Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Thursday, November 8, 2012

Mgeni huyu...

Wageni wengine noma...........!!!!!!!! MWENYEJI: "Utakunywa soda au chai?" MGENI: "Ntakunywa soda wakati nasubri chai ichemke!....."

Tuesday, October 9, 2012

Kambi ya jeshi

Jamaa alikatiza kambi ya jeshi. Akapewa adhabu ya kubeba tofali 1,000. Alipofikisha 900 akakumbuka mkuu wa kambi kasima nae, akaenda msemea aliempa adhabu: mkuu akanena "umeshabeba mangapi hadi sasa?" Jamaa akajibu "900" mkuu akanena "basi yarudishe halafu uendelee na safari yako."

Taxi na ofa

Jamaa kwenye taxi alimuona mke wake anaingia hotel na njemba akamuambia taxi driver "unataka tengeneza laki 2 sasa ivi?" Akajibu "ndio" akapewa kazi akamchukue mke wa jamaa amlete. Akarudi na mwanamke sie jamaa akanena "huyu sio mke wangu" taxi driver akanena "najua! Huyu ni mke wangu mshikilie namfuata wako sasa."

Monday, October 8, 2012

Dokta na mgonjwa wake

Daktari mmoja alienda wodini akamkuta mgonjwa wake amelala usingizi maongezi yakawa hivi baada ya kumuamsha "nimekuja kukuletea dawa ya usingizi hii hapa kunywa"

Friday, September 21, 2012

Mjamaika na ndoa mpya

Mjamaika (Rasta) mmoja alikua anafanya mapenzi kwa mara ya kwanza na mkewe. Ghafla akasema kwa sauti kubwa na kutoka mbio chumbani alipokuwa, akarudi na maji kwenye jagi na kuamwagia eneo tamu la mkewe(Ukeni. Mke kwa ukali akafoka "watta gwan what you rasta man do that for?" Janaume likajibu (Rasta) "this thing too sweet me wanna dilute it. Remember am diabetic and sweet thing not good for me rasta man."

Dunia kwishneii

Kaka wakati anafanya mapenzi na dada ake waliponogewa dada akasema "Mhh Unan... vizuri kuliko baba" Kaka nae akanena "Hata mama nae kasema ivo ivo"

Vibweka vya mapacha

Mapacha wawili walipenda kula kuku na chips siku moja katika maongezi yao pacha wa kike akamuambia wa kiume "Kuku wameniambukiza manyoya." Pacha wa pili kiume akanena "nionyeshe" yule wa kike akamvulia na kumuonyesha akaona vinywele vimeota. Yule wa kiume akavua na yeye akisema "ona hata mimi wameniambukiza" Pacha wa kike anamalizia kwa kusema "Wamekuambukiza vibaya mpaka firigisi."

Kaaazii ipo...

Njemba baada ya kuchoka fanya kazi zake nyumbani akazima taa akalala. Punde akaona mtu kasimama pembeni akauliza "we ni nani chumbani kwangu" Akajibiwa "mimi malaika." Njemba ikauliza ina maana "nimekufa, mbona bado kijana nirudishe duniani bado nna nafasi..." Malaika akamjibu "labda tukurudishe kama mbwa au kuku, njemba ikaona bora kuwa kuku, akiwa bandani akaanza hisi anawashwa nyuma, jogoo akamuuliza "unajihisi kama unataka kutaga?" akajibu ndio. Basi jogoo akamuambia "chuchumaa utoe mayai utamie" Akawa anafanya ivo akijikamua ghafla akastukia kapigwa kibao na mkewe "wewe (kwa sauti ya ukali) ni nini unakunya kitandani?"

Thursday, September 20, 2012

Nani wa kuja kati ya...

Nani mshamba kati ya hawa hapa? 1. Aleenda shop kuulizia bluetooth. 2. Aliekula hotelini akaosha vyombo. 3. Alienunua Ice Cream akaipasha moto. 4. Aliemuamkia mtu kwenye TV. 5. Alieenda bank kununua sabuni.

Tuesday, September 18, 2012

Faini ya mwizi

Mume kamfumania jamaa fulani akifanya mapenzi na mke wake, akamtoza faini ya 500/= Yule jamaa akatoa fastafasta noti ya 1000/= Mume akasema,"Kesho njoo umgonge tena...mi sina change!!"

Hasira mmbadala

Mke alimwuliza mmewe "ambona mume wngu nikikuudhi huwa hukasiriki?" Mumewe akajibu "huwa ukiniudhi nachukua mswaki wako na kusugulia chooni"

Nani zaidi?

Jamaa: I love you sweet. Msichana: I love you too...ila tupendane tu,mambo ya ngono sitaki namtunzia mume atakaenioa. Jamaa: Hilo si tatizo,na mimi mambo ya kuniomba pesa sitaki namtunzia mke nitakaemuoa!

Wednesday, September 12, 2012

Kichaa jalalani

Kichaa mmoja alikutwa jalalani.
Jamaa akamuuliza wewe mbona ukohapa wakati wenzio wapomilembe?
Akajibu wale wako boding mimi nipo day

Thursday, September 6, 2012

Nani azaidi?

Jambazi kaoa mwanamke mchawi, mtoto alipozaliwa nae akawa changudoa. Swali ni je nani atabaki nyumbani usiku?

Mwizi wakati anatoka...

Mwizi mmoja aliingia nyumba moja kuiba, sasa wakati anatoka mtoto wa mwenye nyumba asiependa shule akamshika mguu na kumuambia yule mwizi "usipochukua na begi langu la madaftari ya shule napiga kelele"

Saturday, September 1, 2012

Kibaka na polisi

Polisi walikua wakimkimbiza kibaka usiku, kibaka kuona hivyo akakimbilia kunako makaburi.
Alipowapotea akavua nguo na kukaa juu ya kabuli, polisi walipofika akaulizwa "aroo hujaona kibaka akipita hapa?"
Kibaka akajibu "mie mwenyewe mgeni hapa nimezikwa jana tu, labda uwaulize hao waliolala."

Friday, August 31, 2012

Kitu cha posa...

Jamaa alienda kuposa kwa mzee mmoja.
Mzee: Umekuja kuposa huku unatafuna big g!!?
Jamaa: Natoa harufu ya sigara.
Mzee: Yani unavuta sigara!?
Jamaa: Vile nikitoka kilabu kulewa tu.
Mzee: Unalewa!?
Jamaa: Nilianza kulewa nilipokuwa jela.
Mzee: Yaani na kufungwa pia!?
Jamaa: Ah niliua mtu.
Mzee: Duh kumbe wewe muuaji!?
Jamaa: Ah, si kuna mzee nilitaka kumposa mwanae akanikatalia, mimi nikamuulia mbali.
Mzee: Karibu baba, unataka harusi lini? Mimi sina tabu, mke mkeo uyu! Na mahali utaleta ukipata haina shida.

Thursday, August 30, 2012

Wizi Vs. mkwara

Jamaa mmoja alimuibia nauli mzee kwenye daladala..
Mzee: jamani alieniokotea nauli yangu airudishe kabla sijafanya nilichofanya mwaka 1947. Kijana kwa kutetemeka akarudisha hela ya babu alafu akauliza kwani babu ulifanya nini mwaka 1947 Mzee akajibu nilitembea kutoka mbagala mpaka posta.

Tuesday, August 28, 2012

Nani atupe...

Ndani ya meli,watu makabila tofauti walikua na mizigo,meli ilizidiwa ilibidi mizigo ipunguzwe,Mzungu akatupa computer, akasema"kwe2 zpo tele,Mchina akatupa box la cmu akasema"kwetu zipo tele" Muhindi Akamwaga kiroba cha tambuu akasema kwetu zipo kibao, Mmasai akatupa shanga.. Mchaga anahaha hajui atupe nini kila kitu chake anakionea uchungu ,ghafla alimtumbukiza Mmasai akasema"Yesu na maria hawa wapo tere ARUSHA"

Sunday, August 26, 2012

Kwa Dokta

JANE:"Daktari,kila mara baada ya kukojoa mwisho wa mkojo hutoka rangi ya brown." DAKTARI:"Mmmh,h uwa unafanya mapenzi mara ngapi kwa siku?" JANE:"Hee,ati siku! Mi hufanya mara mbili kwa mwaka dokta." DAKTARI:"Huo si ugonjwa ni kutu!"

Saturday, August 25, 2012

Mchungaji nae

MCHUNGAJI: Mgeukie jirani yako na umwambie Mungu yumwema, WAUMINI wote wakageukiana na kusema Mungu yumwema, MCHUNGAJI: Leo nitawaombea wale wote wasio zaa,mgeukie mwenzio na umwambie leo utapata mimba, mara likasikika bonge la kofi siti za nyuma! Kumbe mtoto 1 alimgeukia baba yake na kumwambia leo utapata mimba.

Wednesday, August 22, 2012

Pete ya dhahabu

Dada mmoja aliingia duka la urembo, akaona pete 1 ya dhahabu, wakati akiisogelea aione vizuri, bahati mbaya akajamba, akaangalia pande zote kama kuna mtu kamsikia, alipogeuka nyuma akakutana macho kwa macho na muuzaji. Kwa aibu akazuga akamuuliza muuzaji hii pete unauza shilingi ngapi? Muuzaji akamjibu "kuiona tu umejamba, je nikikutajia bei si utakunya hapa hapa?"

Tuesday, August 21, 2012

Mkristo na futari

Ivi unafaham... Mkristu kavamia futari vuuuupu. Baada ya kula Sheikh akamchagua asome dua ya kushukuru! Jamaa kataka kuingia mitini ila akajikaza kiume na kuanza kama ifuatavyo: Jamaa:Ya Tawfiq. Watu:Amin. Jamaa:Ya Habib. Watu:Amin. Jamaa:Ya Shabiby. Watu:Amin. Jamaa:Ya Abood. Watu:Amin. Jamaa:Ya Hood. Watu:Amin. Jamaa:Ya Scandnavia. Watu:kimya! Jamaa:Ya Ngorika. Watu:Mhhhhhhh! Jamaa:Ya Dar Express! Watu:Aaaaa, chezea sisi kamata tia bakora mwanaharamu huyu!

Utambulisho

Semina Ubungo Plaza... watu wakaanza kujitambulisha, Wa kwanza: Mimi naitwa John niko UDOM mwaka wa pili nasoma LAW. Wa pili: Mimi naitwa Stella niko UDSM mwaka wa 3 nasoma PUBLIC RELATION. Wa tatu: Kwa kusuasua sana huku akijishtukia, mimi naitwa Paul niko TANESCO mwaka wa4 nasoma MITA!!

Thursday, August 16, 2012

Kichaa juu ya mti

Siku kichaa mmoja alipopanda juu ya mwembe asubuhi akakaa huko mpaka jioni, kisha ilipofika jioni akajiangusha chini mzima mzima
Daktari wa wagonjwa akili akamuuliza "mbona umejiangusha?"
Yule Kichaa akajibu "Nimeiva tayari"

Tuesday, August 14, 2012

Simu ya nani?

Jamaa mmoja alipanda kwenye gari, wakati wapo safarini dereva wa ile gari akawasha redio, kwa vile ilikuwa na sauti ndogo na spika zake ndogo yule aliyepewa lifti akajikuta akipayuka bila kujua "simu ya nani hiyo inaita muda mrefu?" asijue kuwa ni mziki toka kwenye redio.

Baba mbali na familia

Mzee mmoja alikua anafanya kazi mbali na familia yake, siku moja alipata likizo akarudi kuwa karibu na familia yake. Alipoika mtoto wake akamuuliza mama yake "mama huyu nani?" mama nae bila hiyana akajibu "ni baba yako huyu" Mtoto akahoji tena "sasa na yule anaelalaga chumbani kwako kama baba hayupo sio ndio baba yule?"

Thursday, June 21, 2012

Baba na Bintie

Binti: Hi Baba Baba: Hi binti yangu? Binti: Nimempenda huyu mlinzi wa hapa nyumbani na nimeamua kutoroka nikaolewe nae Baba: Pumbavu kweli wewe unadhani nitashtuka? Safari njema na nisione sura yako tena hapa! Binti: Samahani baba... Nilikuwa nakusomea barua aliyoacha mama Baba: Umesema.????.!

Monday, June 18, 2012

Mlinziiii

Binti: Hi Baba Baba: Hi binti yangu? Binti: Nimempenda huyu mlinzi wa hapa nyumbani na nimeamua kutoroka nikaolewe nae Baba: Pumbavu kweli wewe unadhani nitashtuka? Safari njema na nisione sura yako tena hapa! Binti: Samahani baba... Nilikuwa nakusomea barua aliyoacha mama Baba: Umesema.????.!!

Mpenda mpira

Jamaa mpenda mpira kajichora tattoo mwilini mwake majina ya vifaa vya michezo, demu wake akawa anayasoma. kifuani NIKE pajani REEBOK, mgongoni PUMA kiunoni UMBRO matakoni FIFA, kwenye uume AIDS, msichana akashtuka kwa nini umeandika hapa AIDS jamaa akamwambia usiogope imelala tuu ikisimama patasomeka ADIDAS!

Jogoo

Jogoo alimkimbiza jike huku akiwaza nikimpata ataipata nikimkosa nitazuga nafanya zoezi, jike aliwaza nikisimama nitaonekana malaya nikikimbia nitalala na hamu ya kufanya.

Friday, June 15, 2012

Swali gumu

Mtoto alimuuliza baba ake aliporudi nyumbani akamuuliza "eti baba na wewe una nywele huku karibu na kitovu?" Baba kwa mshangao "wee mtoto umeona wapi hizo nywele?" Mtoto akajibu bila wasi wasi "baba mi meuliza tu maana yule anko anaekuja kwa mama ukiwa haupo nlimuona anazo"

Wazo la mtoto

Mtoto akimuambia baba yake pale sebuleni kwao palipokuwa na tanki dogo la kioo la kufugia samaki. Mtoto "baba mi naona kama hao samaki wana kiu si uwaekee maji ya kunywa!"

Tuesday, June 12, 2012

Kipigo icho

Mwanaume alienda kwa daktari wake ikawa hivi: Mwanaume: Dokta, mke wangu ananitwanga mangumi mno. Dokta: Kivipi na kwa nini haswa? Mwanaume: Mara zote anikutapo chumbani kwa house girl.

Semea mbovu

Mwanamke akimsemea mbovu bwana ake kwenye simu "mtu mwenyewe huna ishu, kwanza sio type yangu..." Mwanaume akajibu: Mpenzi wangu kwani vipi? Nipo bank kwa sasa... Mwanamke kusikia ivyo akanena "ohh mpenzi basi uje na laki moja nimeishiwa kitu..."

Sunday, June 10, 2012

Wazaramu

Wazaramu walimkamata mwizi wakamuweka mtu kati wakamsema weee mpaka mwizi akafa.

Wednesday, June 6, 2012

Faini ya kukojoa

Polisi alimdaka jamaa anakojoa pembezoni mwa ukuta. Polisi: Wewe unajua panakatazwa kukojoa hapa? Jamaa: Sasa nimebanwa nifanyaje? Polisi: Faini yake elfu tano. Jamaa akatoa noti ya elfu 10. Polisi: Sasa chenji tunaipataje? Jamaa: Tafuta chenji unipe changu. Polisi: Basi kojoa tena...

Wednesday, May 30, 2012

Ajali ilivyotokea

Trafiki polisi akihoji palipotokea ajali "ahaa! Sasa naanza elewa embu nielezee jinsi ajali ilivyotokea wewe ukiwa kama dereva mhusika." Dereva akajibu "hata sikumbuki nlifumba macho"
Mwanaume kwenye simu "dokta, mke wangu ameanza kuwa anafikira kama sungura...." Dokta akajibu "ihh mlete hospitali nimcheki. Mume akanena "dokta vyovyote itavyokuwa usimpe tiba lakini.

Dawa yake

Mume alizoea kila mara akirudi usiku ananyimwa unyumba na mkewe kwa kisa anaumwa kichwa. Siku mume akarudi na moja kwa moja akampelekea panadol mbili na maji, mkewe akanena "nani kakuambia naumwa kichwa?" Mume akajibu "yes nimekukamata leo"

Mshtuko wa moyo

Mume karudi akasikia sauti asiyoielewa toka chumbani kwake, akaenda na kukuta mkewe analalamika amepata mshtuko wa moyo. Mbio anaenda sebuleni kupiga simu kuomba msaada. Punde mwanae akaja "baba anko Jose kajificha kabatini kwako uchi" mzee mbio mpaka chumbani. Fungua kabati akamkuta ndio na kumuambia "wee mke wangu anapata mshtuko wa moyo we umejificha tu uchi humu unawatisha watoto, njoo tumpe msaada haraka."

4WD

Mwanaume alimnunulia pete ya almasi mkewe, rafiki akauliza "si ulisema anapenda gari yenye four wheel drive, mbona umenunua pete?" Mume akajibu "unadhani wapi ntapata rav4 feki?"

Ya leo mgonjwa

Dokta alipotembelea wodi ya mgonjwa wake aliepata ajali. Mgonjwa akiwa amening'inizwa mikono juu akauliza "dokta ntaweza kweli kupiga kinanda nkitoka hospitali?" Dokta: Bila shaka utaweza, wewe ni mpiga kinanda mzuri enh? Mgonjwa: Hapana sijawahi kabisa bado.

Sunday, May 27, 2012

Pombe basi

Cha pombe alikunywa sana pombe akataka ongeza mhudumu akamjibu "hapana imetosha sasa umekunywa saaana." Mlevi akajibu "nimeanza kunywa miaka 36 ilopita sijawahi jua kama metosheka wewe umejuaje?"

Kwa mama lishe

Jamaa kwa mama lishe baada ya kula wali nyama akaletewa vijiti vya kutolea nyama kwenye meno. Vilipofika tu mezani kwake akahoji "vimechemshwa hivi? Maana kipindupindu nje nje."

Saturday, May 26, 2012

Wasiwasi

Dogo akimuongelesha mama yake aliepo sebuleni yeye akiwa jikoni "mama!" Mama nae akaitikia "ooh mwanangu" Mtoto: Unaikumbuka ile sahani inayokupa wasiwasi isije niteleza ikavunjika siku moja. Mama: Ndio mwanangu. Mtoto: Basi wasi wasi wako umeisha leo.

Swali jibu tofauti

Mwalimu aliuliza wanafunzi wa darasa la 3 wakike kwa kiume "mlikuwaje hapo awali kabla hamjawa hivi mlivyo leo wanafunzi?" Mwali akisubiria jibu akitaraji watajibu "walikua wadogo" wanafunzi wao wakajibu "tulikua na furaha, wengine wakilia nk"

Home work

Mwalimu: Haya James iko wapi homework yako? Mtoto: Mwalimu ilmeliwa na mbwa wetu nyumbani. Mwalimu: Nimefundisha kwa miaka 18 sasa, unadhani nitaamini hilo? Mtoto: Ni kweli mwalimu nimemlazimisha mpaka kaila.

Friday, May 25, 2012

Mbio za ushindi

Baba: Wewe Japhet hiyo saa umeipata wapi? Mtoto: Neshinda mbio ndio nkaipata. Baba: Hizo mbio mlikua na akina nani? Mtoto: Alikuwepo polisi, mwenye saa na mimi.

Fala wa kwanza

Mume: Unaniambia walikutongoza wanaume wanne ili wakuoe? Mke: Ndio hivo hivo kama ulivyosikia. Mume: Bora hata ungeolewa huyo fala wa kwanza kati ya wote waliokutongoza. Mke: Ndio nlivyofanya hivyo.

Thursday, May 24, 2012

Mwizi wa atm

Jamaa aliibiwa kadi yake ya benk akaulizwa kama ameripoti polisi akajibu "sijaripoti bado, mwizi mwenyewe hamfikii matumizi kama mke wangu"

Kifamilia zaidi

Mke na mume wakiongelea suala la fedha kifamilia: Mwanaume: Sikiliza isingekua fedha hii nyumba isingewepo. Mwanamke: Na wewe sikiliza isingekua fedha zako nisingewepo hapa.

Wednesday, May 23, 2012

Hii nayo

Mvulana: Nilimuita boifrendi wako shoga, si akanipiga na pochi yake.

Bia

Mama akisimuliwa na mwanae wa miaka saba "mama tulienda bar na dada, akajisikia vibaya na kushindwa kunywa bia yake. Ikabidi mimi ndio niinywe."

Tuesday, May 22, 2012

Jamaa alinunua friji jipya la zamani akaliweka nje na kuandika "friji hili ni bure nalitoa" zikapita siku mbili hamna alieamini yale. Siku ya tatu akaandika "friji hili lauzwa laki mbili" usiku wake likaibiwa.

Monday, May 21, 2012

Msaidie mwenzako

Jamaa mmoja alikua anamrekodi mwenzake kutumia video camera huku mhusika akicheza na moto. Ghafla moto ukashika shati la jamaa... Mpita njia akamuambia mwenye camera "wewee acha kamera muokoe mwenzako..." Mwenye Camera akajibu "kaniambia nimrekodi tu sasa mi nifanyaje?"

Saturday, May 19, 2012

Cheka kidogo

Njia rahisi kusahau matatizo yako (japo kwa muda mfupi) vaa viatu vinavyokubana.

Wednesday, May 16, 2012

Mlizi mbio mbio

Tulikuwa bar moja jana mlinzi kaingia spidi, akamwambia jamaa mmoja aliyekaa kaunta, Mlinzi: Mzee gari lako limeibiwa Mzee: Umemtambua aliyeiba? Mlinzi: Hapana lakini nimeandika namba za gari hizi hapa.

Hakimu & hongo

Kesi imeanza hakimu kakaa kwenye kiti chake akatangaza; Hakimu: Mlalamikaji na mtuhumiwa wote mmeniletea hongo niwapendelee. Mlalamikaji umenipa laki moja, mtuhumiwa umenipa umenipa laki moja na hamsini. Sasa nawarudishia hii hamsini elfu ili nisiwe na sababu ya kumpendelea mtu. Tunaendelea...

13, 13...

Jamaa alikuwa anapita nje ya wodi ya vichaa akasikia mtu anesema, 13, 13, 13, 13, 13, 13,..... akaamua kuchungulia kwenye kitundu alichokiona ajue kuna nini, ile kuchungulia tu akamwagiwa mchanga wa machoni, sauti ikabadili ikaanza 14,14,14,14,14......

Ushauri wa dokta

Jamaa alikuwa anaumwa sana mkewe akamwita daktari, alipofika akamkuta jamaa kafumba macho; Dokta: Huyu mbona amekwisha kufa Jamaa: Sijafa bwana Mke: Hebu nyamaza bwana acha kubishana na wataalamu.

Mume anaenda kazini

Jamaa kaamka asubuhi sana Jumamosi, mvua inanyesha kang'ang'ania kuwa anaenda ofisini. Kawasha gari yake, kufika njiani hali ilikuwa mbaya kaamua kurudi. Kafika home kavua nguo kaingia tena kitandani, kamnong'oneza mkewe aliyekuwa usingizini; "Yaani hali ya hewa huko nje mbaya sana" Mke: Si ndio nimemshangaa huyu mpumbavu eti kaenda kazini.........

Friday, May 11, 2012

Mama aliporudi

Mtoto "mama afadhali umerudi baba yupo nyumbani na anti, baba kamlalia anti kwa juu wote wanapiga kelel sijui wanaumwa nini mimi meshindwa wasaidia

Simu ya tochi

Jamaa mmoja alikua na simu yenye tochi Po. Kwenye kagiza giza rafiki yake akaiomba awashe kumulikia mwenye simu akamjibu "aahh usiiwashe itamaliza vocha yenyewe kimeo"

Wednesday, May 2, 2012

Kitana mapengo

Dukani: Nikusaidie nini kaka? Mteja: Kitana changu vile kichanio kimevunjika. Dukani: Sasa si kimoja tu vilivyobaki vingine si vipo. Mteja: Hapana kilichovunjika ndio cha mwisho kabisa.

Hasira za mtoto

Baba na mtoto: Baba: Mwanangu ukiwa na hasira unafanya nini? Mtoto: Naenda chooni. Baba: Chooni? Kufanya nini? Mtoto: Kusafisha. Baba: Halafu ndio hasira zinaisha? Mtoto: Ndio nasafisha choo kwa mswaki wako.

Duka la tai

Jamaa alienda nunua tai alipofika ikawa hivi: Muuza duka: Karibu, nikusaidie nini? Mteja: Natafuta tai iliyochanganyika na maziwa na kahawa hivi. Muuza duka: Sijajua na sukari je au hutoitaji?

Tangaza ndoa...

Njemba ilienda kutangaza ndoa: Njemba: Mzee mimi nataka kumuoa mwanao. Mzazi: Unafanya nini kusukuma siku? Njemba: Nakaba, kupora na kubaka. Mzazi: Mbona vyote na hasi huna hata moja chanya? Njema: Ohh! Chanya nina HIV +ve.

Friday, April 27, 2012

Diet

"Kaka nasikia siku hizi unafanya diet" kijana mmoja akimuambia rafiki yake aliekua mnene mnene kidogo" Papo hapo jamaa mmoja mingine kati yao akadakia "mhh! Labda afanye diet ya kunywa bia"

Wednesday, April 25, 2012

Mkopo huo

Jamaa akimshushua mwenzake "mshkaji wangu we tatizo unakopa sana, chuupi unakopa, maji unakoopa, mwanamke ukienda nae gesti unakopa pia" Jamaa akajibu: Sasa hali tete mie nifanyeje?

Tuesday, April 24, 2012

Kibweka cha leo

Soma hii ucheke kidogo: KESHO KUNA MAANDAMANO YA WEZI WANATAKA WAONGEZEWE SIKU, BADALA YA SIKU ZA MWIZI NI 4O, SASA ZA MWIZI ZIWE 60. UKIPATA UJUMBE HUU WATUMIE NA WEZI WENZIO WOTE.

Friday, April 20, 2012

Mgonjwa na Dokta

Mgonjwa: Dokta nimekuja nahisi nna umwa malaria na kifua. Dokta: Sasa ushajua unaumwa nini hapa umefuata nini kwangu? Mgonjwa: Sasa si nimekuja kwa dokta. Dokta: Wanaojua kuwa wanaumwa kama wewe wanapitiliza maabara.

Wednesday, April 18, 2012

Pilau la bachela

Bachela mmoja aliekua akiishi kwa muda mrefu peke yake kwenye nyumba aliyopanga siku moja alitaka kupika pilau kwa mara ya kwanza. Sasa asijue nini kinachobadilisha rangi ya wali kuwa rangi ya brown, yeye akapika kama kawaida (wali) kisha wakati wa kula akavaa miwani yenye rangi ambayo ukiuangalia wali unauona kama pilau wakati anakula.

Nani alaumiwe?

Mwanamke: Nilikubali kuolewa na wewe haraka haraka kwasababu nlikua nna hasira siku ile. Mwanaume: Ooh! Mie sikuliona hilo nlikua kwenye dimbwi la mapenzi juu yako.

Full tank

Kijana mmoja alinunua gari, akaenda mpaka petrol station akajaza mafuta full tank. Alipotoka pale akaenda kwa fundi na kumuambia "fundi nna shida kidogo" fundi nae bila hiyana akajibu "niambie shida yako tu mkuu" Mwenye gari akanena "nahitaji unibandikie huu mshale wa mafuta kwa gundi ubaki huku huku juu kwenye full, ili mafuta yasiishe"

Nani kaliwa?

Nani imekula kwake hapa???? Phone call Girl:hellow Boy:sweet mambo vp? Girl: poa Boy:utakuwa free weekend?nilikuwa nataka uje nyumbani....kwangu. Girl: oh sorry,sintoweza kuja coz kuna harusi ya aunt yangu na siku ya pili kutakuwa na wageni nyumbani. Boy:kama ni hivyo sawa just nilikuwa nataka nikufanyie suprise nimekununulia i phone. Girl: oh usijali mpenzi wangu nitakuja,hata ukitaka nilale huko huko nitalala. Boy:vp kuhusu harusi? Girl:harusi ipi?nilikuwa nakutania sweety! Boy: poa na mimi nilikuwa nakutania hny!!

Hodi hodi

Usiku mkubwa mara ngo ngo ngo mlangoni: Wenye nyumba: Nani? Aliepo nje: Mimi. Wenye nyumba: Ndio wewe naani? Aliepo nje: Mimi mwizi nimeshindwa fungua mlango nimukuja kuiba tv.

Tuesday, April 17, 2012

Cheka kispoti

Wakulima wawili walikua wanatoka shamban na zana zao za kilimo wakapita katika uchochoro mmoja gafla waka sikia sauti, " simameni wote wawili wakasimama bana, weka jembe chini jamaa akaweka, weka kisu chini mmoja akasema sina kisu-ok kama huna kisu weka mavi-jamaa akatusua bana mdimba, ok we lamba mavi hapo fasta-jamaa wapili akalamba bana gafla wakasikia game sindo imeisha sasa tuchangen tena karata.

Monday, April 16, 2012

Mtoto alipotea

Mtoto wa miaka miwili na nusu alipotea alipotea na alipokua anaulizwa ili apewe msaada. Msamaria akamuuliza "enhe mama yako anaitwa nani?" Mtoto akajibu "anaitwa mama" Akaulizwa na "baba yako je anaitwa nani?" Mtoto akajibu "baba yeye anaitwa baba pia"

Sunday, April 15, 2012

Kilo zilipozidi...

Jamaa alienda kupima uzito akajikuta ana kilo nyingi kuliko akivyotegemea akashangazwa na kunena kama ifuatavyo "haiwezekani mi ndio nna kilo nyingi hivi? Embu tupime kimoja kimoja anza na mkono... Tufuate kichwa..."

Mwizi na chizi

Mwizi kaiba tv na kuanza kukimbia nayo, kumbe ile nyumba mlikuwa na chizi akaanza kumkimbiza yule mwizi. Kila mwizi akiongeza mbio chizi nae huyo, mwishowe mwizi akasalimu amri na kusimama, yule chizi akamsogelea na kumwambia.. Daah umesahau remote hii hapa mwizi kafleti.

Uuwii

MAMA:Mwanangu unamjua mkwawa? MTOTO:Cmjui MAMA: pumbav kuwa makin na masomo. MTOTO:Mama unamjua joyce MAMA:Hapana MTOTO:Mama kuwa makin na mumeo..

Saturday, April 14, 2012

Jino linauma

Mume akiumwa jino kweli kweli alifika kwa dentist na mkewe. Dokta akamuuliza "jino lipi linauma?" Mgonjwa akamgeukia mkewe na kumuambia "muonyeshe dokta jino linalouma"

Gongo no. 1

Njemba moja ilienda kwenye baa ya uswahilini akaagiza gongo ile namba moja. Wakati anakunywa mwenzake akamuambia "mzee jiangalie utalewa mpaka shati ukatufia hapa buuree, taratiiibu tafadhali" Njemba akajibu "kama nikifa nistue nilianzishe tifu hatakaa mtu hapa ma*#nin"}...".

Nani ajifiche

Majira ya saa moja usiku mtoto alimuona mama yake anarudi nyumbani akamuwahi na kumuambia "mama... mama usiende nyumbani kwanza baba yupo na mwanamke mwingine, ngoja nkamuulize nani ajifiche kati ya wewe au yeye?"

Live tv

Mtoto mmoja alikua anaangalia kipindi maalumu kilichokua kikirusha kwenye tv moja kwa moja toka eneo la tukio (kipindi cha mahojiano ya hoja). Baba aliporudi nyumbani akamuambia baba ake "baba mekuona kwenye tv, mekugusa hata husikii"

Friday, April 13, 2012

Swali la mwalimu na mwanafunzi

Mwalimu: Ema kulikua na ndege watano ukamtungua mmoja watabaki wangapi? Mwanafunzi: Wataruka wote hamna atakaebaki. Mwalimu: Watabaki wanne mmoja atakufa. Mwanafunzi: Mwalimu na mimi nna swali. Mwalimu: Uliza tu. Mwanafunzi: Kulikua na wanawake watatu wanakula koni wa kwanza anailamba, wa pili ana imega, wa tatu anainyonya yupi kati yao kaolewa? Mwalimu: Mhh! Wa tatu ndio kaolewa. Mwanafunzi: Umekosa alieolewa mwenye pete ya ndoa kidoleni.

Chemsha bongo

Baba akimuuliza chemsha bongo mwanae anaesoma shule ya chekechea "haya niambie kitu gani hakiwezi kuliwa wakati wa breakfast?" Mtoto akajibu "iyo mbona rahisi baba, si lunch na dinner"

Mume na mke kaazi...

Mwanamke: Mume wangu naomba hela nkanunua bra. Mwanaume: Mbona huna cha kuweka humo? Mwanamke: We mbona umevaa boxer wakati huna cha kukiifadhi humo?

Lipi bora

Mwanamke huki akimchapa mumewe "wee si ulisema umekoma kutembea na wanawake wa nje?" Mume: Mke wangu basi nisamehe sitarudia ntatembea na wanawake wa ndani tu.

Je umelewa?

Askari wa doria walimdaka mzee mmoja akiwa chakali kwa pombe huku akiendesha gari. Askari: Mzee unajua kwamba unaendesha ukiwa umelewa. Mzee: Hapana sijalewa afande kwani vipi (akiongea kilevi levi) Askari: Naomba leseni na kadi ya gari. Mzee: Ok, nishikie hii bia yangu nkutafutie hivo vitu.

Simu ya mke...

Mume wa mtu alikua yupo gesti hausi na nyumba ndogo yake. Punde simu ikaita mkewe akiwa anampigia "mume wangu nimekuja ofisini sijakukuta nimeambiwa umetoka upo wapi?" Mume nae bila hiyana "ohh my wife nimetoka nafanya kazi za nje leo"

Pombe hii?

Cha pombe mmoja akifokewa na mkewe "tatizo lako ukilewa huwa unaongea sana" njemba nayo haikukaa tu kimya akaamu kumjibu "mke wangu tatizo pombe nnazokunywa zinakua zisha-chacha ndio maana."

Wednesday, April 11, 2012

Hela

"Mzee umedondosha hela" kijana mmoja alimuambia. Mzee akapuuzia na kusema "okota tu hela yenyewe feki"

Tsunami

Taharifa ya Tsunami kutokea pwani ya maeneo ya Tanzania baada ya kupata tetesi kuwa haitatokea jamaa mmoja akanena "tsunami imeahirisha kuja Tanzania kisa umeme umekatika"

Tuesday, April 10, 2012

Mpenzi pombe

Jamaa akiiambia bia yake akiyokiinywa "wewe ndio mpz wngu! Huna wivu hata kdg hata mkiwa watatu meza moja. Tatizo lenu nikiondoka nashindwa kujua nani kati yenu kanilewesha sana"

Monday, April 9, 2012

Wapi ufunguo?

Mwanamke mmoja alipoteza ufunguo wa nyumba maeneo ya nyumbani. Sasa wakati anautafuta mumewe aliporudi akauliza na kuambiwa ufunguo umepotea. Mume akatoa simu na kumuambia mkewe "hebu nipe namba niu-beep"

Sunday, April 8, 2012

Kibweka - Pasaka

Mtoto alienda uganini siku ya pasaka, kabla ya mlo wa mchana akamuuliza mama yake kwa kumnong'oneza "eti mama na hapa watapika na toothpick?" Mama akajibu "mwanangu hizo huwa hazipikwi" Mtoto: Mbona nyumba ya jirani house girl huwa anazipika na zenyewe?"

Saturday, April 7, 2012

Jina la kijiji utata...

Mkoa wa Ruvuma una kijiji kinaitwa SENGE. Rais alienda ktk kampeni za Uchaguzi 2010. Mambo yakawa hivi: M/kiti na Katibu WA SENGE. Ndugu wananchi WA SENGE, Vijana, Wazee Wenzangu, na Watoto Wooote Wa SENGE. Mabibi Na Mabwana Wa SENGE "Asalam aleykum". "Wa Senge Oyyeeee!" Wa Senge Kimyaaaaa!.

Friday, April 6, 2012

Shetani bar

Wakiwa bar wanakunywa ghafla aliingia shetani, bar nzima kila mtu akakimbia mlevi mmoja akabaki. Shetani: We mbona hujakimbia huogopi? Mlevi: Niogope nini wakati nimemuoa dada yako miaka 20 iliyopita.

Mazungumzo - madereva

Dereva wa kwanza: Mie nlikuwashia taa nkikuambia kuwa acha mimi niende wa kwanza. Derava wa pili: Na mimi nilikuwashia wiper nikikuambia hapana, hapana.

Hamna kisichowezekana

Mtoto mmoja akimuambia baba yake jambo "hamna kinachoshindikana katika hii dunia" Baba yake akajibu "okay! Itoe dawa ya mswaki kwenye chupa yake kisha uirudishie humo humo.".

Faini chuoni

Mkuu anaehusika na wanafunzi wa chuo akiwafafanulia jambo wanafunzi wapya chuoni "ndugu zangu... Bweni la wasichana ni wasichana tu na wanaume ni wanaume tu." Akiendelea kuwaasa "atakae kamatwa mara ya kwanza atalipishwa faini ya elfu 20, mara ya pili elfu 60, mara ya tatu elfu 180." Mwanafunzi mmoja akanyoosha mkono kuashiria anaomba kuuliza swali, aliuliza hivi "je? Ni shilingi ngapi kwa muhula mzima?"

Swali na jibu

Mwalimu: Nini kinakufanya uone? Mwanafunzi: Ni Macho, pua na masikio! Mwalimu: Pua na Masikio? Kivipi? Mwanafunzi: Pua na Masikio hushikilia miwani yangu.

Mlevi na Mkewe bar

Mlevi mmoja alitoka na mkewe kwenda pata baridi moto katikati ya kinywaji njemba ikanena "I love you so much" mkewe akamuuliza "unaongea na mimi au bia?" Jamaa akatoa jibu lake "naongea na bia sio wewe."

Kutengeneza keki

Mtoto aliona mbwa wakifanya mapenzi akauliza mama yake "mama wale wanafanya nini?" Mama akajibu "wanatengeneza keki." Siku ingine akaona mbuzi akajibiwa ivo ivo. Siku moja mbele baada akaenda kwa mama yake "mama wewe na baba jana mlitengeneza keki sebuleni?" Mama "wewe umejuaje?" Mtoto akajibu "si nimekuta juisi juisi imedondokea kwenye kapeti"

Thursday, April 5, 2012

Mke muoga

Njemba moja: Mke wangu muoga na anaogopa maji. Rafiki yake: Unamaanisha nini? Njemba: Kila nirudipo nyumbani namkuta kwenye sinki la kuoga na houseboy bafuni.

Wednesday, April 4, 2012

Msg kwa wife

Meseji kwa mke wake "darling nipo bar napata mbili tatu, nitarudi ndani ya dk 50 zijazo, ukiona kimya soma tena hii meseji"

Besdei ya mke

Jamaa akimuuliza rafiki yake jambo "aisee nisaidie namna ya kuweza ikumbuka siku ya kuzaliwa mke wangu maana..." Rafiki nae akamjibu "mbona rahisi tu, isahau mara moja tu utapata..."

Mtoto miaka 18

Baba: Mwanangu sasa umetimiza miaka 18, njoo tuongee masuala ya mapenzi, kuachwa nk nk Mtoto wake wa kike akajibu: Sawa baba njoo nisikilize matatizo yako. Haya wapi panakukwaza nikusaidie kutatua?

Gym...

Kijana alienda GYM kufanya mazoezi akamuuliza mkufunzi wa mazoezi "nataka kumvutia mchumba wangu mashine/kifaa gani nitumie sana?" Mkufunzi akamjibu "mi nadhani mashine nzuri ya kumvutia mchumba ako ni ATM"

Mvuto nk

Mvulana: Navutiwa sana, sura nzuri, mvuto, kucha nzuri miguu ndio usiseme. Naweza pata namba ya simu? Msichana akijibu kwa aibu: Enhhe! Asante. Namba ya simu ni... Mvulana akamkatisha: Aahh sio wewe ni yule rafiki yako.

Changanya changanya

Deo akimsimulia mshkaji wake "unajua nini? Duniani hapa wanaume kuna mambo mawili huwa wayaelewi." Juma akajibu "kipi hicho wasichokielewa?" Deo "kumuelewa mwanamke kabla na baada ya ndoa."

Majina ya mapacha

Injinia mmoja wa program za kompyuta alipigiwa simu na kuambiwa mkewe kajifungua mapacha, hivyo wamekwama kuwatafutia majina... Jamaa akafikiria ndani ya muda mfupi akapata jina akawaita copy mwingine paste.

Nani kapoteza muda

Mwanafunzi wa darasa la pili: Yule mvulana anapoteza sana muda. Mwalimu: Wewe umejuaje unasema hivyo? Mwanafunzi: Nilikua nimekaa tuu namuangalia muda wote.

Saa ya bei chee

Jamaa walienda kununua saa! Mmoja akanunua saa ya laki 2 mwingine akanunuasaa ya elfu 30. Jamaa wa kwanza akamuuliza mwenzake "utofauti wa bei je zote zinaonyesha muda sawa?" Jamaa wa pili akajibu "hapana yako inaonyesha muda wako yangu inaonyesha muda wangu."

Njiwa amekufa

Baba akiwa matembezini jioni na mwanae: Mtoto: Baba huyu sio njiwa amekufa? Baba: Amekufa ndio, keshaenda kwa Mungu. Mtoto: Sasa mbona Mungu kamrudisha hapa tena?

Tuesday, April 3, 2012

Samaki baada ya...

Mtoto mmoja akiwa na baba yake restaurant: Mtoto: Najua kwa nini watu wakila samaki hawanyi maji... Baba: Kwa nini unasema hivyo mwanangu? Mtoto: Kwa sababu wanaogopa samaki wataanza kuogelea.

Kwenye harusi

Mtoto: Kwa nini Bw. Harusi huwa anakua upande wa kulia na Bi. Harusi upande wa kushoto? Mhasibu akajibu: Kwa mujibu wa Profit and Loss kwenye accounting, upande wa kulia kunakaa Income na upande wa kushoto expenses.

Kazi ya mwalimu

Mkufunzi walimuuliza mwanafunzi wake mmoja "wenzako woote wamekusanya kazi nliyotoa wewe ya kwako sijaiona kwanini?" Mwanafunzi akajibu "mbona nime-i-upload muda mrefu facebook nikaku-tag pia, hujaiona?"

Kibweka cha leo

Jamaa walikua wanapiga stori za hapa na pale maongezi yalikuwa hivi: Jamaa A: Unajua pale ilala unapata vitu karibu vyote vya mtumba! Jamaa B: Aacha utani bwana. Jamaa A: Ndio nakuambia hivyo sijui nguo, ma-jagi ya umeme, mabegi nk Jamaa B: Chakula je kipo cha mtumba?

Thursday, March 29, 2012

Kisanga cha mke

Mwanamke akihojiwa na mumewe. "mbona umechelewa kufika na ulisema ungefika saa 7mchana" mwanamke akajibu "ohh mingefika mapema ila boss alinituma nimsaidie kutafuta condom tulizotumia mkewe asijue kama nimetembea nae tulipokuwa semina." Mwanaume "mke wangu una... Nje ya ndoa?" Mwanamke "hapana tukizitumia kufundishia, mkewe alimtegeshea tu."

Wednesday, March 28, 2012

Bangi bwana

Jamaa alivuta bangi akavua nguo zote akajicheki kwenye kioo akajiona kavaa suti. Akaenda kwa wenzake akawauliza "nimevaa suti nimependeza enh?" Wenzake wakajibu "umependeza kweli ila tai umekosea kuivalia chini."

Tuesday, March 27, 2012

Kizee hospitali

Dokta akimpa majibu mzee wa miaka 70.
Dokta: Nina habari nzuri na mbaya.
Mzee: Oh nipe nzuri kwanza.
Dokta: Vipimo vinaonyesha una saratani, una miaka miwili tu ya kuishi.
Mzee: Oh! Mbona miaka mingi hivo ntakua nshakufa tayari. Nipe habari mbaya sasa...
Dokta: Ndani ya miezi mitatu utakua umesahau yote nliyokuambia.

Sharobaro kanisani

Mchungaji mmoja akiwapa mikono wa waumini kabla ya ibada, akamkuta kijana sharobaro akamuhoji "kijana karibu ujiunge na jeshi la Mungu"
Kijana: Tayari nimejiunga jeshi la Mungu.
Mchungaji: Mbona nakuonaga kanisani krismas na pasaka tu sasa?
Sharobaro akajibu "Ohh, mimi ni secret service."

Sunday, March 25, 2012

Mpita njia aliuliza

Jamaa alikua anapita njia akaona nyumba moja watu wengi mno. Akauliza "kunani hapa?" Mtu mmoja akamjibu "mjukuu kamuua bibi yake"
Mpita njia akanena "ohh! Atakua na marafiki wengi kweli bibi"
Jamaa akamjibu "hapana hawa watu wanataka inunua hii nyumba."

Huduma ya dharura

Dokta mmoja akimsimulia mwenzake "baasi bwana, alikuja jamaa na dharura ohh mke wangu yupo kwenye taxi anakaribia kujifungua"

Dokta akaenedelea simulia "nkachukua vifaa husika mbio mpaka kwenye taxi, kufika nkamfunua nguo kuanza kumvua chupi, kuja kuhamaki sio mhusika nipo kwenye taxi sio zilikuwepo kama nne hivi."

Mkeo kajifungua...

Jamaa akiwa hospitali anapewa majibu na daktari "hongera sana, mkeo kajifungua mapacha wawili"
Jamaa akanena "sasa mbona sikununua vitanda viwili, nepi mbili mbili sijui itakuwaje sasa?"

Friday, March 23, 2012

Maasai gesti hausi

Mmasai alinde nyumba ya kulala wageni ugenini. Chumbani alikuta neti imeshashushwa. Asubuhi wakamkuta kalala chini kumuuliza akajibu "meona masai shamba enh alale kwenye tego nategeshea mimi?"

Enzi zilee

Mume alimuambia mkewe "tukumbushane enzi za uchumba wetu." Mke akasema ok.
Mume "kesho tukutane kijiweni petu saa 1 usiku"
Mke akajibu "okay sweetie" mume akasubiriaa mtu hakuja kabisa.
Mume akamuuliza baadae "mbona hukuja sasa?"
Mke: Mama alinikataza nisije.

Thursday, March 22, 2012

Baba na mwana

Baba: Jumaa...
Mtoto: Eeh baba.
Baba: Niletee kiberiti.
Mtoto: Cha sigara au bangi?
Baba: Shika adabu yako, cha sigara.
Mtoto: Cha baridi cha moto?
Baba: We leta kiberiti chochote.

Hausi geli mpya

Mzee alirudi nyumbani akakuta mkewe kaleta dada wa kazi za ndani (beki 3).
Mume: Mke wangu huyu nani?
Mke: Ni dada wa kazi za ndani.
Mume: Huyu nilimuona facebook akimsifia hausiboi wa jirani yetu huyu... Hapa kapajuaje?
Mke: Mimi nilimu-add kama rafiki humo humo facebook.

Wednesday, March 21, 2012

Bangi mbaya

Mzee mmoja alikataza vijana wasivute bangi pembeni ya nyumba yake. Vijana wakavuta wakavua mashati na kuanza kuisukuma nyumba.
Kibaka akapitia shati zao. Mmoja akageuka na kusema "tujitahidi kusukuma tumefika mbali hata mashati hayaonekani tena."

Tuesday, March 20, 2012

Habari ya msiba

Jamaa mmoja mila zao ni kuchoma maiti. Alitumiwa ujumbe kuwa mama yake mzazi amekufa na kumuuliza kama wauchome moto mwili au wamsubiri mpaka afike.
Jamaa akajibu ujumbe "uchomeni tu moto, halafu na majivu pia msisahau kuyachoma naja siku mbili hizi."

Mpaka kwa dokta

Jamaa alienda mpaka kwa daktari na kumuelezea "dokta ona nna karoti kwenye pua, na kipande cha pera kwenye sikio, ntakua na tatizo gani?"
Dokta akajibu "hauli inavyotakiwa"

Kasichana

Mtoto mmoja wa kike miaka 12 akimsimulia mama aliporudi toka kazini. "mama mi nadhani yule hausi boi wetu atakua shoga tu."
Mama kwa mshangao akauliza "hee kwa nini wasema hivyo?"
Mtoto akajibu "nimemshika naniliu weee hata haisimami."

Ajali hii mhh!

Trafic polisi: Unatambua kua umeua watu 10 kwenye ajali hii?
Dereva: Breki ziligoma, kushoto kuna mtu mmoja kulia wawili ungekua wewe ungeelekezea wapi gari?
Trafic polisi: Ningeelekea upanda wa mtu mmoja.
Dereva: Unaona, ndio nlifanya ivo ivo ila yeye alikua anakimbilia kwenye watu wengi mi nkamfuata huko huko.

Kosa lingine

Mwanafunzi: Mwalimu nimekosa sitorudia ten a, nipo chini ya miguu yako.
Mwalimu: Yaani umeongeza kosa huko chini ya miguu yangu unachungulia nini?

Mlokole na mlevi

Mlokole alipanda daladala akakaa pembeni mwa mlevi. Maongezi yao yakawa hivi:
Mlokole: Unajua wewe unaenda motoni?
Mlevi: Oh! Kumbe, wee konda nishushe bwana mi nlidhani unaenda mjini.

Saturday, March 17, 2012

Mwizi wa wallet

Mlevi mmoja aliibiwa wallet kwenye bus, "jamani kuna mtu kaniibia wallet yangu, naomba airudishe. Isije yakatokea yaliotokea mwaka jana."

Baada ya muda mwizi akairudisha, jamaa akapekua kila kitu kipo poa. Mwanamke mmoja akamuuliza "kwani mwaka jana kilitokea nini?"
Mlevi akajibu "niliibiwa wallet hivi hivi ikabidi nitembee mpaka nyumbani."

Friday, March 16, 2012

Pombe bwana

Walevi wawili walikua chakali wamelewa. Wakawa wanabishana "ule mwezi ni wa kijani" mwingine anasema mwekundu.
Mbele wakamkuta mtu wakamuuliza "eti, samahani ule mwezi ni kijani au mwekundu?"
Alieuliza aliangalia juu kisha akanena "upi sasa wa kushoto au kulia?"

Boss na masikio

Kwenye usahili boss asiekua sikio hata moja alikua anahoji ili apate mfanyakazi mwenye sifa.
Boss: Hii kazi inahitaji ufanisi, ni kwanza nini umekiona toka kwangu?
Mtu wa kwanza: Huna masikio kabisa.
Boss kwa hasira "toka nje"

Wa pili ivo ivo akatotelewa, mlangoni akamuonya mtu wa tatu. Alipoingia wa tatu nae akajibu "haujavaa miwani leo"
Boss: Umejuaje?
Mtu wa tatu: Kwa sababu huna masikio.

Thursday, March 15, 2012

Vituko vya dereva

Jamaa mmoja alidakwa na polisi akapaki pembeni. Gari ina vioo vyeusi aliekua anaendesha ni mmoja, akahamia kiti cha abiria mbele. Polisi alipofika akauliza "dereva wa hii gari yupo wapi?"
Jamaa akajibu "alikuwepo hapa sekunde chache zilizopita."

Spidi kali

Njemba moja ilisimamishwa na trafic polisi:
Polisi: Nimekusimamisha unakimbiza sana gari, spidi 90 sehemu ya kupita spidi 50.
Njemba: Afande embu angalia kwanza gari si hii hapa imesimama hiyo spidi unayosema mbona siioni?

Kutoka gesti hausi

Mke: Mume wangu nimepata news zako umetoka gesti na leo.
Mume: Mke wangu si kweli kabisa kama huamini kaangalie kitabu cha wageni ameandika mwanamke mie nlijua utaenda angalia tu.

Mwizi wa dhahabu

Mwizi mmoja alidakwa akikwapua moja ya saa kwenye duka la dhahabu, alipodakwa akasema "mkuu najua hutopenda vurugu, tufanye hivi niinunue hii saa yaishe hapa hapa."
Mwenye duka akakubali alipoanza kuandikia risiti bei ya hiyo saa kibaka alipoiona bei akanena "enh samahani naona bei yake kubwa kidogo hamna ingine ya bei rahisi?"

Gari zavutana

Mtoto mmoja alikua amegeuka akaona gari zinavutana akamuuliza baba ake "baba zile gari zinavutana?" Baba akajibu "ndio mwanangu"
Mtoto akanena tena "sasa ile inayovutwa si imu-over_take anaemvuta?"

Toka usingizini

Jamaa alikua ametoka kulala na sura yake ya usingizi usingizi... "oya vipi umetoka kulala nini?" Jamaa akajibu "ndio" alueuliza akanena tena "ndio maana unanukia ndoto ndoto bado."

Wednesday, March 14, 2012

Kitu cha dokta

Jamaa aliulizwa "mbona una picha kubwa ya daktari unataka kuwa dokta baadae nini?"
Jamaa akajibu "nimeambiwa maumivu yakizidi muone daktari."

Darasa la dini

Kwenye kipindi cha dini darasa liliulizwa "nani anataka enda mbinguni?" Darasa zima likanyoosha. Mmoja hakunyoosha, akaulizwa kulikoni wewe hujanyoosha kidole akajibu "mama kaniambia nikitoka shule nsipitie popote ninyooshe nyumbani."

Pochi mpya

Jamaa mmoja alimnunulia mkewe pochi mpya. Alipofika nyumbani kumpa mkewe nae akajibu "hee hii pochi si ndio alitaka ninunulia Rashid nkamuambia hainitoshi."

Kucha za vidoleni

Jamaa mmoja alikua anapenda sana kuweka/kula/kukata kucha za vidoleni. Siku moja akiwa bize na kucha jamaa ake baada ya mida fulani akamkaribisha chakula, mkata kucha akajibu "dah aisee nshashiba kucha hapa nipe maji tu nishushie."

Kitu cha kanisani

Jamaa akiongea na mwenzake "jana kuna mshkaji aliwasha fegi (sigara) kanisani, nlikua naogopa na kutetemeka kidogo nidondoshe bia yangu mkononi."

Majambazi kichakani

Majambazi watatu walijificha kichakani wakiwa wamelala chini. Polisi wakati wanawatafuta wakamkanyaga mmoja:
Jambazi wa kwanza "oyaa vipi unanikanyaga" akadakwa.
Jambazi wa pili "wee siukae kimya!" Nae akadakwa.
Jambazi wa tatu "bora mie nimekaa kimya" nae akadakwa.

Tuesday, March 13, 2012

Siti zimejaa

Kondakta: Ma mdogo pakia twende gari nyeupe sana.
Abiria: Imejaa sana siwezi kupata siti.
Dereva akadakia "ma mdogo we pakia tu mimi nashuka kituo kinachofuata utakaa changu."

Kipigo

Jamaa mmoja aliambulia kipigo na mume wa mtu mmoja hivi baada ya kuulizwa "wewe umejuaje size ya sidiria ya mke wangu?" Jamaa aliepata kipigo ndio akajibu "mzee mie muuza sidiria tu huwa namleteaga mara kwa mara."

Monday, March 12, 2012

Mimba zingine

Chris: Mke wangu kaniambia ana mimba ina miezi mitatu sasa.
Ben: Ohh hilo jambo la heri sana hongera.
Chris: Lakini nilikua sipo mjini kwa muda wa miezi sita!

Fumanizi

Jamaa alikua na mke wa mtu ghafla mwenye nyumba akarudi. Pa kujificha ni uvunguni...
Wakati jamaa amekaa kitandani kikavunjika alie uvunguni akapayuka "yalaah unaniumiza."

Saturday, March 10, 2012

Ulevi barabarani

Trafiki polisi alimkamata jamaa akilewa huku ana endesha gari.
Trafiki: Tafadhali nitolee leseni yako na kadi ya gari.
Dereva akiongea kilevi: Ohh! Nishikie hii bia yangu kwanza ni nikutafutie hivyo vitu...

Mahesabu

Mwalimu: Haya 7 x 6 jibu ni?
Mwanafunzi: Jibu ni 42.
Mwalimu: Safi, je 6 x 7 je?
Mwanafunzi: Jibu ni 24.

Friday, March 9, 2012

Baada ya uroda

Msichana alimuhoji jamaa baada ya kumaliza uroda.
Msichana: Mbona gitaa lako dogo sana?
Mvulana: Sikujua kama ntantumbuiza uwanja wa,taifa.

Visa vingine bwana

Jamaa mpita njia alijiangusha nje ya geti la kiwanda cha bia. Walinzi wakati wakimsaidia "leteni maji ya kunywa haraka..." Alieanguka akanena "ningetaka maji si ningeenda anguka dawasco"

Mwalimu na mwanafunzi

Mwalimu: Kati ya hela ma akili utachagua nini?
Mwanafunzi: Mi ntachagua hela.
Mwalimu: Mimi ningechagua akili.
Mwanafunzi: Kila mtu amechagua asichokua nacho.

Thursday, March 8, 2012

Yai la kuchemsha

Mzee "kanichemshie yai moja na moja ulikaange"
Baada ya dakika 15 aliletewa mzee akaanza kuwaka "ahaa! Umekosea hili ulilochemsha ndio ungelikaanga"

Askari na dereva

Jamaa alisimamishwa na polisi "unajua kwa nini nimekusimamisha?"
Dereva "ndio afande leo sijatoka na mkeo nipo na mwanao ntamrudisha baadae"

Mwandiko

Mbona unaandika taratibu unatutafunia muda wetu na hiyo kalamu yetu. Mzee akajibu "namuandikia barua mjukuu wangu wa miaka 6, hawezi kusoma haraka haraka."

Saturday, March 3, 2012

Vibaka mzigoni

Vibaka walienda kimya kimya usiku kuiba nyumba moja, punde mmoja wao akapiga chafya. Mwenye nyumba kwa vile alishawaona akanena "uwe unaziba pua ukipiga chafya"

Naumwa nini

Mtoto: Baba ndio unaumwa, lakini mbona unawaambia watu una ukimwi na sio saratani?
Baba: Mwanangu ili nikifa hamna atakaemgusa mama yako.

Mimba ya...

Msichana: James mpenzi nna mimba yako dia.
Mvulana: Una uhakika kabisa ni ya kwangu?
Msichana: Kwa nini kila ninaemuambia anasema hivyo?

Friday, March 2, 2012

Somo la hisabati

Mwalimu: Wewe mimi nafundisha hisabati wewe unapaka mate kichwani. Ndio nini?
Mwanafunzi: Nilimsikia mama akimuambia baba "kama haiingii paka mate"

Amechelewa shule

Mwalimu: Wewe mbona umechelewa shule?
Mtoto: Baba na mama walikua wanapigana.
Mwalimu: Sasa wanahusiana nini na kuchelewa kwako?
Mtoto: Mama alikua anatumia kiatu changu kupigana, baba ndio anaeniletaga na gari shule.

Wajua wapi ma wapi?

Kijana: Mzee Iddi ulisema wewe umesafiri sana enhe?
Mzee Iddi: Ndio nlikua baharia nimezunguka nchi nyingi sana.
Kijana: Basi Geography utakua unaijua vyema sana.
Mzee Iddi: Tena huko Jographia nilipita mara nyingi sana.

Wednesday, February 29, 2012

Gari mupya

Jamaa alinunua benz automatic gia. Akaendesha vizuri lakini usiku uligoma kabisa kwenda. Kuita fundi akawa anaelezea baada ya kuhojiwa ni vipi imemgomea kwenda akajibu "ni hivi... Mchana nikiweka D inaenda vizuri, ila usiku haiendi nkiweka N. Au N sio for "Night and D for Day?"

Jina kwenye simu

Msichana mmoja alichukua simu ya mpenzi wake akaandika namba yake ili ajipigie aone jamaa amesave jina gani. Alipofanikiwa akakuta imeandikwa "fundi tiles"

Darasa la kimombo

Mwalimu aliuliza: Do you undestand the importance of period?
Mwanafunzi mmoja akajibu mdogo kwa umri "yes i know, siku moja my sister alisema amekosa period mama akazimia na baba akachanganyikiwa."

Kipi bora?

Mwalimu: Kwa nini wanasema mapenzi bora kuliko vita?
Mwanafunzi mmoja akajibu "kwa sababu condom ni bei rahisi kuliko bunduki."

Kibaka

Raia walifukuza mwizi akakimbilia makaburini usiku. Punde akavua nguo zote na kuelekea walipo raia wenye hasira. "tunamtafuta mtu kapita hapa na kifurushi" jamaa akajibu "sijamuona, mi mwenyewe mgeni hapa nimezikwa jana ngoja niwaulize wenyeji wangu"
Raia hamna aliebaki baada ya hapo.

Posa

Jamaa alienda kutoa posa akaambiwa "mtoto yupo shule bado anasoma" njemba nayo ikajibu "sawa ntakuja wakati wapo mapumziko "break time"

Tuesday, February 28, 2012

Askari mnarani

Jamaa mmoja alipofika mjini pale posta mpya kwenye askari (mnara) akanena, "hee kipindi kile nlipokuja dar huyu askari alikua bado mdoogo, leo amekua hivi."

Wednesday, February 22, 2012

Mawazo ya mtoto

Mtoto: Baba na mama nimemleta fundi yupo hapo nje anawaaubiri"
Baba akadakia "mimi nimekuagiza au mama yako?"
Mtoto: Hamna alieagiza, mimi nimemleta awatengenezee kitanda chenu kina kelele sana usiku kulala shida."

Mtoto mzuri

Mtoto alimuona dada mja mzito.
Mtoto: Humo tumboni una nini?
Dada: Kuna mtoto.
Mtoto: Mzuri enh kama wewe?
Dada: Ndio.
Mtoto: Sasa mbona umem-meza?

Disco

Marafiki wawili walienda disco maongezi yao yalikua hivi.
Mshkaji 1: Ee we vipi tangu umekuja hauchezi hata nyimbo moja vipi?
Mshkaji 2: Kuna nyimbo naipenda sana halafu haichezwi mpaka muda huu...
Mshkaji 1: Mwimbo gani huo?
Mshkaji 2: Si wimbo wa taifa.

Ugeni wa mambo

Mwananchi mmoja alietoka nyumbani kwake na kuelekea duka la dawa. Alipofika yakawa hivi "dada samahani nimerudi tena, hivi ulisema zile plasta nimeze mara ngapi kwa siku? Nimepitiwa kidogo."

Simu zina mambo

Mvulana: Mambo? Upo wapi mpenzi?
Msichana: Nipo chumbani nasikiliza mziki. Wewe je?
Mvulana: Mimi nipo nyuma yako humu club, geuka utaniona.

Kimombo.com

Mtoto wa miaka 11 alikua ameketi na baba ake. Kwa mbali akamuona msichana wake anakuja. Dingi hataki mwanae kujihusisha na mapenzi mapema, kuua soo msichana alipofika akaamua kumuongelesha kimombo.

Mvulana: Ohh umekuja fuata kile kitabu "speak english my father doesn't speak?"
Msichana: Yah na kile cha "where should i wait for u"
Mvulana: Hicho hakipo labda kile "wait for me under coconut tree"
Msichana: Sawa kama kipo cha "i give you 5min" njoo nacho kesho shule.

Baba akajua mwanangu anapenda shule sana.

Mwendo wa ringtone

Jamaa mmoja aliweka ringtone kwenye simu yake mlio wa kifaranga. Siku simu ikaita si kunguru akaikwapua. Jamaa akabaki ananena "oyaa rudisha simu yangu"

Tuesday, February 21, 2012

Mwindaji na mchunaji

Mwindaji alishuka na kwenda kuwinda, ghafla akawa anarudi mbio "fungua fungua mlango simba ananifukuza" kabla hajaingia akaanguka hatimae simba akaingia garini jamaa yupo nje. Akainuka na kumuambia mchunaji "anza kumchuna huyo naenda kumleta mwingine."

Kengele

Mtoto mmoja alikua akijaribu bonyeza kengele kwa vile mfupi hakuifikia, kaka,mpita njia akaenda na kumsaidia kubonyeza. Kisha akamuuliza "nini kingine nkusaidie mtoto?"
Mtoto akajibu "tukimbie tukajifiche mwenyewe asituone"

Mzigo wetu

Mke: Mbona upo ivo umefukuzwa kazi?
Mume: Hapana sio hilo.
Mke: Sasa nini? Shida yako yetu sote mume wangu.
Mume: Oh afadhali... Sekretari wangu ana mimba yangu.

Vizee viwili

Babu: Mke wangu hujisikii wivu mimi kuvizia visichana?
Bibi: Hata mbwa wanakimbizaga magari na kuendesha hawajui.

Peteee!

Mke kwenye simu kwa ukali: Uko wapi mpaka muda huu?
Mume: Mke wangu unakumbuka lile duka la pete ile tuliyoiona nkakuambia naipenda sana na sikuwa na pesa wakati ule?

Mke akajibu huku akiona haya kidogo "ndio mume wangu naikumbuka sana."
Mume: Basi nipo bar jirani na hilo duka.

Monday, February 20, 2012

Kwenye tuta

Jamaa walikua kwenye gari, kwenye tuta likagusa. Ulipofika tuta la pili halikugusa mmoja kati yao akanena "nimenyanyua miguu ndio maana halijagusa asa ivi"

Saturday, February 18, 2012

Mtoto wa nje

Mwanamke mmoja alijifungua mtoto, si mume wake wa ndoa. Mume alikubaliana na hali halisi. Akapaka sumu kwenye chuchu ili mtoto afe, siku iliyofuata alipigiwa simu arudi nyumbani kuna msiba.

Akiwa njiani huku akitabasamu kutimia kwa lengo lake alipofika nyumbani akapewa taarifa kuwa, aliefariki ni "house boy" na si mtoto.

Kusali kabla...

Mwalimu wa hesabu na mwanafunzi wa darasa la tatu.
Mwalimu: Fredy mbona una sali saa hizi?
Mwanafunzi: Mama aliniambia niwe nasali kabla ya kulala.

Wednesday, February 15, 2012

Wivu

Mwanamke mmoja alikua akiangalia tv, alikua akiangalia mahojiano ya mchumba wake akihojiwa na mtangazaji mzuri wa kike. Wakati wanamaliza kipindi mtangazaji akamkumbatia mchumba wa huyu dada.

Wivu wa mapenzi dada akainuka kwenda kuchukua mwiko aje kumpiga mtangazaji. Aliporudi akakuta kipindi kimeisha na kuna matangazo, akanena "bahati yako umekimbia ungenitambua leo..."

Majibu...

Nesi alitoka leba na kumpa majibu mume wa mama aliepo leba.
Nesi: Hongera sana mkeo kajifungua watoto watatu wenye afya nzuri.
Mume: Nilijua tu ona sasa hao watoto wa ziada wawili ni wa nani?

Masikio vipi?

Jamaa alienda kazini masikio yote yakiwa yamefungwa plasta.
Boss: Vipi masikio mbona ivo?
Jamaa: Nlikua napiga pasi then simu ikaita, nkapokea kumbe ilikuwa pasi.
Boss: Na hilo sikio la pili je?
Jamaa: Nilikua nataka mpigia dokta, pasi tena ikanichoma.

Sunday, February 12, 2012

Msiba wa tembo

"Mbona unalia?" Mtoto aliulizwa.
Akajibu "tembo amekufa"
"alikua mnyama wako?"
Mtoto akajibu "hapana mimi ndio wa kumchimbia kaburi"

Mchumba wa...

Mtoto: Baba kesho birthday ya mchumba wangu sijui zawadi ganibya kumpa?
Baba: Yupoje kwani?
Mtoto: Mzuri, Mrefu ana Hips na nywele ndefu.
Baba: Ohh! Mpatie namba yangu.

Friday, February 10, 2012

55

Mwalimu aliwaambia wanafunzi wa chekechea waandike namba 55.
Mwanafunzi mmoja akaandika 5 akawa kaganda tu.
Mwalimu akamuuliza mbona huandiki ingine?
Mwanafunzi akajibu "mwalimu sijui niandike upande gani, kwa mbele au kwa nyuma?"

Mgahawani

Mteja: Nimeona kabisa kidole gumba chako kwenye supu wakati unaniletea...
Mhudumu: Ndio... Supu haikua ya moto sijaungua.

Kifungua kinywa

Jamaa: Kwa kukuangalia usoni najua kabisa umekula mkate na mayai.
Rafiki: Hehe hiyo ilikua jana leo kiporo na uji.

Hoja hii

Mtoto: Hawa wanakimbia nini?
Mzee: Wanashindania kombe.
Mtoto: Sijaelewa babu.
Mzee: Yaani mshindi "mmoja" ndio atapata kikombe.
Mtoto: Sasa hawa wengine wanakimbia nini?

Bibi kizee kwenye basi...

Bibi kizee kwenye daladala alikaa karibu kabisa na driver. Dereva akawa anaendesha mkono mmoja nje dirishani, kwa vile hapendi akamgusa bega na kumnong'oneza "endesha na mikono yote, mvua ikinyesha nje ntakuambia"

Chura kwenye...

Mteja: Mhudumuuu njoo kuna chura kwenye supu yangu.
Mhudumu: Ohh pole kaka, inzi wapo likizo.

Boss wako

Jamaa aliulizwa amzungumzie boss wake akawa anajibu "boss wangu mhh! Yupo yupo tu hajulikani hata kivuli chake kimekataa kumfuata"

Chimba dawa

Muhindi alipigwa faini ya 1,000Tsh kwa kukojoa kichochoroni. Yeye akalipa 1,500Tsh. Akaulizwa mbona kalipa zaidi akajibu "wakati makojoa iko jamba kodogo"

Thursday, February 9, 2012

Kitu msikitini

Jamaa aliingia na panga msikitini "nani muislamu hapa?" Msikitini kiimyaa. Akamchukua mmoja akatoka nae nje akamchinjie kuku. Akarudi msikitini na panga likiwa na damu akauliza tena "nani muislamu humu?" Waumini wakamuonyeshea imamu, imamu nae akajitetea "jamani mie kusalisha siku mbili tu ndio nshakua muislamu?" Jamaa mwenye panga akajibu "nataka ukanisaidie kumchuna ngozi mbuzi wangu"

Siku ya kwanza

Mama: Enhe mwanangu, ume-enjoy siku yako ya kwanza shuleni?
Mtoto: Siku ya kwanza? Ina maana kesho naenda tena?

Samaki wa kufuga

Samaki wawili wa kufungwa wakiwa kwenye chombo cha kioo:
Samaki wa kwanza: Unaamini Mungu yupo?
Samaki wa pili: Ndio, unadhani nani anaebadilisha maji yakichafuka?

Bidhaa gani?

Mwalimu: Ni bidhaa gani tunaipata kutoka mtibwa?
Mwanafunzi: Hata sijui mwalimu.
Mwalimu: Wewe ina maana hamnunui sukari?
Mwanafunzi: Hatununui tunaombaga kwa jirani

Mke anakufa

Mke akiwa hoi/mahututi hospitali "mume wangu kuna jambo nikuambie kabla sijafa niwe na amani niendako"

Mume: Usihangaike kila kitu kipo sawa mke wangu...
Mke: Mume wangu nililala na rafiki yako, jirani yako na boss wako... Hivyo naomba unisamehe.
Mume: Usijali najua yote hayo ndio maana nimekuwekea sumu.

Swali darasani

Mwalimu aliuliza swali darasani "kwa nini sokwe ana pua kubwa?" Mwanafunzi mmoja akajitokeza na kutoa jibu "mwalimu, kwa sababu ana vidole vikubwa."

Konda na Sharobaro

Kondakta: Oyaa ingia ukamate bomba tusepe.
Sharobaro: Siwezi men hamna siti naona full ndani.
Kondakta: Huna lolote si ungekuja na kiti chako sasa.

Konda na abiria

Kondakta: Dada ingia kuna kiti pale nyuma.
Dada: Siwezi kukaa siti za nyuma.
Kondakta: We si mwendaji kwani za nyuma zipo nje ya gari...

Tuesday, February 7, 2012

Nyimbo gani

Mtoto mmoja aliulizwa swali "ni mziki gani anaupenda sana kuusikiliza?"
Mtoto akajibu "kengele ya saa nane ya kwenda nyumbani"

Monday, February 6, 2012

Mtoto keshaanza

Mama mmoja alianza pata wasi wasi kua mwanae wa kike atakua ameanza mahusiano, kwa kuogopa asije akapata mimba akamuita na kumpa somo nk nk.

Mwisho wa siku akampa condom. Mtoto akacheka sana kisha akajibu "mama una wasi wasi ntapata mimba? Hapana mimi natembea na Lisa."

Sunday, February 5, 2012

Kupiga pasi

Jamaa mmoja aliambiwa akapige pasi shati:
Jamaa: Nisaidie kulinyoosha kwa pasi hilo shati hapo na pasi hiyo hapo ya mkaa.
Alieambiwa akajibu "hii pasi yako haipigi shoti, naogopakurushwa"

Saturday, February 4, 2012

Safari ya boti

Mzee mmoja alikua kwenye boti akielekea visiwani, bahati mbaya upepo ukavuma na msuli aliovaa ukapeperuka. Mzee muda wote huo aliwahi kikofia chake (baraka-sheikh).

Kumuuliza matokeo ya kuzuia kofia na kubaki uchi yeye akajibu "hizo nywele mzionazo na hiyo naniliu vyote vya zamanj, hii kofia bado mpyaa."

Kwa mchungaji

Mchungaji akitoa maombi... "waumini mkirudi nyumbani muinue matatizo yenu juu na Mungu atayatatua.

Muumini mmoja aliporudi nyumbani yeye akamnyanyua juu mkewe.

Friday, February 3, 2012

Maembe yakigawana

Jamaa wawili walinunua maembe sasa wakaamua wakayahifadhi kwenye chumba cha kuhifadhi maiti. Baadae mlinzi akasikia watu wakiongea "...we chukua hii nipe hiyo..." Mlinzi,akakimbia na kukutana na dokta akamuambia huku akihema "dokta... Hahh hahh... Mochuari maiti zinachukuliwa na shetani wanagawana"

Utaniii

Jamaa mmoja mrefu alilala kitandani, kwa vile kitanda ni kidogo miguu ilizidi nje. Rafiki zake walipokuja wakamfunga kitambaa chekundu wakimaanisha mzigo umezidi bodi kama kwenye gari ya mizigo.

Thursday, February 2, 2012

Kupanda na...

Jamaa mmoja alitoka kijijini akaja mjini Dar es Salaam. Siku moja wakati ameenda kupanda daladala kabla hajapanda akamuuliza konda "kondakta samahani naruhusiwa kupanda na viatu?"

Wednesday, February 1, 2012

Amemeza...

Jamaa: Mtoto wangu si alimeza condom yangu jana bwana...
Rafiki: Aah sasa ulipata ingine au ilikua iyo iyo tu?

Mtoto alichokiona

Mtoto mmoja akimsimulia mama ake, "mama leo nimemuona mwanamke kavaa sketi fupi huyoo kaama yule anaekuwaga na baba ukienda kazini"

Dereva alipoambiwa

Dereva mmoja alishuka kwenye gari haraka haraka baada ya kusimamishwa na mtu haraka haraka na kuhoji "vipi mbona umenisimamisha ghafla hivi kuna nini?"
Jamaa aliemshusha akanena "matairi yanazunguka huku nje ndio nkikuambia."

Saturday, January 28, 2012

Bafuni kwetu

Mtoto mmoja alimuuliza baba yake swali "baba kwanini kila mtu hapa nyumbani akiingia bafuni tu anaanza kuimba?"
Baba akajibu "sababu ni kitasa cha mlango kimekufa mwanangu"

Tuesday, January 24, 2012

Mipango ya wezi

Wezi waluenda kuiba duka la sonara, wakagawana na kuondoka. Baada ya muda polisi wakaja na kumkuta mmoja wapo wakamuuliza nae akajibu, "tumepanga na wenzangu tugawane mie nimechukua duka"

Friday, January 20, 2012

Chai

Mzee mwenye nyumba alipopelekewa chai:
Mzee "hii chai mie nimesema nataka ya maziwa si rangi!"
Dada "maziwa yameisha tangu jana"
Mzee "kwani mama Issa si ananyonyesha mwambieni anikamulie japo robo kikombe..."

Mtoko...

Wachawai wakiwa katika maongezi yao:
Mchawi 1: Leo si ijumaa hatutoki?
Mchawi 2: Dah! Bahati mbaya ungo wangu umeisha inshuarensi so nikipata ajali imekula kwangu.
Mchawi 1: Basi kamuazime mbuggu wa kwake.
Mchawi 2: Wa kwake juzi tu umepigwa pasi ivo upo gereji.

Ndoto zingine...

Ally: Jana usiku meota nipo Japan.
Saidi: Mimi nimeota nina party nyumbani.
Ally: Sa mbona hukunialika?
Saidi: Mi nlijua bado upo Japan.

Mayai ya kuku

Muuza chips alivunja mayai takribani matatu yote matupu kilichofuata akanena "inaelekea hadi kuku wanatumia condom

Thursday, January 19, 2012

Imekuwaje tena?

Mwanamke mmoja alimnasa kibao cha uhakika mwanaume mmoja, jamaa wa pembeni akasogea kuuliza "vipi kaka mbona makofi hadharani?"
Jamaa aliepigwa akajibu "si fulana yake imeandikwa maeneo ya kifuani "gusa taratibu" ndio yaliyonisibu baada ya kugusa"

Gazeti

Dada mmoja aliketi kwenye kiti cha bustani, alikua,amekalia gazeti asichafue sketi yake nyeupe. Akatokea kijana mmoja akamuuliza "unasoma gazeti hapo?"

Dada kuepusha maongezi yasiendelee akajibu "ndio" kisha akainuka na kufunua ukurasa unaofuata kisha akaendelea kukalia.

Changudoa

Jamaa alizidiwa ikabidi akaopoe malaya wanaojiuza.
Jamaa: Enhe biashara inakuwaje?
Malaya: Short time elfu 15, mpaka asubuhi elfu 30.
Jamaa: Ok hamna shida si mnatoa na risiti lakini?
Malaya: We bwege nini umesikia hapa kibaruani kwako.
Jamaa: Sasa mie ntajuaje kama nakatwa VAT kihalali?

Monday, January 16, 2012

Kitu cha mbagala

Wakati watu wanagombania kupanda kwenye basi la mbagala kama kawaida yao, bibi mmoja alipanda bila shida akapata siti. Baada ya muda konda akamuuliza "bibi unalia nini sasa?"
Bibi akajibu "miaka yote 25 nliyoishi Mbagala sijawahi pata siti" konda akanena baada "bibi pisha siti hapo umekaa ya dereva."

Chenchede

Kidume: Haloo, naongea na Rehema?
Rehema: Ndio mie.
Kidume: Rehema yule nliekua nae tukalewa sana?
Rehema: Ndio mie, ukanisifia nna kiuno kitamu.
Kidume: Ohh! Safi za tangu siku ile?
Rehema: Nzuri tu, na nna mimba yako.
Kidume: Enh! Wrong namba.

Mke na Mume

Mume alipanda kitandani akiwa tayari tayari kula tunda la ndoa na mkewe.
Mke alipokuja akanena "mie naumwa kichwa leo siwezi."
Mume akaenda jikoni kurudi naniliu yake ilikua kama ina unga unga mke akauliza "nini iyo?"
Mume akajibu "nimeipakaza asprini na panadol haya njoo."

Kwenye harusi

Mwalimu: Kwanini hujaja shule jana.
Mtoto: Nilienda kwenye harusi ya anko wangu.
Mwalimu: Amemuoa nani?
Mtoto: Amemuoa mke wake.

Malavi davi

Jamaa aliandika sms kwa mchuchu wake ifuatavyo.

Kama unatabasamu ntumie tabasamu lako.
Kama umelala ntumie ndoto uiotayo.
Kama unalia nitumie machozi yako.

Mwanadada akajibu ifuatavyo:
"nipo chooni je nitume chochote"

Sunday, January 15, 2012

Vichaa wakiwa beach

Vichaa kadhaa walipelekwa beach kupunga upepo, mmoja akawa kajitenga na wenzake. Nesi akamuuliza "mbona umejitenga na wenzako vipi?"
Kichaa akajibu "najiuliza hii bahari ingakua supu ningekula chapati ngapi?"

Talaka je?

Mwanaume: Kwa nini sasa usumuombe talaka mumeo kama humpendi na kumchukia?
Mwanamke: Yaani namchukia sana kiasi kwamba akinipa talaka ntampa wakati wa kuwa na furaha sana ndio sitaki.

Mie naumwa

Mfanyakazi alimtumia sms/msg boss wake...
Mf'kaz: Boss leo siwezi kuja kazini naumwa.
Boss: Mi nikiumwa nambusu mke wangu kisha napona na nakuja kazini.
Baada ya masaa mawili mfanyakazi akatuma tena sms "boss nakuja kazini nimeshambusu mkeo"

Swali kwa studentiii

Mwalimu: Haya nani anaweza kuniambia njia rahisi ya kuwa milionea?
Mwanafunzi mmoja: "Ni kuolewa na millionea."

Afadhali sija...

Jamaa akitembea njiani ghafla aliona asichokielewa akasimama na kugusa na kidole akalamba kupata testi. Akagundua kua ni poo (haja) ya mbwa kisha akanena "doh afadhali sijakikanyaga" ...lakini amekionja...

Saturday, January 14, 2012

Swali

Jamaa mmoja aliuliza swali hili "mbona tukikutana petrol stations hatupeani ofa ya mafuta kama bia tukiwa bar?" Jibu unalo.

Wapi leseni?

Askari (trafik) alimsimamisha dereva mmoja kwa spidi kubwa na kumuambia "unakimbiza sana gari, hebu nipe leseni yako"
Dereva akajibu "jana tu umeichukua leseni yangu, sa nikuonyeshe passport au?"

Kitu 100mil

Bibi kizee alishinda milioni 100, akapewa mtu ampe utayari kisaikolojia kuzipokea hizo pesa zisije muua kwa presha.

Mwanasaikolojia: Bibi ukipata 10mil utafanya nini?
Bibi: Ntanunua ng'ombe wa kulimia mashamba yangu.
Mwanasaikolojia: Ok, je 20?
Bibi: Ntanunua trekta niendeleze kilimo.
Mwanasaikolojia: Sasa je ukipata 100mil?
Bibi: Ntakupa wewe mimi ntashindwa pa kuziweka.
Mwanasaikolojia presha ikapanda na kumuua.

Friday, January 13, 2012

Dah aibu kusema

Njemba moja ilikua na korodani 3 alipofika kwa dokta kwa aibu ilimbidi aongee hivi:
Njemba: Dokta, kwa mfano mimi na wewe jumla tuwe na korodani 5...
Kabla hajamalizia dokta akadakia
Dokta: Usiniambie wewe unazo nne jumla?

Dawa

Kwenye simu...
Mama: We Daudi umempaka mdogo wako ile dawa ya kuchua mkononi?
Daudi: Ndio mama nime-mnywesha asubuhi na mchana...

Opena...

Kwenye simu maongezi...
Mwanaume: Dokta mtoto wangu amemeza opena.
Dokta: Usiwe na wasi wasi atakua salama tu.
Mwanaume: Sasa ntawafunguliaje soda wageni?

Tangazo kwa abiria

Wakiwa angani tangazo kwenye ndege lilitolewa kama ifuatavyo "mabibi na mabwana tunaomba radhi safari yetu leo itachelewa dakika 7 zaidi, hii ni kulingana na rubani tulie nae leo ni mgeni wa njia pia ni kipofu..."

Kisanga cha...

Jamaa ambae mke wake nesi alikua akimsimulia jambo mkewe, "si unamjua dokta shabani? Kanyang'anywa leseni ya udokta kisa alikua ana fanya mapenzi na wagojwa wake."

Mtoto wa jamaa akiemsimulia mkewe akadakia na kusema "sasa baba hapa nyumbani utamfukuza mama au houseboy wetu?"

Mzee wa miaka 90

Mzee mmoja wa miaka 90 alitaka kumuoa msichana wa miaka 30, akaenda kwa dokta wake kwanza.
Dokta akamuambia "ohh okay sasa toa vitendea kazi vyako nikague kama utaweza mzalisha huyo msichana" mzee akatoa ulimi na kidole cha kati.

Faida za maziwa ya mama

Kijana alikua kwenye mtihani, moja ya swali aliuliza faida 3 za maziwa ya mama akajibu:
a) Yana rutuba kwa afya ya mtoto.
b) Hayapatwi na bacteria.
c) Yapo kwenye kibebeo kinachovutia wanaume.

Thursday, January 12, 2012

Bar na watu wachache

Jamaa mmoja aliingia bar ilikua ya ndani hivi na watu wachache. Akapita kila meza, kila alipomaliza kuongea neno meza husika walitoka nje. Mpaka akabaki mhudumu wa kaunta tu. Alipomaliza akatoka nje ma kuwaambia warudi ndani.

Walikuta bia zao zote jamaa kanywa, mmoja akatoka mbio na kumfukuza. Kila akijaribu kumuacha jamaa huyu hapa nyuma akauliza "we unanifukuzia nini?" Jamaa akajibu "umekunywa bia yangu niliweka sumu, naitaka."

Ndoa ijayo

Ofisini kulikua hivi:
Mfanyakazi: Boss naomba off kesho nisije nna party ya kumvisha pete mchumba wangu.
Boss: Mwanamke gani chizi atakukubali wewe?
Mfanyakazi: Ni mwanao Jesca boss.

Mgonjwa wa akili

Mgonjwa wa akili alikua akikojoa ghorofani kuelekea chini. Alipomuona nesi akaahirisha. Baadae kumuuliza mbona ulipomuona nesi ui liacha akajibu "angenivuta je si ningeanguka!"

Wednesday, January 11, 2012

Mwizi a.k.a kibaka

Mwizi aliamua kumteka mtoto mmoja wa miaka 10 akikatisha nae sehemu yenye giza nene...
Mtoto: Naogopa...
Mwizi: Sa unafikiri ntakatisha na nani hapa?

Bangi zime...

Jamaa alipiga polisi simu "haloo, jirani yangu ameficha bangi kwenye kuni nyumbani kwake"
Kesho yake polisi walifika na kupekua pamoja na kupasua pasua kuni bila kuona bangi.

Jirani akampigia simu jirani yake "vipi polisi walikuja?" Jamaa akajibu "ndio"
Jirani akaendelea "unaona nlikuambia watakusaidia kupasua kuni, sasa zamu yako wapigie waambie nimefukia cocain kwenye bustani yangu."

Mgojwa hasira

Mgonjwa: Dokta nnasumbuliwa sana na hasira za mara kwa mara hata jambo dogo tu mi ni hasira.
Dokta: Tatizo haswa ni nini?
Mgonjwa: Si nimeshakuambia pumbavu zako unakua kama mwehu bwana.

Kitu msikitini

Msikiti mmoja wakati wa swala ya ijumaa, sheikh alitoa mawaidha muda mrefu saana. Waumini wakaanza ondoka mmoja mmoja.

Mmoja akabaki, sheikh akanena "bora wewe umebaki hao wengine wamekosa heshma"
Muumini akajibu "mi mwenyewe nasubiria mkeka wangu uliokalia."

Mwizi

Jamaa alikua akiandika meseji kwa boss wake akiwa katika daladala kuwa atachelewa kidogo kazini. Ghafla alipomaliza kuandika mwizi akaikwapua jamaa badala ya kuita mwizi... Mwizii akamuambia "bonyeza send, bonyeza send..."

Unyumba

Mwanamke akiwa mbele ya wazazi wake, yaani,wakwe wa mumewe.
Mwanamke: Wazazi wangu nimewaita mume wangu hanipi unyumba kabisa wiki sasa.
Mzazi: Mkwe wetu haya tuambie nini shida?
Mume: Dokta kaniambia nisipendelee vitu vitamu kwa sababu nna kisukari.

Kila kitu kikubwa

Kipofu aliagiza bia wakamletea kwenye jagi kubwa. Akanena "hee mbona kubwa hivi?"

Wa pembeni akajibu "Dar kila kitu kikubwa"
Kipofu akaomba kwenda chooni, akaingie mlango wa pili kushoto.

Kipofu akaingia mlango wa 3.
...akatumbukia kwenye bwawa la kuogelea akijua katumbukia kwenye choo akawa anapayuka kwa sauti "usiflash... Usiflash..."

Tuesday, January 10, 2012

Taxi driver mpya

Abiria kwenye taxi siti alimgusa bega dereva, alistuka mpaka kugonga ukuta wa watu.
Dereva: Dah kaka usifanye hivyo tena.
Abiria: Hamna shida nilikua nakuita tu.
Dereva: Ndio, leo ndio nimeanza hii kazi ya taxi kabla ya hapo nikiendesha gari la kubeba maiti.

Mteka nyara

Njaa ilimbana jamaa akaamua kumteka nyara mtoto wa miaka 6. Akamuandikia kikaratasi kimeandikwa hivi:
"nimemteka mwanao, anakuja kukupatia hiki kikaratasi na kesho uweke milioni 10 kwenye kona pale jalalani"

Mwenye mtoto nae akaandika kikaratasi na kumtuma mtoto kimeandikwa hivi:
"Kivo huu si mwandiko wako asa inakuwaje unamteka mwanangu?"

Maandazi 6

Mwalimu: Joseph nikikupa maandazi 6 nkatoa mawili yatabaki mangapi?
Joseph: Kama ukinipa na mchuzi halibaki hata moja.

Monday, January 9, 2012

Nyoka na panya

Nyoka: Oya vipi mbona unaniangalia sana?
Panya: Mbona unajistukia?
Nyoka: Muone ndo maana una ndevu...
Panya: Bora mie, we kubwa zima watambaa hadi leo.

Sunday, January 8, 2012

Darasa la hisabati

Mama: Mbona umenuna mwanangu?
Mtoto: Mwalimu wa hesabu hajaja leo.
Mama akajua mwanae kichwa kwenye hesabu na kupenda.
Mama: Usijali mwanangu ntamuambia aje kukufundisha hapa hapa nyumbani.
Mtoto: Tatizo yeye pekee ndio anauza ubuyu ndio maana.

Sumu ya panya

Jamaa aliwategea sumu ya panya kwwnye nyama ya nguruwe nyumbani kwake. Asubuhi alipoamka akakuta kikaratasi kimeandikwa "hatuli nguruwe, we samaki kesho uone."

Utambulisho

Walipofika mbeya kikazi wakati wa kujitambulisha.
Wa mimi naitwa Mwakasitu.
Wa pili: Mimi naitwa Mwakasege.
Wa tatu anaitwa Juma nae akanena "mimi naitwa Mwajuma"

Friday, January 6, 2012

Ombaomba

Mwanamke alikaa kwenye viti vya bustani za katikati ya mji. Punde akaja ombaomba wa kiume.

Ombaomba: Oh mpenzi umekuja tu-enjoy.
Mwanamke: {kwa hasira} We umechanganyikiwa...!!?
Ombaomba: Sasa unafanya nini kitandani kwangu.

Mkojo ulibana

Jamaa alibanwa mkojo, akawa mbio mbio anakimbilia chooni kukojoa. Bahati mbaya akajikojolea njiani. Akaamua kurudi kwenye mkutano ivo ivo kwa vile ameshakojoa.

Majambazi

Majambazi waliingia benk kuiba, baada ya kubeba fedha za kutosha wakati wanaindoka mmoja wa majambazi waliovaa mpaka usoni; alimuandikia namba mrembo mmoja wa pale kauta namba ya simu vile amemzimikia.

Mchina kaibiwa

Mchina alipigwa mtama na kibaka akaibiwa simu. Mchina akaanza mfukuza kibaka, kibaka akaona isiwe tabu akaidondosha simu. Mchina akaiokota na kuendelea mfukuza.

Kibaka "we si nimekupa simu yako?"
Mchina akajibu "ndio umenipa bado mtama"

Tuesday, January 3, 2012

Mapacha

Mke alizaa mapacha, mume alipofika hosp. Akamuuliza mkewe "huyu mtoto m1 wangu na huyu mwingine utanieleza vizuri wa nani?"

Ndoa ikifungwa

Padre akiuliza umati kabla ya kufungisha ndoa kanisani "kuna yeyote mwenye kipingamizi ndoa hii isifungwe?"

Sauti ikasikika nyuma "padre subiri kidogo." Kisha jamaa akasogea mbele mbele.
Padre: Je, unapingamizi lolote ndugu?
Jamaa: Hapana kule nyuma nlikua sikusikii vizuri.

Maiti ikioshwa

Maiti ilikua inaoshwa, ngafla ikaanza kucheka waoshaji wakauliza "hii maiti inacheka nini?"
Maiti ikajibu "mnanitekenya bwana alahh!"

Mapadre na vekeshen

Ma-padre wawili walenda mbali kidogo kula starehe (bata). Ili wasijulikane wakanunua nguo na kupiga swaga za mtaani. Punde akapita dada mmoja wakammezea mate, dada akawasalimia "fatha mambo?"

Wasijue kawajuaje... Siku ya pili na ya tatu ivo ivo wakamuuliza: "we umetutambuaje...?"
Dada akajibu: Mi si Sister Rosa umenisahau?

Monday, January 2, 2012

Condom

Vijana wawili walienda mbiombio kwa dokta:
Kijana: Dokta nimemeza condom bahati mbaya nisaidie kuitoa.
Dokta: Huyu uliekuja nae yeye ni nani yako?
Kijana: Rafiki yangu ndio mwenye condom yake.

Nzuri na mbaya

Dokta: Mzee nna habari mbaya na nzuri, nianze ipi?
Mzee: Anza na mbaya ifuate nzuri.
Dokta: Mbaya mguu wako tumeukata kabisa. Na nzuri nitakununulia kiatu kwa bei rahisi tu.

Sunday, January 1, 2012

Alipobanwa mtihani

Mwanafunzi alibambwa kwenye mtihani:
Mwalimu: Uliiua unampigia simu nani akupe majibu?
Mwanafunzi: Mwalimu ile haikua cheating mtu nliempigia hajui jibu pia.

Jaza fomu

Jamaa mmoja alipokwama kujaza kwenye fomu.
Jamaa: Samahani sikumbuki jina la hospitali nlilozaliwa.
Mhudumu: Si lazima hospitali jaza mji uliozaliwa tu.
Jamaa: Nimejaza Kitandani, ndii sehemu nlipozaliwa.

Mwaka Mpya.

Heri ya Mwaka Mpya kwa wanablog hii wote.
Mwenyezi Mungu ashukuriwe.