Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Friday, August 26, 2011

Hii ya msalani

Ndani ya vyoo vya hoteli mlango mmoja kuna mtu na unaofuata una mtu wakikata gogo, jamaa mlango wa pili alianzisha maongezi ifuatavyo:

Mlango wa 1: Habari yako?
Mlango wa 2 akajibu bila kujielewa kinachoendelea "nzuri tu"
Mlango 1: Unafanya nini sasa hivi?
Mlango 2 bado akawa haelewi elewi akajibu "nipo nafanya kama wewe.."
Mlango 1: Naweza kuja?
Mlango 2 baado akazidi shangaa huku akijibu "hapana usije nipo bize"

Baada ya hapo Mlango 1 akasikika akisema "ngoja nitakupigia simu tena kuna mtu naona anajibu maswali sio yake"

No comments:

Post a Comment