Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Thursday, May 19, 2011

Swali kwa mwanafunzi

Mwalimu: Mfano nikikupatia paka wawili, na wengine wawili na mwingine tena wawili je utakua na wangapi?

Mwanafunzi: Saba mwalimu.
Mwalimu: Hapana, sikiliza tena... (Mwl. Aliuliza vile vile)

Mwanafunzi: Saba Mwalimu.
Mwalimu: Ngoja nikupe mfano mwingine, mikikupa maembe mawili, na mengine mawili na mawili tena je ni mangapi ntakua nimekupa?

Mwanafunzi: Sita.
Mwalimu: Saaafi sana.

Mwalimu: Haya marudia lile swali la awali (Mwalimu akauliza vile vile tena).
Mwanafunzi: Saba.

Mwalimu akanena kwa hasira, ''shut up hiyo saba unaipata wapi sasa?''
Mwanafunzi akajibu, '' kwa sababu tayari ninae paka mmoja nyumbani!''

No comments:

Post a Comment