mmoja alienda kwa daktari wa wanyama, safari hii alienda na mbwa wake akamuambia dokta "dokta naomba umkate mkia mbwa wangu"
Dokta: Kwanini jamani?
Dada: Bibi anakuja kesho sitaki amtikisie mkia"

Dawa ya...

Jamaa mmoja mweupe wa ngozi alienda kwa dokta. Akamuambia dokta "dokta nna kiji-alama kekundu kwenye ngozi, sivi ni nini?

Dokta akampa dawa akapake nyumbani.
Kesho yake aliporudi akamuambia dokta, "kile kidoa kimeishia kabisa, ni dawa gani umenipa?"

Dokta akajibu " ni lipstic remover"

Hela

Babu alimuona mjukuu wake akifungua mlango bila kuugusa.
Babu akampa elfu kumi, mtoto akajibu "hapana babu, kaa nayo tu nimedanganya nimejifunga uzi.

Asubuhi ilipofika babu akampa elfu kumi tena, mtoto akasema "babu lakini umenipa jana."
Babu akajibu, "ile ya jana ya bibi yako"

Ndevu

Mtoto akimuambia Baba yake "baba... Yule mkata majani wetu ana ndevu kama zako?"
Baba: Ndevu?
Mtoto: Ndio ndevu kwa chini ya kitovu.
Baba: We umeonaje?
Mtoto: Nilimuona mama akimnyoa...

Thursday, August 26, 2010

Wamama watatu

1: Jana si nlifungua pochi ya mwanangu, nkakuta bangi. Nlikua sijui kama anavuta.

2: Hiyo mbona afadhali mi nlikuta Kitambulisho feki, sikuweza amini.

3: Hizo zenu hamna kitu, me nlikuta condom kwenye pochi ya mwanangu, nlikua sijui kama ana uume.

Matumizi ya kondom

Jamaa alifundishwa matumizi ya condom, kwa vile mfundishaji hakuwa na zana ilimbidi atumie chupa ndogo ya maji kama mfano wa uume.

Jamaa alikua chumbani aki-do na mwanamke akaivisha chupa condom huku akido pembeni mwa ilipo chupa, huku akijua yupo sahihi.

Gari

Jamaa mmoja wakati wanasafiri gari ndogo mbili zikawapita (overtakin) akasema "ile gari ya nyuma itachoka kumfuata ile ya mbele."

Wednesday, August 25, 2010

Redioni

Jamaa mmoja alikuwa anahojiwa redioni, akaambiwa achague mwimbo wa kumburudisha si akachagua wimbo wa taifa.

Maongezi

Jesca: Za masiku my dia?
Hilda: Njema, nimekumiss shosti.
Jesca: Hata mie shosti. Hivi babu yako bado yupo?
Hilder: Enhe yupo bwana, anazeeka tu.
Jesca: Hivi ana miaka mingapi sasa?
Hilder: 98 sasa.
Jesca: Mh! Bado mdogo kumbe.

Condom

Jamaa mmoja alienda pharmacy kununua condom, alipofika akamkuta dada ndio mhusika kisha akasema "...nahitaji condom..."

Muuza madawa akajibu "unahitaji size gani?"
Mteja akajibu "sijui habari ya size"
Muuza madawa akajibu "vua suruali tuone."

Sumu

Baba alikua ana wivu kwa mwanae mchanga anavyonyonya hivyo akaweka sumu kwenye chuchu za mke wake. Siku iliyofuata wakakuta dereva wao akafa kwa sumu.

Tuesday, August 24, 2010

Window 7

Jamaa mmoja alinunua laptop, sasa siku moja fundi akawa anamuelekeza jambo "open window 7 kwanza!"
Jamaa akajibu "nyumba yangu haina madirisha saba fundi."

Bar | Maegesho

Kaka mmoja aliingia bar. Akaenda mpaka kaunta, akaagiza bia kwa kuinyooshea kidole. Mhudumu akakataa kumpatia bia.

Jamaa akauliza kwa nini?
Mhudumu akajibu, "ukitoka hapa utaenda ku-drive"
Jamaa akauliza "sasa mbona nje kuna parking za magari?"

Simu|Pesa

Mama: Jamani simu zinakula heela khaa! Hadi nachukia.
Mtoto anasikiliza tu. Siku moja anko ake akaja akawa anaweka simu ya mkononi mezani. Mtoto akamwambia "anko usiweke pesa karibu na simu italiiwa hee!"

Pesa inaongea

Mtoto: Baba, eti pesa inaonge?
Baba: Ndio mwanangu.
Mtoto: Sasa mbona naisemesha haijibu?

Swaumu

Dokta wa meno alipomaliza mng'oa jino mgonjwa wake akamuambia "unaweza piga kelele kwa sauti kubwa uwezavyo?"

Mgonjwa akauliza, "kwa nini mbona umening'oa vizuri tu."
Dokta akajibu, "nje pana foleni kubwa sana, na swaumu imekolea nataka wapungue."

Maji

Mtoto mmoja asubuhi moja alimsikia dad yake akimuambia kaka yake mkubwa akajaze maji kwenye gari.

Basi muda ulipofika baba kufika kwenye gari akauliza "nani amejaza maji kwenye gari?"
Katoto kakajibu "ni mimi baba"

Baba: Niliposema kaka yako akajaze maji sikumaanisha ndani ya gari, ona viti, kapeti vyote maji tupu.

Lift

Jamaa mmoja alipewa lift. Nje mvua ikaanza kunyesha kwa vile lift alopewa ina vuja ikabidi amuulize mwenye gari "mbona gari yako inavuja kama mti wa maembe?"

Tafuta gari

Mlevi mmoja alilewa chakari, akawa yupo yalipopaki magari. Akawa anatafuta gari lake huku akigusagusa ama kupapasa karibu kila gari asilitambue la kwake.

Jamaa mmoja akamkuta na kumuuliza "unafanya nini?"
Mlevi: Natafuta gari langu.
Jamaa: Sasa ndo utalijuaje kama ndio lako?
Mlevi: Lenyewe ambulance.

Msafiri|Mpokeaji

Jamaa mmoja alikuwa anasafiri toka mkoani kuelekea Dar. Mwenyeji wake akamtumia meseji "unakuja na basi gani?" Msafiri akajibu "nipo kwenye Sumry Air-line" Mpokeaji akajibu "oh, na mimi nasogea sogea ubungo air port kukusubiri."

Mbegu

Jamaa mmoja alienda kwenye party. Baada ya kula keki kwa jinsi ilivyotamu akauliza kwa jamaa wa pembeni yake "aisee hamna mbegu ya hii..."

Raia

Kijana mmoja alikaa chini ya mti akiwaza "ili kujua mie ni raia wa nchi yangu au la! Ntajaribu gombea ubunge."

Mswaki

Mzee mmoja wakati wa kula mezani na familia yake aliuliza "nani kapika mboga leo?"
Mtoto mmoja akajibu "Jesca baba"
Baba akanena "Oh! Hajapiga mswaki"
Mama akauliza "why?"
Baba: Chumvi nyingi.

Monday, August 23, 2010

Moshi

Jamaa mmoja alizoe maisha yake yote kijijini, kupika kwa kutumia kuni nk nk...
Alipofika mjini siku moja akaona gari linatoa moshi ile mbaya akauliza "ile gari inatumia kuni?"

Maongezi|Watoto

Mtoto mmoja akiongea kwenye simu na mtoto mwenzake, "mesikia baba na mama yako wamefunga pingu, sasa unaishi na nani?"

Sms

Mwanamke: Mpenzi wangu mbona hujibu sms zangu jamaani?
Mwanaume: Nasubiri zifike 25 nikurudishie zilizoshika top 10.

Chura

Mtoto mmoja.. "mama.. mama.. Njoo haraka baba anakufa huku amemeza chura njoo haraka."
Mama kufika anakuta baba kalala huku anakoroma.

Bahati nasibu

Jamaa alishinda bahati nasibu.
Mshindi: Nimeshinda milioni 30, nipatie pesa yangu.
Mchezeshaji b.nasibu: Haiwi hivyo, huwa unapatiwa milioni moja leo halafu zingine baada ya wiki mbili.

Mshindi: Mi sielewi, nipeni pesa yangu.
Jamaa mchezeshaji akamjibu vile vile.

Mshindi: Basi nipe elfu moja yangu nliochezeshea.

Pombe bwana

Mwanaume mmoja aliopoa mwanamke huku akiwa amelewa, na huyo mwanamke kalewa pia.

Walipofika nyumbani kwa jamaa, mwanamke akachukua kioo na kujiangalia kisha akasema "huyu kwenye frame ya picha ni mkeo? Mbona anarembua kama kalewa pombe?"

Jamaa akakichukua kioo, kuangalia akajibu "yupi huyu? Frame hii ni mimi enhe chukua uangalie tena..."

Uchoyo

Mwanaume mmoja alipomfumania mkewe akiwa na njemba uchi wa nyama, "...yaani una thubutu kunivunjia heshima yangu? Unaleta mwanaume mpaka chumbani kwangu...."

Mke akajibu, "sasa mume wangu me ntamnyimaje mtu kitu ngali nnacho?"

Shabaha

Mijamaa miwili ilikuwa inatoka kuwinda, mmoja akamwambia mwenzake "aisee naiona nyumba yako tokea hapa nlipo, halafu mkeo yupo na njemba ndani." (kwa darubini ya bunduki).

Mwenye mke akajibu "enh!!? Mshuti mke wangu kichwani, na hilo lijamaa sehemu za siri."
Jamaa akajibu "ooh, hiyo rahisi. Risasi moja tu itapiga sehemu zote hizo."

Talaka

Mama, baba na mtoto walikuwa wamekaa sebuleni. Baba akatoa laptop kwenye begi ili aiwashe. Kabla hajawasha mtoto akadakia "baba.. baba.. Naijua password yako."

Baba kwa mshangao akauliza "umeijuaje we mtoto?"
Mama nae yupo anasikiliza.
Mtoto akadakia "naijua si 'talaka'? Au unabisha?"

Maua...

Mama mmoja alipanda maua yake mazuri nyumbani nje.
Siku moja house girl wake alikuwa anatongozwa na kijana wa mtaani tu. Kuja kuhamaki baada ya kutongozwa yale maua kayavunja vunja...

Sunday, August 22, 2010

Mbu

Mbu mmoja alimuambia mwenzake "sijui nna malaria?"
Mwenzake akamjibu "tatizo lako hutumii neti."

Mbu

Mbu mmoja alimuambia mwenzake "sijui nna malaria?"
Mwenzake akamjibu "tatizo lako hutumii neti."

Sumu ya panya

Mtoto mmoja alimuambia mama yake, "mama leo sijawasikia panya kabisa wakigonga gonga masufuria"

Mama akajibu, "enhe kweli kabisa mwanangu"
Mtoto: Unajua kwa nini mama?
Mama: Enhe kwa nini mwanangu?
Mtoto: Nimewaekea ile sumu ya panya kwenye mboga tuliyokula jioni hii...."

Ukuta

Katika wodi ya wagonjwa wa akili, walichorewa ukuta wakaambiwa waruke waende zao.

Wootee wakakimbilia wakabaki wawili wanawaangalia wenzao. Wakaulizwa na daktari wao.

"Nyie mbona hamfanyi kama wenzenu?"
Wa kwanza akajibu, "ukuta wenyewe si haujakauka bado"
Wa pili akajibu, "ona, ona tayari umeshaweka ufa ukuta wenyewe"

Na mama yake

Mtoto: Mama kwa nini mmeachana na baba?
Mama: Mwanangu hilo sipendi lizungumzia....

Siku chache baadae katoto baada ya pekua pekua akaona taharifa kadhaa kwenye kitambulisho cha mama yake. Siku ya pili akamfuata mama yake.

Mtoto: Mama najua kwa nini umeachana na baba?
Mama: Ee!! Umejuaje?
Mtoto: Kwa sababu una F kwenye Sex nimeona kwenye kitambulisho.

Swali tamu

Mwalimu aliuliza swali wanafunzi wa chekechea wakawa wanajibu.

Mwalimu: Sehemu gani ya mwili mtu akifa inaenda mbinguni?
Mwanafunzi 1: Roho ndio inaenda.
Mwanafunzi 2: Moyo.
Mwanafunzi 3: Miguu.

Mh! Mwalimu alistuka akauliza "enhe kwa nini miguu?"

Mwanafunzi wa 3 akajibu "jana nliona mama kanyoosha miguu juu uku akisema "oh God am coming... Huku baba kamlalia juu asiende"

Saturday, August 21, 2010

Siku ya hukumu

Mchunga alikuwa anahubiri kanisani akasema 'siku ya mwisho (hukumu) watu watalia na kusaga meno ndipo walipoinuka kibogoyo na bubu wakasema sisi tumesevu kwenye hukumu.

Bafu|Singo

Jamaa anajulikana kabisa amepanga chumba single yaana hamna bafu wala choo ndani. Siku moja rafiki yake wakati anamuita huku nje akajibu ''nakuja nipo bafuni naoga kabisa!''

Kuoa

Mtoto mmoja alikua anamuona jirani yao kwa miaka takribani miwili wakiishi na mchumba wake nyumba moja.
Siku moja hao majirani walitangaza nia ya kuoana, mtoto alipozidaka nyepesi hizo akaenda mwambia mama yake, "mama! mama, yule jirani yetu anataka kumuoa mke wake."

Mwizi|Mwalimu|M'sheria

Mwizi, Mwalimu na Mwanasheria wote walikufa ghafla kwenye ajali mbaya.

Walipofika peponi wakaambiwa nako kumejaa ila atakaepatia jibu la swali ndio ataingia...

Mwalimu aliulizwa "ni meli gani ilizama Tanzania?" akajibu MV. Bukoba.
Akaambiwa amepatia aingie.

Mwizi akaulizwa "ni watu wangapi walipoteza maisha kwenye hiyo ajali?" mwizi akajibu 150.
Akaambiwa amepatia na aingie.

Mwanasheria akaambiwa kulingana na jibu alilotoa mwizi "wataje majina?"

Aje...

Askari polisi mmoja akiwapa maagizo askari walio chini yake "Mkamtafute mtuhumiwa aje akiwa HAI au MAiTi aje ajibu Tuhuma zinazomkabili"

Makaburini

Mama mmoja na mwanae wakipita pembezoni mwa makaburi, mama akasoma maandishi kwenye kaburi moja kisha akajisemea kwa masikitiko "maskini alikuwa DAKTARI na MUWAZI tu.

Mtoto nae akasoma kisha akamuuliza mama yake "mama kwanini wamewazika wawili sasa?"

Dharura|Ndege

Rubani alitangaza watu wote wakae vitini ndege imeleta shida wanatakiwa watue kwa dharura.
Pilot akamuliza mhudumu wa ndege "watu wote wamekaa?"
Mhudumu akajibu "ndio kasoro mwanasheria mmoja anapita pita kuchukua biznez cards"

Vekesheni

Jamaa alienda vekeshe na mkewe. Bahati mbaya akafia wakati wapo vekesheni Jerusalem.

Akaambiwa kumsafirisha mpaka nchini mwao ni dola 3000, wakimzika Jerusalem ni dola 300 tu.

Jamaa akakataa kumzika pale pa dola 300 huku akisema "hapo zamani sana alikufa akafufuka baadae, mi sipo tayari mke wangu afufuke."

Kibosile akifa

Boss mmoja hospitalini hoi kitandani, alimuita mwanasheria wake, daktari na mchungaji.
Akawaambia "hapa nna dola elfu90 chini ya mto. Nimeziweka kwenye bahasha dola elfu 30 tatu. Nataka nikifa kabla hawajatupia udongu mzirushie kaburini."

Wakaitikia "sawa, haina shida"

Baada ya mazishi:
Mchungaji: Acha niseme ukweli nimechukua dola elfu10 tu kwa ajili ya ujezi wa kanisa ingine kama marehemu alivyoagiza.

Dokta: Mie nimechukua dola elfu15 tu ingine kama marehemu alivyosema.

Mwanasheria: Mie niliziweka kwenye akaunti yangu, nikaandika cheque na kuiweka kwenye bahasha nkafanya kama marehemu alivyosema...

Za nyuma

Unaikumbuka hii?
Nyoka m1 asked the atha "ivi sisi tuna sumu?" Mwenzake akajibu "ndio, why?" AKAMJIBU "nimejing'ata bahati mbaya!"

Ndio|Hapana

Kwenye mtihani wenye majibu Ndio|Hapana
Msimamizi mmoja alimfuata mwanafunzi wakati anasimamia mtihani akamuuliza "mbona unarusha rusha hiyo sarafu ya sh 100?"
M'funzi: Nahakiki kama majibu nlojaza ni sahii.

Mboga za majani

Mama mwenye nyumba aliporudi akauliza "mbona sebule ipo hivi leo?"
House girl akajibu "nimesahau kupanga vizuri, nilichukua hiyo mboga ndo naipika"
Mama akanena "weewe!! Hayo uliochukua ni urembo sio majani halisi (artificial mimea)

Akon

Unaujue wimbo wa AKON "lonely" basi nausikiliza hapa, AKON anauimba kanyong'onyeaa sijui "swaumu imemkolea?"

Kipindi cha tv

Mtoto mmoja wakati anaangalia kipindi kizuri kwenye televisheni akamuita mama yake "mama... mama njoo haraka uone"

Bahati mbaya mama yake akakosa hiyo sehemu, mwanae akasema "aaahh umecheleewa"

Mama nae akajibu "tv ya chumbani si unajua ipo dakika 4 nyuma itakuwa haijaonyesha ngoja nikaangalizie huko."

Ndoto tatu

Vijana watatu wakisimuliana ndoto ya jana usiku:
Wa 1: Aisee jana nimeota namiliki BMW new model.
Wa 2: Mie ndo funika, nimeota namiliki PPF Tower.
Wa 3: Mie yangu jana si nimeota namiliki wake zenu.

Mke na mume

Mwanamke mmoja alimpigia simu mumewe akiwa mbali nae.
M'ke: Umeamkaje m'me wangu?
M'me: Nimeamka na hang-ova leo mpenzi wangu.
M'ke: (kwa ukali alisema) nilijua tu nikisafiri utamleta tena huyo mwanamke wako.

Toto tundu ii

Mama mmoja wakati anamfokea mwanae mdogo alieharibu jambo alimalizia kwa kumuambia...
"...muone kwanza, sura mfuko wa jeans"
Mtoto akauliza "wa mbele, wa nyuma?"

Toto tundu

Mtoto mmoja alikua anaitwa Happy, na dada wa kazi za ndani nae anaitwa Happy. Sasa siku moja mama yake mtoto akamuambia mwanae Happy amuite dada aje...

Kwa vile alikuwa mbali kidogo yule mtoto ilimbidi aite kwa sauti kubwa kidogo "H.a.p.p.y!... Haaappy..." kituko ni pale alipokua akiita na yeye muitaji anaitika.

Mama yake akamuuliza "sasa mbona unaitika we mwenyewe tena?"
Mtoto akajibu "kwani na mimi si jina langu Happy?"

Friday, August 20, 2010

Mtoto kupotea

Mtoto mmoja alipoteana na dad yake mlimani city. Akakutana na askari akamuambia "nimepoteana na baba yangu namtafuta"

Askari akauliza "huwa anapenda nini haswa?"
Mtoto akajibu "bia na wanawake wenye nyonyo kubwa"

Pampus

Mtoto mmoja wakati anavishwa pampus huku baba wa toto akiwa pembeni.
Alikuwa anaangalia mwanae akivishwa pampus akamuuliza mkewe "hivi hizo kitu (pampus) huwa zina mifuko?"

Mke anapaki

Jamaa alirudi nyumbani akakuta mkewe anapakia nguo kwenye begi lake la safari.

Mume akauliza, "unapaki nguo unaenda wapi mke wangu?"
Mke akajibu, "naenda Daslam, nasikia wanawalipa dola 300 malaya. Bora niende huko kuliko kukupa tu bure."

Mchumba

Katoto kamoja siku moja alimuuliza bibi yake wa miaka 94.
"bibi... kwani we kuna mchumba?"

Bibi akajibu "mjukuu wangu, mchumba wangu ni tv, ndio anaenipa furaha na kuniondolea mawazo"

Sasa siku moja tv ilikuwa inaonyesha chenga chenga... Bibi akawa anaipiga piga/gonga gonga ionyeshe vizuri.

Kidogo mtoto akasikia mlango unagongwa akaenda fungua.
Kumbe alikuwa mchungaji kaja kumuona bibi.

Mchungaji: Hujambo...? Bibi yupo?
Mtoto: Yupo chumbani anampet pet mchumba wake.

Kupima damu

Mtoto mmoja alimkuta rafiki yake hospitali analia, akamuuliza "unalia nini?"
Dogo mwenzake akajibu "nimekuja kupima damu wamenikata kidole.''

Rafiki yake nae akaanza kulia. Mwenzake aliekuja kupima damu akamuuliza "unalia nini sasa na wewe?"
Mwenzake akajibu "mi nimekuja kupima mkojo"

Mgonjwa kwa dokta

Mgonjwa: Dokta nimekuja unibadilishie dawa.
Dokta: Dawa? Kivipi? Sijaelewa.
Mgonjwa: Mi naumwa kichwa ila dawa uliyonipa mbona nikimeza inaenda tumboni badala ya kichwani?

Naomba maji

Mtoto mmoja alipoenda kulala mara ghafla akaita... ''baabaa... naomba maji ya kunywa"

Baba akajibu, "lala bwana utakojoa kitandani."

Dakika chache baadae mtoto akasema vile vile tena. Baba nae akajibu vilele.

Awamu ya tatu mtoto akaomba tena na baba akajibu "sasa ntakuja na kiboko nikuchape, mbona hunielewi"
Mtoto akajibu "baba ukija na hiyo fimbo njoo na maji ya kunywa"

Kuchora mbwa

Kwenye kipindi cha sanaa wanafunzi waliambiwa wachore mbwa kafungwa kamba...

Baada ya muda mtoto mmoja akawa anatoka nje. Mwalimu akamuuliza "wapi unaenda?"
Mwanafunzi akajibu "namtafuta mbwa imebaki kamba tu nliyoichora, itakuwa amekata"

Bunduki

Jamaa alinunua bunduki, majaribio akam-shoot mwanae.
Alipokufa akasema ''aanha kumbe sio ya kichina"

Hii kutoka kwa...

Kichekesho hiki nlikisoma siku nyingi toka kwa cartoonist fadhil (jina la pili limenitoka)

Jamaa alienda kwa daktari wake alipofika akamuuliza dokta wake ''dokta! Hivi ile dawa ya kupaka uliniambia ninywe mara ngapi?"

Kuibiwa simu

Jamaa mmoja aliibiwa simu, sasa wakati anabishana ''simu yangu simu yangu.." akasema "kama unabisha tukapime DNA.

Thursday, August 19, 2010

Kupata mtoto

Katoto kamoja ka kike kalinyoosha mkono darasani kakauliza;
Mtoto: Mwalimu, bibi yangu anaweza kupata mtoto?
Mwalimu: Hapana ni mzee sana, hawezi.

Mtoto: Mama yangu je?
Mwalimu: Anaweza kupata, lakina na yeye amefikia uzee pia.
Mtoto: Mimi je?
Mwalimu: Ee! Hapana huwezi bado mdogo sana kupata mtoto.

Kavulana kamoja kakadakia na kusema mbele ya darasa zima ''unaonaa? Mi nlikuambia usiogope''

Nikifa

Jamaa alitishiwa kisu wakati wanataniana na rafiki yake, alietishiwa kisu wakati wa utani huo akasema ''weuwe, ooh, shauri yako. Nikifa utanitambua.''

Maelekezo

Jamaa akimuelekeza dereva aliekuwa nae vijijini wakati wa kuvuka daraja la kienyeji la magogo.

Kilichokua kinatakiwa kufanyika ni amuelekeze dereva akanyage kulenga magogo ili isije ikatelezea mtoni.

Mwongozaji akawa anamuelekeza ''njoo njoo njoo..." huku eti mkono mmoja kajiziba uso kwa uoga wa kushuhudia.

True story

Kuna siku wakati wa mizunguko ya ukaguzi vijijini tulifika kijiji kimoja, wananchi wawili watatu katika nyumba moja walitoka nje haraka haraka wakidhani askari. Kisa cha yote kwenye kijumba hiko kinauza podbe haramu ya Gongo.

Wednesday, August 18, 2010

Ujiko

Kijana mmoja wa makamo aliopoa mrembo. Sasa wakati wapo evening walk alipoona gari aina ya prado inakuja kwa mbele akajirusha mbio kwenye kichaka.

Yule mrembo akamshangaa na kujiuliza. Akamuuliza ''vipi?''
Kijana akajibu, ''umeiona ile prado?''
Dada akajibu ''ndio'' kaka akaendelea ''ni ya nyumbani ile sijui baba yule?''

Maongezi yalipoisha jamaa akamuambia yule mrembo ''samahani nisaidie kutoka miba zimezidi nikamata''

Kiti

Baba mmoja alipata wageni kwake nyumbani. Akamtuma mwanae aongeze viti pale sebuleni.

Mtoto kwa vile ilikuwa hamna namna tena ya kupata kiti kimoja cha ziada, akaenda kung'oa kiti kimoja toka kwenye gari ya baba yake.

Alipoulizwa na baba yake amekitoa wapi akajibu ''nimekiazima kwa jirani baba''
Baba akajibu ''ooh kumbe, kizuri, usikirudishe tutamuambia kiliibiwa.''

Kesho yake baba kutoka nje akaona gari yake haina kiti akaanza kufoka, mtoto akadakia "baba ni hivi jirani aliona nachelewa kurudisha akachukua cha gari yako, sasa wewe mkomeshe chukua hiki ufunge kwako."

Simenti

Jamaa mmoja alijikuta anakanyaka ciment. Na alikuwa amelewa. Alipofika nyumbani akalala hivyo hivyo na viatu.

Asubuhi alipoamka akakuta mwanae anamwagia maji miguuni ''wewe unafanya nini?'' aliuliza kwa ukali.

Mtoto akajibu ''mama kaniambia nimwagie maji ciment ishike vyema usiende kulewa.''

Nusu kwa nusu

Bibi na babu walienda best bite, wakaagiza burger moja babu akaanza ikata nusu ampatie bibi.

Kijana mmoja alikuwa akiwaangalia akawauliza "niwanunulie ingine?"
Babu akajibu ''hapana hii tutagawana nusu kwa nusu.''

Kijana akamuuliza bibi "bibi na wewe utaanza ila?''
Bibi akajibu ''nasubiri kwanza, sasa hivi ni zamu yake kutumia meno yetu.''
(sijui ya bandia...?)

Tuesday, August 17, 2010

Simu kwenye basi

Mtoto mmoja wa makamo siku moja mama yake alimnunulia chupi inafanana kabisa na baba yake.
Sasa siku moja wakati yupo kwenye daladala na mama yake mara simu ikaita ya mama yake.

Mama kabla hajaipokea akamuambia mwanae ''baba huyo anapiga simu''
yule mtoto kabla hata mama yake hajaipokoea kwa sauti ya kusikika mote kwenye daladala akasema ''mama kisha muulize kama amejisahau amevaa chupi yangu, mie sijaiona leo.''

Kijiti

Jamaa alipomaliza pata mlo kwenye retaurant moja na mrembo wake akamuuliza mrembo wake hivi ''nikuagizie toothpick?''
Yule mrembo akamjibu huku akiona ona aibu ''enhe! Asante nimeshiba sana''

Mwalimu darasani

Mtoto mmoja alimuuliza mama yake...
''mama, kwani mwalimu haruhusiwi kuvaa chupi?''
Mama kwa shauku na mshangao akauliza ''...mh! kulikoni mwanangu umesikia wapi hiyo?...''

Mtoto akajibu ''mi nashangaa mama, labda atakua anasahau... Si mwalimu wetu wa darasa ndio havaagi''
Mama akauliza ''we umejuaje?''

Mtoto: Si namtegesheaga kioo chini ya miguu yake.

Viatu vya ngozi

Mtoto mmoja alikutywa na mama yake akiwa na viatu vya ngozi... Mama yake akamuuliza ''Jasmine mbona umekaa chini?''

Jasmine akajibu ''ninaviandaa viatu vyangu''
Mama: Ooh umekua mtoto mzuri siku hizi unajua mpaka kupaka kiwi viatu? Wow!
Jasmine: Mama!! Nikipaka kiwi viatu si vitaharibika?

Mama akajibu ''haapaana mwanangu kwani vipi?''
Jasmine: Me mevipaka losheni kwani si vya ngozi na vyenyewe? Kiwi itaharibuu...

Swaumu

Jamaa alimuona mwenzake ni kama anatafuta kitu alichokipoteza akamuuliza ''mwenzangu vipi mbona kama hueleweki umepoteza kitu nini?''

Ndipo jamaa akamjibu ''ndio, nimeshangaa njaa imeacha kuuma ghafla nlipofika maeneo haya, hivyo laziima ntakua nimeidondosha hapa swaumu yangu''

Babashop

Mahause girl wameenda town wakawa wanaona kila salon imeandikwa barber shop. Wakatiaje, huyo baba shop tajiri ana maduka mji mzima.

Monday, August 16, 2010

Uwanjani

Siku moja wakati tupo uwanjani twacheza mpira wa kikapu, jamaa yetu mmoja ana maneno mengi sana.

Moja kati ya wachezaji akapewa pasi ikamponyoka mikononi... Yule maneno mengi akasema kwa sauti ''wee viiipi weewe unashindwa daka mpira? Unaogea kopo nini?''

Siku moja nyingine akaja uwanjani akiwa amevaa fulana nyeupe, mwisho wa siku baada ya kucheza kikapu akagundua fulana yake imechafuka maeneo ya mabegani akauliza kwa sauti ''nani kanikanyaga jamani?''

Moto

Jamaa mmoja alipoingia nyumba moja na kuona moto kwa ajili ya kutoa joto sebuleni (fire place).
Akaanza kwa kusema ''moto moto... moto..." huku akitafuta ndoo ya maji akauzime.

Lift

Jamaa mmoja aliomba lifti, ikawa hivi:

Jamaa: Naomba lift ndugu yangu.
Dereva: Utapakia wapi sasa ndugu yangu?
Jamaa: Hata hapo mbele.
Dereva: Hapa mbele hairuhusiwi abiria.

Jamaa: Basi hata huku nyuma.
Dereva: We huoni kama hili ni karandinga (lori la kubebea mahabusu/wafungwa).
Jamaa: Sasa mbona hao jamaa nyuma umewapa lift (wafungwa/mahabusu)?

Sunday, August 15, 2010

Kumtembelea mchumba

Kijana mmoja alienda mtembelea msichana wake anaesoma nae chuo kimoja. Jamaa alipofika nyumba husika akawa anataka kuishia nje, mzee mwenye nyumba akamsihi mtoto wake huyo mgeni aingie tu ndani.

Jamaa alipoingia si akakuta mzee anasafisha bunduki huku akiongea ''kijana... mambo ya shule huko huko shule... mmemaliza assignment zenu?''

Nyoka

''Dokta nadhani nna matatizo ya kuona siku hizi'' nyoka akimuambia daktari.
Daktari akamuambia ''ntakusaidia.''

Baada ya siku kadhaa nyoka akarudi tena, dokta akamuuliza ''vipi ile miwani niliyokupatia haijakusaidia?''

Nyoka akajibu ''dokta nimegundua kuwa kumbe kwa muda wa miaka mitatu nilikuwa nikiishi chini ya maji''

Mugongo mugongo

Baba mmoja na mama wakati wanajiandaa kufanya mapenzi mtoto wao mdogo wa miaka miwili na nusu aka-a-mka ''baba na mimi naomba nipande mgongonu'' mtoto aliomba.

Baba akawa anakataa, mama akasema ''muache tu hamna shida'' basi mtoto akapanda.
Wakati wanashughulika mama akawa amezidiwa na utamu kweli kweli mtoto akasema ''baba jishikilia jana kidogo tuanguke wakati wakati nimepanda mgongoni mwa yule mleta maziwa''

Saturday, August 14, 2010

Msibani

Mtoto mmoja alishuhudia kwa mara ya kwanza msiba mtu akizikwa akamuuliza mama yake ''mama... mama... Sasa nani atakua anambadilisha nguo huyo mtu wanaemfukia kwenye sanduku la mbao? Si zitachafuka haraka?''

Nguo ya mapenzi

Mwanamke mmoja alikuwa uchi wa nyama bibi yake akamuuliza pale sebuleni, ''mbona hivyo kulikoni?''
Mwanamke akajibu ''hii ni nguo ya mapenzi namsubiri muwe wangu.''

Baadae mume aliporudi akamkuta bibi yake mkewe nae hajavaa nguo ''bibi vipi leo una nini?"
Bibi akajibu, ''nimevaa nguo ya mapenzi namsubiri babu yenu''

Mume wa yule mwanamke akamjibu ''oh kumbe, sasa mbona hujainyoosha na pasi?"
(makunyanzi mwilini)

Biashara

Kaka mmoja akiitangaza biashara yake mbele ya mteja, ''kaka nauza vyombo vya plastic, vya udongo na miswaki used''

Kuchimba dawa

Mtoto mmoja alikuwa na anko ake wakitoka kijiji kimoja kwenda kingine, mara yule mtoto akabanwa na haja kubwa akamuomba anko yake amsubiri aingie kuchimba dawa.

Wakati yupo upande wa pili wa kichaka akamuuliza anko yake ''anko nachimba shimo kabla au baada?''

Friday, August 13, 2010

Mwalimu wa biology

Mwalimu mmoja wa baiolijia akifundisha darasani lile somo la viungo vya uzazi, akauliza "Kuna ambae hajaelewa mpaka nilipofikia sasa?"
Mwanafunzi mmoja akanyoosha kidole na kuuliza "Mwalimu mi umeniacha kidogo, labda ungevua suruali ukatuonyesha ndio tutaelewa vyema kwa mifano hai"

Bwenini

Mkufunzi mmoja wa chuo akiwaambia wanafunzi wa mwaka wa kwanza masharti "Bweni la wanaume ni la wanaume tu na la wanawake ni la wanawake tu" huku akiendelea kuongea "ukifumwa mara ya kwanza utalipa faini ya shilingi elfu 20, mara ya pili elfu 60, mara ya tatu laki mona na 80"

Mwanafunzi mmoja akauliza "Je kwa semester (Muhula) nzima ni shilingi ngapi?"

Wakili na Daktari

Mzee mmoja alipoona ana masaa 24 kabla hajafa pale hospitali. Akaagiza dokta na Mwanasheria wake waje.

Dokta akauliza ''hapa nafanya nini?'' mzee akajibu ''nothing, we simama tu hapo hapo.''

Mwanasheria nae akauliza ''hapa nafanya nini?'' mzee akajibu ''nothing, we simama tu hapo hapo.''

Baadae wakauliza tena pale waliposimama mzee akawajibu ''Kristo alikufa na wezi wawili, so na mimi nafanya vivyo hivyo''

Kuachana

Mwanamke mmoja alipovunja ukimya akamuambia mpenzi wake waachane. Mpenzi wake kwa vile alikuwa mji mwingine kabisa, akatuma picha 13 na kumuambia ''sikumbuki vizuri we ni yupi, chukua picha yako zingine nirudishie''

Thursday, August 12, 2010

Kabla ya kufa

Mume: Mke wangu nikifa utaolewa tena?
Mke: Ndio, itategemea.
Mume: Utampa gari yangu aendeshe.
Mke: Mh! Nadhani.
Mume: Utamuacha akae kwenye kiti changu sebuleni?
Mke: Labda.
Mume: Utamuacha avae suti yangu nzuri?
Mke: No, ye ni mfupi.

Wodini

Jamaa mmoja aliamka akiwa kitandani wodini baada ya kupata ajali mbaya. Akauliza ''dokta... dokta... Mbona siusikii kabisa mkono wangu wala mguu..."

Dokta akajibu, 'huwezi isikia kwa sababu nimeikata yote'

Huzurio kwa dokta

Mwanamke mmoja alienda kwa dokta kufanya check-up. Kwa vile alikuwa anaona aibu akamuambia dokta azime taa ili avue nguo. Alipomaliza akamuuliza ''dokta niweke wapi nguo zangu?''

Dokta akajibu ''weka kwa hapa karibu na zangu''

Ajali-pikipiki

Dereva mmoja wa pikipiki alivaa koti nyuma mbele, akapata ajali.

Wasamaria walipokuja kumsaidia wakajua shingo imegeuka wakaanza kuigeuza kugeukia usawa wa koti. Kumbe ndio kifo.

Wednesday, August 11, 2010

Kuibiwa

Mzee mmoja na mkewe wakati wanatoka supermarket na mkewe walikuta gari yao haipo walipoipaki. Wakaenda polisi kutoa taharifa.
Polisi akashauri waje nae sehemu ya tukia kutafuta ushahidi.

Wakalikuta gari lao limerudi na kuna kibahasha kimewekwa kwenye wiper kimeandikwa hivi ''samahani nilichukua gari lako, mke wangu alishikwa na uchungu nkaamua kumkimbiza hospitalini. Pole kwa usumbufu. Chukua tiketi mbili hizo mje kwenye tamasha kama zawadi yangu''

Siku walipoenda kwenye tamasha kurudi wakakuta nyumba imeibiwa vile vitu vya thamani vyooote na kukuta barua imeandikwa ''nina shida ya ada ya mwanangu hivyo nimekuja tena.....''

Maji ya kunywa

Jamaa mmoja aliomba majiya kunywa, alipopewa akanywa. Alipomaliza akauliza maji yako matamu kweli ya umeyahifadhi kwenye mtungi nini?

Mwenyeji wake akajibu, ''hapana atii, haya ya mferejini''
Jamaa akashtuka ''mferejini?''
Yule jamaa akamjibu ''yakhe si bomba la maji kule Zanzibar twaita mfereji atii.
Ndipo jamaa akasema ''aanhaa kumbe, duh!''

Ajali

Mtoto mmoja alimuambia mama yake alipopigiwa simu: ''hujambo mwanangu?''
Mtoto akajibu ''sijambo mama ila nimepata ajali, na polisi wananifukuza hivi nnavyoongea''

Mama akashtuka na kumuuliza vizuri, ''eenh!! Unasema??''
Mtoto akaendelea kujibu, ''ndio hapa nyumbani kwenye video game''

Tuesday, August 10, 2010

Ndoto isiyoeleweka

Jamaa: Dokta nna tatizo, nikilala nasikia kitu uvunguni mwa kitanda. Nikichungulia nasikia juu ya kitanda.
Dokta: Noo mara mbili kwa wiki ofisini kwangu ntakusaidia kulitatua.

Jamaa: Itakuwa shingapi kwa kila nikija?
Dokta: Itakuwa elfu 30 tu.

siku chache baadae walipokutana mtaani.
Dokta: Mbona hukuja tena?
Jamaa: Nilipata mtu alinisaidia kumaliza tatizo lile.
Dokta: Alikusaidiaje sasa?
Jamaa: Aling'oa miguu yote ya kitanda kwa shilingi elfu 10 tu.

Monday, August 9, 2010

Nyama ya mbuzi

Kwenye sherehe ndogo nyumba fulani waliandaa party. Mzee mwenye nyumba akaagiza wachinje mbuzi.

Mwisho wa siku aliporudi nyumbani alipopita zizini akaona jambo... Akaanza kubwata alipoingia sebuleni, ''...mmeniudhi sana... Mi mesema mchinje mbuzi mmoja mmechinja wawili..." alifoka akafoka.

Mke: Mume wangu jamani ni mbuzi mmoja tu kachinjwa...
Mume: HAPANA SI KWELI...
Mke: Si kweli kivipi?
Mume: Si mmemchinja yule mbuzi wangu mjamzito...

Ajali na msaada

Gari moja lilipata ajali, mwanamke mmoja akawa wa kwanza kufika kutoa msaada.
Hata kabla hajaanza akatokea jamaa na kumsukuma yule mwanamke na kusema "pisha dada, nimesomea kutoa first aid.''

Yule mwanamke baada kama ya dakika 3 nae akanena ''ukifika muda wa kumuhitaji daktari nipo hapa''

Kwa mshauri

Mume na mke walienda kwa mshauri kuhusiana na matatizo ya ndoa yao. Walipofika, mwanamke akaanza elezea kwa muda wa dakika 15 kuhusu kero azipatazo.

Alipomaliza, mshauri akanyanyuka kwenye kiti akaenda akamshika yule mwanamke kwa kuonye anamjali, akambusu hapa na pale. Yule mwanamke akabaki kimya bila la kuongea.

Mume akauliza, ''umewezaje kumnyamazisha?''
Mshauri akajibu "unatakiwa umfanyie hivyo kila siku."
Mume akajibu "basi ntakua namleta kwako"

Sunday, August 8, 2010

Mitumbani

Kuna kaka mmoja alienda nunua nguo za mtumba akampatie mpenzi wake zawadi. Aliposagura sagura akakutana na kisketi kifupi.

Akauliza, ''khaa hii sketi mbona fupi sana...?
Akajibiwa na muuza mitumba ''aanha? Hicho si cha kuzimia tv tu nyumbani...''

MC

Lectural wetu alikuwa akikamata paper mbili mmedeseana (mmegezeana/cheat paper) alikuwa anaomba mje kuidentify the original..

Mtihani upi...?

Wakati nipo chuo siku moja lecture wetu wakati anasahisha mitihani, bahati nzuri/mbaya akakuta mitihani miwili inafanana majibu yake.

Akawaita wote wawili wenye mitihani husika, walipofika akawauliza ''upi original?''

Bar

Jamaa mmoja aliingia bar moja uko majuu. Alipofika akaagiza pale kaunta kichwaji kwenye glasi ndogo akanywa.

Alipomaliza akaambiwa bei yake ni sarafu (coin).
Kwa vile kaunta ni kubwa akaipiga na kidole sarafu moja mpaka mwisho wa kaunta upande wa kushoto, na nyingine upande wa kulia na ya mwisho akaiweka katikati ya kaunta (viti virefu). Kisha akatimua.

Mhudumu akamuangaliaa asijue la kumfanya.

Siku ya pili jamaa akaja tena akafanya vile vie.
Siku ya tatu pia... Akatoa noti wakati wa malipo na chenji inatakiwa zirudi Sarafu mbili.

Mhudumu akachukua sarafu ya kwanza akaiweka mwisho kabisa mwa kauta kushoto na ingine kulia. Ili tu ampe huyo jamaa usumbufu aliompatia siku mbili zilizopita.

Yule mteja alipoona vile akato sarafu na kuiweka katikati ya kaunta na kumuambia ''nipe glasi nyingine.''

Biashara

Jamaa mmoja nje ya duka lake aliandika tangazo dogo kwenye kibao. ''Mali mpya imeingia, Mali mpya imeingia... Wale wenye matatizo ya kutotabasamu wakiwa barabarani. Sasa tumewaletea tabasamu la kila aina toka China. Bei yetu ni nzuri. Karibuni sana.

Saturday, August 7, 2010

Mtoto ali...

Mtoto mmoja alimuuliza mama yake, ''mama kuna siku chache kabla ya kunizaa nilisikia mdundo wa mziki mkubwa, ulikuwa umeenda disko au kwenye harusi?''

Friday, August 6, 2010

Mlevi mlemavu

Mlevi mmoja alikuwa hana mikono aleinda Bar, kwa vile hakuwa na mikono yote miwili alikua akimuomba mhudumu amsaidie kumnywesha bia, kumfuta mdomo na kumtolea pesa ya kichwaji toka mifukoni mwa huyu asie na mikono.

Ikafika kipindi jamaa asiye na mikono akamuuliza mhudumu ''samahani msalani/chooni ni wapi hapa bar?''

Mhudumu akajibu, ''sisi hatuna choo we toka nje halafu kuna jengo hili ilipo hii bar la kwanza, la pili halafu utakuta choo.''

Basi mpaka ubungo

Abiria mmoja alipanda basi toka Arusha mpaka Dar, alipofika ubungo akamuambia konda hivi: ''konda tukifika ubungo naomba unishushe mule ubongo ndani stand ya mabasi ya mkoa''

Maisha ya alfajiri Dsm

Jamaa mmoja kwa vile anaishi mbali na katikati ya mji wa Dar es Salaam, ilikuwa inambidi kuamka saa 10 usiku ili saa 11 awe barabarani, na kwa sababu jiji la Dar lina foleni za magari kila kona, anajikuta nyumbani anarudi saa 5 usiku.

Siku moja aliporudi alipoingia sebuleni mwanae kwa vile hamuonagi mara kwa mara akasema hivi... ''mama... Mama... Kuna mgeni sebuleni.''

Pa kushushwa

Jamaa mmoja alipanda basi toka mbeya, alipokaribia karibia ubungo akiwa maeneo ya kimara akanyanyuka kwenye kiti chake na kwenda mpaka kwa dereva, kisha akamuambia ''dereva! Samahani unaweza ukanishusha kwanza hapo sinza halafu uje zako ubungo?''

Sinema kwenye basi

Abiria mmoja wakati yupo kwenye basi toka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine.
Aliangalia sinema waliyoekewa abiria wote alifika hatua akamsogelea dereva kwa vile alikuwa karibu nae akamuuliza.

''dereva, tangu tumetoka Mwanza na bado tupo njiani. Wenzio twaangalia sinema... Mbona wewe huangalii?''

Ajali

Marafiki wawili wa kiume walipata ajali, bahati nzuri hawakuumia kama ilivyo kwa gari.

Mmoja akamuambia mwenzake, ''kabla hatujalaumiana kosa la nani ngoja tushereke tumepona''
Mwenzake akajibu, ''kweli kabisa tufanye hivyo.''

Wakachukua chupa ya pombe kali kwenye gari haikuvunjika wa kwanza akanywa kisha akaifuta chupa na kumpa mwenzake nae anywe.."

Mwenzake akamjibu ''hapana ngoja kwanza mpaka trafiki polisi aje...''

Ajali

Marafiki wawili wa kiume walipata ajali, bahati nzuri hawakuumia kama ilivyo kwa gari.

Mmoja akamuambia mwenzake, ''kabla hatujalaumiana kosa la nani ngoja tushereke tumepona''
Mwenzake akajibu, ''kweli kabisa tufanye hivyo.''

Wakachukua chupa ya pombe kali kwenye gari haikuvunjika wa kwanza akanywa kisha akaifuta chupa na kumpa mwenzake nae anywe.."

Mwenzake akamjibu ''hapana ngoja kwanza mpaka trafiki polisi aje...''

Njia nyembamba

Dereva mmoja wa lori akiwa barabari akiendesha. Mbele akaona alama ya barabarani ikionyesha njia nyembamba mbele, na daraja dogo.

Alipokuja kuhamaki tayari alikuwa ameshakwama. Askari alipokuja akamuuliza ''we hukuona alama za barabarani?''

Jamaa akajibu, ''niliiona ila nimeishiwa tu mafuta ndio maana nipo hapa.''

Thursday, August 5, 2010

Kwenye mtihani

Mwanafunzi mmoja baada ya mtihani aliitwa na mwalimu wa darasa. ''wewe kwanini umefanya mitihani miwili?''

Mwanafunzi akajibu, ''hapana mwalimu mi nimefanya mmoja''
kisha mwanafunzi aliendelea kuelezea ''mwanafunzi mmoja alikuwa ananigezea labda amegezea mpaka jina langu.''

Jina...

Wanafunzi kwenye mtihani walipoambiwa aanze kufanya mti mmoja akamuita mwalimu msimamizi wa mtihani na kumuuliza, ''Mwalimu samahani, nimesahau jina langu.. Hivi naitwa nani vile?

Wednesday, August 4, 2010

Kwenda msalani

''naomba kwenda msalani...'' aliwaomba enzake aliokua amekaa nao.
Baada ya muda mfupi sana akarudi ''wenzake wakamuuliza "vipi mbona umerudi fasta hivyo? Au chooni kuna mtu?''

Jamaa akajibu ''nimesahau kikojoleo changu hamjakiona hapa?''

Mwendo wa kasi

Siku moja jamaa mmoja wakati anamsimulia jambo mwenzake, ghafla ikapita gari spidi kweli kweli.

Jamaa aliekimsimulia jambo mwenzake akasema ''khaa, ile gari ikipata ajali hata mponda majiko hatohitaji lile body la gari.''

Tuesday, August 3, 2010

Chupi ya chuma

Mwanaume mmoja alimchongea kufuli ya chupi ya chuma. Ili akienda masomoni amkabidhi rafiki yake awe mlinzi...

Siku ilipofika akampa rafiki yake kipenzi akamuambia aitunze mpaka atakaporudi.

Jamaa akawa anamkimbilia mwenye mke mda mfupi baadae... Akaulizwa... ''vipi kuna tatizo?''
Aliepewa fungua akajibu ''samahani umenipa ufunguo sio wenyewe.''