Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Sunday, January 4, 2015

Mama akimuambia mwanae jambo, "Steve tafadhali kuwa makini na hiyo nyundo, utajiponda vidole." Steve nae akajibu, "Usijali mama, Emma ndio atashikilia msumari."
Baba: Juma umeliona gazeti langu? Juma: Ndio, mama kalivurugavuruga na kulitupa. Baba: Agghh! Nilikua nataka yaliyomo kabla hajalitupa. Juma: Nikusimulie, kulikuwa na maganda ya nyanya, vitunguu na karoti.
Baba: Mwanangu, nina habari nzuri. Umepata mdogo wako wa kike sasa. Mtoto: Oh! Kweli baba? Mama ana hizi taharifa?
Sauti toka kwenye simu: Halo, mama ako yupo nyumbani? Msichana kakajibu: Ndio yupo Sauti kwenye simu: Unaweza kumuita aje niongee nae tafadhani? Msichana: Sawa, inabidi niende mtaa wa pili kumuita. Sauti kwenye simu: Nilidhani umesema yupo nyumbani lakini? Msichana: Ndio yupo. Hii simu ni nyumbani kwa rafiki yangu, sie tunaishi mtaa wa pili.