Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Monday, August 29, 2011

Mke apokea simu

M'ke mmoja alipokea simu toka kwa mumewe (namba ngeni) akawa anajibu hivi (huku wote wakiwa ndani ya nyumba) "nipigie baadae hili fala lipo ndani saa hizi"

Mzee kwa dokta

Mzee: Dokta mkono wangu wa kushoto unauma sana!
Dokta: Usihofu ni hali ya uzee tu hiyo.
Mzee: Kama ndio hivyo mbona na wa kulia pia unauma?

Sunday, August 28, 2011

Lofa

Dogo mmoja aliingia saloon, kinyozi akawaambia wateja oneni huyu dogo ndio lofa kweli. Akachukua noti ya elfu 10 na 200Tsh. Dogo akachukua 200Tsh.

Kinyozi akanena, mnaona niliwaambia. Baadae mmoja wa wateja alikutana na dogo akamuuliza mbona hukuchukua ile elfu 10? Dogo akajibu "nikiichukua.tu mchezo utaisha"

Wiki 1 kuolewa

Msichana: Naolewa wiki ijayo, party itakua ya wachache na maalumu.
Mvulana: Ok! Utapendelea zawadi gani muhimu?
Msichana: Niletee mtu atakaenioa.

Kuwa nani maishani?

Mwanaume mmoja aliulizwa katika maisha yako unatamani kuwa kama nani? Akajibu "mende"
Alieuliza akashangaa na kuuliza kwanini?
Mwanaume akajibu "mke wangu anamuogopa sana mende kuliko mimi"

Nauli

Kwenye daladala jamaa alilipa nauli kwa kondakta. Kisha baada ya muda akamuambia konda "hehehe leo siku ya wajinga nlishalipa ticket hii hapa"

Saturday, August 27, 2011

Ratiba

Mpita njia: Haina haja ya kuwa na ratiba ya treni wakati kila mara inachelewa!
Injinia: Tutajuaje kama inachelewa kama tusingekua na ratiba sasa?

Samaki

Kijana mmoja alinunua samaki wawili wa kufuga akawapa majina mmoja A mwingine B. Rafiki ake akamuuliza "sa kwa nini umewapa majina hayo?" Akajibiwa "ili akifa A bado ntabaki na B"

Ujinga Ni...

1. Kujiita romantic na uko single.
2. Kukaa mbele kwa daladala alafu unaturn kwambia konda 'shusha' na umekaa na driver
3. Kutumia cursor kuscare mosquito itoke kwa screen ya comp.
4. Kureduce volume ya radio usome sms.
5. Kuruka line Angaza.
6.Kupigiwa simu halafu unaangalia balance yako after the call.
7. Kutafuta remote ya TV for 10 min, na tv iko a step away
8. KuDELETE namba ya ex wako na unaijua off head
9. Kubargain kitu kutoka 1000 hadi 500 alafu bado unapea muuzaji 5000 akupatie change
10. Kubuy beer ingine moja ukitegea fare ishuke hadi 200 ucku mkali
Jamaa na familia yake walienda kutoa mahari mida ya saa moja moja hivi kagiza kameanza kuingia, ghafla umeme ukakatika, mkwe akatamka kwa waliokuja kutoa mahari "pia tulisahau kujumuisha kwenye list ya mahari, jenereta pia linahitajika..."

Plastic Surgery

Dada mmoja mguu kwa mguu mpaka hospitali moja ya kukarabati sehemu za mwili ikiwepo sura yaani "plastic surgery" alipofika ikawa hivi:
Dada: Kufanya Plastic Surgery Shilingi ngapi?
Daktari: Inagharibu Laki moja taslimu.
Dada: Je, nkija na plastic langu bei itapoa?

Birthday.

Katoto ka miaka mitano siku ya kusherekea tarehe ya kuzaliwa kwake aliulizwa na baba ake anapendelea zawadi gani akajibu "nimezunguka sana sijapata size yangu, wewe ukipata ninunulie condom nne tu"

Bi. Kizee na uzee wake

Bi. Kizee mmoja alienda hospitali, akamkuta mwanadada mjamzito akamuuliza "mbona tumbo lako kubwa?"
Mjamzito akajibu "nina mimba"
Kizee: Ooh una mimba? Unamaanisha una mtoto?
Mjamzito: Ndio.
Kizee: Sasa kwa nini umem-meza?

Friday, August 26, 2011

Hii ya msalani

Ndani ya vyoo vya hoteli mlango mmoja kuna mtu na unaofuata una mtu wakikata gogo, jamaa mlango wa pili alianzisha maongezi ifuatavyo:

Mlango wa 1: Habari yako?
Mlango wa 2 akajibu bila kujielewa kinachoendelea "nzuri tu"
Mlango 1: Unafanya nini sasa hivi?
Mlango 2 bado akawa haelewi elewi akajibu "nipo nafanya kama wewe.."
Mlango 1: Naweza kuja?
Mlango 2 baado akazidi shangaa huku akijibu "hapana usije nipo bize"

Baada ya hapo Mlango 1 akasikika akisema "ngoja nitakupigia simu tena kuna mtu naona anajibu maswali sio yake"

Njemba hizi...?

Njemba mbili zilienza kwenye Pub, wakaagiza vinywaji kisha kila mmoja akafungua mfuko na kutoa burger na kuanza kula. Mhudumu akaja na kuwaambie "samahani hairuhusiwi kula burger yako hapa"
Njemba zikaangaliana wakatikisa bega na kubadilishana burger zao na kuendelea kula.

Karanga

Kizee kimoja kwenye daladala alimpa kondakta karanga, baada ya mda akampa tena zingine. Konda akauliza "we mbona huli?"
Kizee akajibu "sina meno" Konda akauliza "sa umenunua za nini?"
Kizee kikajibu "mi napenda chocolate iliopo juu ya karanga tu"

Darasani

Mwalimu akifundisha darasani:
Mwalimu: Wee Kelvin kwa nini unaongea darasani wakati nafundisha?
Mwanafunzi: Na wewe kwanini unafundisha wakati sijamaliza maongezi?

Kijana na mapenzi

Kijana mmoja alikua anampenda msichana mmoja ila akishindwa kumuambia. Siku moja akamtumia email na kumuambia "nakupenda sana" kisha akaituma. Punde akasikia kama kuna email imeingia. Akasamua asiisome aje aisome asubuhi iwe kama 'surprise' kwake.

Ilipofika asubuhi akaenda ili alisome akakuta ujembe umeandikwa hivi "Message sending failed due to insufficient balance! Please recharge your Account."

Thursday, August 25, 2011

Blackberry

Jamaa mmoja akitumia simu ya blackberry aliwatumia ujumbe wenzake kwenye mfumo wa kucha kama ifuatavyo "Warning: don't accept request from Muammar Gaddafi (218DE940) he is looking for a place to stay!"

Ubishi ubishi

Walikua wanabishana bwana, njemba moja ikanena "mi nlirudi usiku mkubwa wife akafungua mlango na nyodo, kumkomoa nikaamua kusimama mlangoni mpaka asubuhi na mpaka leo hatugusani"

Rafiki akamuuliza, "haiwezekani? Sa mtoto mmpempatia wapi?" Njemba ikajibu "mi nshasema simgusi mtoto itakua aliiba mimba ya mtu tu si bure"
Jamaa na rafiki zake wawili aleinda nao kwao, alipofika mlangoni mwenyeji akachomoa ufunguo wa mlango alipoificha rafiki zake wakimuangalia huku akinena "hapa ndio nafichaga ufunguo ila kesho nautoa hapa"

Tuesday, August 23, 2011

Ulevi noma

Mlevi mmoja mchana wa jua kali alikua tayari pombe mtu, akapanda daladala sasa lile joto na hewa nzito si akazomea ardhi (kutapika), baada ya hapo akamuambie kondakta "konda njoo udeki" punde kwenye foleni akaona bajaj nje ipo kwenye foleni mlevi akanena "wee dereva wa bajaj una ufagio?"

Sunday, August 21, 2011

Mbakaji

Polisi huku kamshikilia njemba moja wakiwa mbele ya jimama moja, polisi akamuuliza yule mama "huyu ndio kijana aliekubaka?"
Yule mama akajibu "Sijui labda arudie tena ndio ntamjua"

Mziki kwenye simu

Jamaa mmoja alienda kwenye party! Kuna mziki ambao upo kwenye simu yake ukapigwa na Dj kwenye hiyo party, akamuambia Dj "zima mziki mara moja" sekunde kadhaa 1 au 2 zikapita akasema "basi endelea kumbe anabeep tu"

Ikajirudia hivyo kama mara 3 hivi mwisho wa siku kumbe alikuja gundua kumbe ni mziki kwenye party na sio simu yake ikiita.

Saturday, August 20, 2011

Trafiki polisi alimsimamisha dereva mmoja mahojiano yakawa hivi:
Dereva: Afande nini shida na leo?
Trafik: Ohh wewe ndio nlikukamata jana enhe?
Dereva: Ndio mimi.
Trafiki: Na umelewa tena kama jana?
Dereva: Askari hii bado ni ile ile pombe ya jana nlikua sijaimalizia kwenye gari.

Friday, August 19, 2011

Mafuta darasani

Mwalimu akifundisha, kamuona mwanafunzi anapaka mafuta kichwani.
Mwalimu: Wee kwanini unapaka mafuta kichwani?
Mwanafunzi: Jana usiku nlisikia baba akimuambia mama paka mafuta kichwa kama haiingii. Napaka ili somo liingie.

Thursday, August 18, 2011

Mfanyakazi wa Mochuari

Mfanyakazi wa mochwari alikata dudu ya maiti moja ili akamuoneshe mkewe jinsi ulivyo mkubwa. MME: "hebu angalia dudu hii ilivyo mkubwa"MKE: "heeh zuberi amefariki"

Hii kali

Kijana mmoja alikuta ameweka kitu chenye rangi ya blue mdomoni alipoulizwa akajibu "we huoni vizuri? Si bluetooth"

Toroli

Jamaa mmoja alipata kazi ya kusafisha jiji na maeneo yake! Sasa kwa vile ni mgeni kazini, siku ile ile ya kwanza wakati anakokota toroli lake la kuzolea taka akalibandika ile stika yenye herufi "L" akimaanisha "Learner kama kwenye magari"

Cheka unenepe!

Wednesday, August 17, 2011

Siku ya siku

Baba alimkuta mwanae anachemsha maji kuuliza akajibiwa "baba mi mesoma havipandi hapa nachemsha madaftari ninywe maji yake tu, kesho mtihani"