Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Friday, July 29, 2011

Polisi alimsimamisha Mzee mmoja akagundua kuwa amelewa huku akiendesha gari, akamuambia yule mlevi "shuka kwenye gari na usimame kwa mguu mmoja". Ili amjua kama stamina anayo au la!?

Yule mzee akamjibu "Askari nitolee wheel chair yangu nyuma kwenye gari kwanza"

Gundua

Jamaa mmoja alikua akinena "eti wazungu wamegundua mlima Kilimanjaro, kwa wachaga walikuwa wapi hapo awali?"
Kisha akaendelea kunena "juzi walimkamata mshkaji akiwa na gari isiyo yake, kumuuliza akajibu ameigundua kuwa ni gari lilikua limepaki"

Thursday, July 28, 2011

Kwenda nyumbani

Mwalimu alinena darasani
Mwalimu: Atakaejibu swali lifuatalo ndio ataenda nyumbani.
Mwanafunzi mmoja akatupa begi lake nje kupitia dirisha.

Mwalimu: Nani katupa begi nje?
Mwanafunzi akajibu: Mimi hapa mwalimu, naweza kenda nyumbani sasa?

Chizi na... Chizi na...

Jamaa alikua anachimba dawa (kubwa) kichakani, kidogo akatokea chizi ama kichaa na kumpora nguo zote. Kilichofuata jamaa akawa anamkimbiza huyo kichaa akiwa mtupu! Watu walishindwa elewa yupi kichaa kati yao wakabaki wakiwaangalia tu....

Watu wakasema wamepita machizi wawili hapa wanakimbizana lakini wa nyuma ndio anakichaa zaidi sababu amevua nguo.

Wednesday, July 27, 2011

Homework

Mwalimu alimuuliza mwanafunzi wake! "Wewe wapi homework niliyokupatia ufanya?"
Mwanafunzi akajibu "Mbona nishaifanya, nimei-upload facebook nikakutag angalia comments zinasemaje?"

Tuesday, July 26, 2011

Jamaa mmoja alisikika akilalamika "dah hili giza nchini mwetu si nimeoga maji ya kunywa badala ya yale ya kuoga!"

Mahari

Siku hizi kutokana na shida ya umeme kupamba moto ukienda kutoa Mahari unatajiwa jenereta.

TV

Wanafunzi shule ya msingi walipewa project ya kutengeneza luninga na vifaa vya nyumbani, Kila mmoja akatumia uwezo wake na akatengene za hiyo tv wengine wakatumia maboxi wengine debe za plastik nk

Mtoto wa SHAROBARO akaenda na karatasi ya A4 akaulizwa na wanafunzi wenzake "mshikaji hi tv kweli? Siutafeli hii project!" akajibu "plasma tv meen!!!"

Simu ya mke

Mwanaume mmoja alirusha kisu kuilenga picha ya mkewe ukutani, bahati mbaya akaikosa na kusema
"ooh I miss it"
Punde mkewe akapiga simu, Mke: Unafanya nini mume wangu?"
Mume akajibu "I missed you"

Monday, July 25, 2011

Majambazi kanisani

Majambazi walivamia kanisa, muda mfupi kabla sadaka zilitangazwa kua ni kiasi cha 15,750Tsh. Majambazi hayo yakaamuru kila mtu atoa alicho nacho cha thamani. Baada ya zoezi hilo zikatatikana takribani 7,000,000Tsh kisha jambazi mmoja wapo akasema "padre waumini wako sio kama hawana sadaka haya pesa hizi hapa tumekusa"
Wakampatia na kuondoka!

Maasai

Mmaasai mmoja alimuona rafiki yake akipita na dumu tupu, akamuuliza "rafiki naenda wapi na dumu?" Rafikie akajibu "naenda nunua maziwa ya ng'ombe"

Mmaasai kusikia vile akanena akimuambia rafikie "rafiki na tafundisha ng'ombe yangu kuusa masiwa"

Sunday, July 24, 2011

Nilikutana na watoto wawili wamebeba kisu na chumvi nikawauliza kulikoni? Wakanijibu "pale mbele kuna mti wa muembe, tukikosa kuna mwingine kwa mbele yake"
Jamaa mmoja alijenga nyumba maeneo ya uwashilini, siku moja alikua ghorofani kwako akachungulia nje akamuona mtu anaoga kwenye yale mabafu ya uswahilini passport, size akamuona mtu amejipaka sabuni usoni akiitafuta ilipodondokea jamaa ghorofani akanena kwa sauti " Sabuni ipo unande wako wa kushoto"

Saturday, July 23, 2011

Ndege

Katoto kamoja kalionda ndege inapita angani kakaanza kusema kwa staili kama ya kuimba "ndeege ndeege ndeege ndeege" akaskuti akahisi kama anakosea akabadilisha na kusema "airplane airplane airplane..."

Friday, July 22, 2011

Ratiba ya umeme

Jamaa mmoja anaefanya kazi shirika la umeme alimuuliza jirani yake "kwani wewe huna ratiba ya umeme mpaka ulalamike kukatwa katwa?"
Jirani nae akajibu, "ratiba yenyewe imetolewa copy, halafu kumbe si ya mtaa wetu ntajuaje sasa?"

Mume kafa

Mke alienda Jerusalem na mumewe ki-vekeshen vekeshen.
Mumewe akafa bahati mbaya, akaambiwa kusafirisha mwili itamgharimu dola 1,000 na kuzika nchini humo dola 100.

Akachagua kusafirisha, mchungaji akamuuliza "huoni ni gharama kubwa sanakusafirisha?"
Mke akajibu: Mara ya mwisho Yesu alizikwa hapa akafufuka siku ya 3, mi sitaki mume wangu afufuke"

Muda kurudi

Mwanamume mmoja akimuambia mkewe kwenye sms "mke wangu narudi nyumbani muda si mrefu namalizia bia ya mwisho, ukiona sijarudi bado soma tena msg hii"

Wednesday, July 20, 2011

Kampuni ya inshuarensi

Ajenti wa kampuni ya inshuarensi: Mzee, pia tunatoa inshuarensi ya uume.
Mteja: Mnafanyaje yani? Mna-replace na uume mwingine ama?
Ajenti: Hapana, inakua kama haufanyi kazi tena tunatoa huduma bure kwa mkeo.

Tuesday, July 19, 2011

Bilionea

Mvulana: Baba yangu ni bilionea na ana miaka 93, karibuni tu atakufa, je utakubali kuolewa na mimi?
Msichana akajibu: Hapana, sitaki.

Week baadae yule msichana akaolewa na huyo baba ake mvulana.
Mvulana akanena: Shenzi kabisa, usitoe wazo kama hili kwa mwanamke...

Msibani na siasa

Mwanasiasa mmoja alienda hudhuria msiba, na kwa vile alikuwa mtu maharufu eneo hilo alipata wasaa wa kunena jambo kuhusu rafiki yake marehemu hali ikawa hivi alipoanza kunena jambo "msiba oyee?"

Monday, July 18, 2011

Malaika

Mtoto mdogo wa kiume kamsimulia mama yake: 'Mama unafahamu kuwa dada (house girl) kumbe ni malaika? Mama kwanini unasema hivyo mwanangu?

Mtoto: Nilimwona akiwa uchi mkono ameshika ukutani akisema mungu wangu nakuja, nakuja kama baba asingekuwa amemshikilia kwa nguvu kwa nyuma angeweza kupaa juu mbinguni.

Vidonge

Mama mmoja alimuuliza mumewe "mume wangu zile dawa zangu zilizokua hapa ziko wapi?
Baba kabla hajajibu mtoto akadakia "mama nimempa mbwa wetu ameza nilisikia ukimuambia baba ni vidonge vya majira, mbwa wetu ana mabwana wengi vitamsaidia"

Sunday, July 17, 2011

Namba mpya

Mwanamke mmoja alimpigia mumewe na simu asiyoijua! Katikati ya maongezi mwanamke akamuuliza mumewe "unajua unaongea nani?"

Mwanaume kuogopa asije akataja baadae akaulizwa huyo mwanamke uliomtaja ni nani mumewe akajibu "naongea na Juma au?

Friday, July 15, 2011

Kwa mganga

Jamaa alienda kwa mganga, baada ya kufanyiwa tunguli za kutosha mganga akampa dawa ya kuila ili huyu alie na shida imsaidie!
Mpewa dawa akamuambia mganga "mganga hii dawa haina tatizo?"
Mganga akajibu "sijui, nenda kaijaribu. Kama haina madhara ntaitumia kwa wengine"

Betri low

Jamaa kaoa na ana kimada cha nje pia ikawa kila akipigiwa simu na kimada wake, mkewe huchukuwa sim na kuiweka kwenye charge sababu amelisave jina la huyo kimada wake BATTERY LOW!

Thursday, July 14, 2011

Kibweka msibani

Jamaa aliacha mpya msibani, alipofika na kukuta wafiwa wanalia akanena "msilie jamani marehemu kani-text muda si mrefu na yeye anakuja msibani"

Sharobaro

Masharobaro wengi walikufa gongo la mboto kutokana na majibu yao. Lala chini bomu hlo "ntachafuka men"
Panda lory" nasubiri taxi men
"Zima simu" naongea na baby men''
"Nenda uwanja wa taifa" naogopa mbu men!
Hayo ndo majibu wakati wa purukushan za kujiokoa.

Saturday, July 9, 2011

Idadi ya kuku

Mwalime: Wekesa nikukupatia kuku mbili tena baadaye nikupe zingine mbili kwa ujmala utakuwa na kuku ngapi?

Wekesa: Tano!

Mwalim : Kweli wewe mjinga

Wekesa: La hasha tiyari niko na moja nyumbani!

Wapi blauz?

Mama mwenye nyumba alipoitafuta blauzi yake bila mafanikio akamuuliza mfanyakazi wake (dada) wa ndani: "dada nguo yangu ya pink pink ipo wapi naitafuta siioni?"

Dada nae akajibu "sijui mama ipo wapi?"
Mama: Nimefanya makusudi kukuuliza nilikuona umeificha.
Dada: Na mimi pia niliificha makusudi.

Tuesday, July 5, 2011

Muwa, Uyoga na Ndizi

Muwa uliongea: Niangalie naonekana kama mti.
Uyoga nao: Niangalie naonekana kama mwavuli.
Ndizi nayo ikasema: Tubadilishe hili somo.

Cheka unenepe

Muwa uliongea: Niangalie naonekana kama mti.
Uyoga nao: Niangalie naonekana kama mwavuli.
Ndizi nayo ikasema: Tubadilishe hili somo.

Sunday, July 3, 2011

Mbwa na mzungu

Mzungu mmoja alikua anafanya matembezi ya jioni akiwa na mbwa wake akakutana na vibaka wawili, sasa kwa sababu ya mbwa kama wale wa polisi. Kilichofuata kwa vile wakiogopa mbwa walimuambia mzungu "we mzungu tunataka kukupora simu tunaiomba."

Mlo haraka

Jamaa alienda hotelini na rafiki yake wakaagiza chakula wakaanza kula:
Punde akamuuliza mwenzake, "mbona unakula haraka hivyo?"
Jamaa akajibu: Kabla sijapoteza hamu ya kula.

Mapenzi Mapenzi

Kabla ya ndoa, mwanaume atadanganya kuchelewa kulala akimuza mchumba wake au walichokiongea kuhusu mapenzi yao.
Baada ya ndoa: Mwanaume atalala usingizi kabla hujamaliza kuongea.

Siku ya uhuru

Jamaa alituma meseji kwa rafiki zake woote wa kwenye listi iliyo kwenye simu yake ya mkononi akiwatakia siku ya kufurahia uhuru wa nchi yao, meseji iliandikwa hivi "If you are married please potezea hii meseji, happy independence day"

Kushikana mikono

Jamaa mmoja alimuuliza mwenzake jambo "hivi kwa nini wapendanao wanashikana mikono wakati wanafunga ndoa?"
Jamaa mwenzake akamjibu "kawaida ni kama vile mabondia wanavyoshikana mikono kabla ya ngumi kuanza"

Maisha marefu

Mwanaume: Kuna njia yeyote ya kua na maisha marefu?
Dokta: Funga ndoa.
Mwanaume: Unadhani itasaidia?
Dokta: Hapana, itasaidia kupunguza mawazo ya kua na maisha marefu.

Homework

Mwalimu: Homework yako ipo wapi?
Mwanafunzi: Nimeipoteza wakati napigana na huyu hapa aliekisema wewe sio mwalimu bora hapa shuleni.

Mr. na Mrs.

Mwanaume alisimamishwa na trafik:
Trafik: Mzee unajua kua ulikua spidi sana?
Mwanaume: Hapana.
Mke: Nilimuambia mimi apunguze spidi mbishi.

Mume akimjibu mke: Kelele, hayakuhusu ntakunasa vibao sasa hivi.
Mke: Na leseni pia nimeimba wee hajachukua.
Trafik anaenda muuliza mke "eti mama anakujibu ivi siku zote?"
Mke akajibu: Hapana mpaka akiwa amelewa.

Malavi davi

Vizee viwili vilikua wapenzi kwa miaka mitano, siku moja mzee akatangaza nia ya kumuoa bibi. Siku iliyofuata akaamka asikumbuke jibu gani alipewa. Akampigia simu yule bibi ajue, bibi kwenye simu akajibu "afadhani umepiga, nakumbuka nilijibu ndio ila nilikua sijui nani niliemjibu hivo"

Saturday, July 2, 2011

Sumu

Jamaa mmoja alitengeneza sumu kisha akamuambia mwenzake ambae ni rafiki yake "aisee sijui kama hii sumu ni kali, ngoja niionje halafu kama sio kali niendelee kuitengeneza iwe kali zaidi"

Mwizi

Kibaka mmoja usiku alienda kuiba cha kuiba, akafika akafungua boneti ya gari akiwa anajua mwenyewe kichwani mwake anachokuja kuiba. Wakati ameishikilia boneti ya gari mikono yote miwili juu mwenye gari na nyumba alikua akimchungulia tu....

Kisha akamuuliza kupitia dirishani yule mwizi "ya kwaakoo?"
Kilichofuata yule mwizi aliachia boneti mbio alizotoka kwenye fensi ya michongoma sijui alipitaje maana geti lilikua limefungwa.... Ila alikimbia ukabaki unacheka tu picha nzima ikivyo kawa....