Mtoto mmoja aliporudi nyumbani toka shuleni akawa anamsimulia baba yake, ''baba leo tumepelekwa jumba la makumbusho tumejifunza mengi''
Baba akanena, ''safi sana mwanangu.''
Mtoto: Pia nimewaambia waje nyumbani kukuona.
Baba: Enh??!! Kuniona? Akina nani?
Mtoto: Si watu wa makumbusho:
Baba: Mimi wananifuata ili iweje.
Mtoto: Nimewaambia baba angu ana gari la zamani na linatoa sana moshi, na wao wanataka gari la zamani linalotoa moshi mwing kama lako.
Karibu Sana.
Cheka Unenepe
Tuesday, November 30, 2010
Afrika kusini
Mama: Mume wangu safari bado haijaiva.
Baba: Najipanga mke wangu, South Africa maisha yapo juu kidogo.
Mtoto: Mhh! Baba, we si ulisema unaenda Afrika Kusini? Mbona mama unamdanganya unamuambia unaenda South Africa?
Baba: Najipanga mke wangu, South Africa maisha yapo juu kidogo.
Mtoto: Mhh! Baba, we si ulisema unaenda Afrika Kusini? Mbona mama unamdanganya unamuambia unaenda South Africa?
Maneno
Mwanaume mmoja alifuatwa na jirani mwema na kumuambia ''baba nanihi nimemuona mke wako yupo na mwanaume mwingine muda huu huu.''
Mwanaume aliefuatwa akajibu, ''ooh bora mwanaume maana nlishamkataza kukaa na wanawake umbea mwingi.''
Mwanaume aliefuatwa akajibu, ''ooh bora mwanaume maana nlishamkataza kukaa na wanawake umbea mwingi.''
Monday, November 29, 2010
Mke na mume
Mwanamke mmoja alikua amekaa sebuleni na mwanae, punde akachukua simu na kumpigia mumewe huku simu ikiwa katika sauti kubwa (loud speaker) ''mume wangu upo wapi? Mbona unachelewa kujibu''
Mume akawa anajibu kupitia simu, ''naja punde mke wangu nipo kwenye jam''
Kale katoto kakaenda jikoni na kurudi huku kakimuambia mama yake ''mama...mama... Baba muongo mbona hayupo humu kwenye chupa ya Jam'' (mithili ya siagi)
Mume akawa anajibu kupitia simu, ''naja punde mke wangu nipo kwenye jam''
Kale katoto kakaenda jikoni na kurudi huku kakimuambia mama yake ''mama...mama... Baba muongo mbona hayupo humu kwenye chupa ya Jam'' (mithili ya siagi)
Unataka kusoma nini
Baba mmoja alikaa kibarazani na mwanae wa miaka minne akiongea nae, akamuuliza swali ''mwanangu ukikua mkubwa ungependa kusoma nini?''
Mtoto nae bila hiyana akamjibu Dad yake, ''mimi baba? Nikikua nataka nisome magazeti''
Mtoto nae bila hiyana akamjibu Dad yake, ''mimi baba? Nikikua nataka nisome magazeti''
Mavituzi
Mwanamke mmoja wa kipemba alikuja Dar, siku moja akaopolewa na kidume. Alipewa malavidavi moto moto ikiwa kunyonywa kona zote.
Siku aliporudi kwa mumewe zanzibar wakati yupo na mumewe wakati wa malavidavi akamuambia ''mume wangu, Dar yaliwa hiyo''
Siku aliporudi kwa mumewe zanzibar wakati yupo na mumewe wakati wa malavidavi akamuambia ''mume wangu, Dar yaliwa hiyo''
Dogo
Dogo mmoja akimuambia ama kumuuliza baba yake, ''baba... nyumba ina dirisha, gari lina dirisha, ndege ina dirisha sasa mbona hamna dirisha kwenye baiskeli?''
Sunday, November 28, 2010
Chai time
Jamaa mmoja alikua anapita sehemu karibu na mgahawa, akaona mini-bus aina ya Coaster ina jeneza imepaki ikiashiria wasindikiza maiti wanapata kifungua kinywa.
Akamuita dereva wa ile bus na kumuuliza:
Jamaa: Samahani we ndi dereva?
Dereva: Ndio kaka, kulikoni?
Jamaa: Mbona mmesimama hapa?
Dereva: Mkuu tunapata chai kidogo safari ndefu.
Jamaa: Sasa mwenzenu kwenye jeneza mbona hamjamnunulia hata andazi?
Akamuita dereva wa ile bus na kumuuliza:
Jamaa: Samahani we ndi dereva?
Dereva: Ndio kaka, kulikoni?
Jamaa: Mbona mmesimama hapa?
Dereva: Mkuu tunapata chai kidogo safari ndefu.
Jamaa: Sasa mwenzenu kwenye jeneza mbona hamjamnunulia hata andazi?
Friday, November 26, 2010
Ajali kusimulia
Dogo mmoja akiwasimulia wenzake ''dah, baba angu si kapata ajali?''
Dogo wa pili, ''kagongwa na gari?''
Dogo wa kwanza, ''ndio! Yaani bora kagongwa na benz kuliko ingekuwa corolla''
Dogo wa pili, ''kagongwa na gari?''
Dogo wa kwanza, ''ndio! Yaani bora kagongwa na benz kuliko ingekuwa corolla''
Taratiibu
Jamaa mmoja alikua na mpenzi wake chumbani, alipotoka bafuni mchumba wake akamuambia ''ee chupi yako saafi''
Jamaa alipofika kitandani akawa anakaa taratiiiibu saaana, mpenziwe akamuuliza ''vipi misuli imekushika?''
Jamaa akajibu, ''naogopa ntaichafua chupi''
Jamaa alipofika kitandani akawa anakaa taratiiiibu saaana, mpenziwe akamuuliza ''vipi misuli imekushika?''
Jamaa akajibu, ''naogopa ntaichafua chupi''
Mimba
Baba mmoja akifanya ishara kadha wa kadha mbele ya tumbo la mkewe ambae ni mjamzito.
Mkewe alimuangaliaa mwisho akashindwa vumilia akamuuliza ''kwani mbona sikuelewi mwenzangu?''
Mumewe bila hiyana akamjibu, ''we huoni kuwa namfundisha mwanangu tangu akiwa tumboni akitoka awe trafiki polisi?''
Mkewe alimuangaliaa mwisho akashindwa vumilia akamuuliza ''kwani mbona sikuelewi mwenzangu?''
Mumewe bila hiyana akamjibu, ''we huoni kuwa namfundisha mwanangu tangu akiwa tumboni akitoka awe trafiki polisi?''
Kuonja
Mtoto: Mama hiyo unayotengeneza ni nini?
Mama: Natengeneza sumu nimuwekee baba yako ananiudhi sana.
Baada ya masaa kadhaa.
Mtoto: Mama nimeionja ile sumu taamu, baba atafaidi kweli leo.
Mama: Natengeneza sumu nimuwekee baba yako ananiudhi sana.
Baada ya masaa kadhaa.
Mtoto: Mama nimeionja ile sumu taamu, baba atafaidi kweli leo.
Mtoto akisimulia jambo
Mtoto: Mama nikuambie kitu?
Mama: Niambie tu mwanangu.
Mtoto: Haya, kwani baba muoga eenhe?
Mama: Mh!! Kwa nini mwanangu?
Mtoto: Maana ukisafiri huwa anaogopa kulalia godoro anamlaliaga dada wa kazi tuuu.
Mama: Niambie tu mwanangu.
Mtoto: Haya, kwani baba muoga eenhe?
Mama: Mh!! Kwa nini mwanangu?
Mtoto: Maana ukisafiri huwa anaogopa kulalia godoro anamlaliaga dada wa kazi tuuu.
Wednesday, November 24, 2010
TV
Mtoto mmoja alizoea kuona TV za kisasa tangu amezaliwa. Siku moja akaenda kutembelea ndugu zao alipofika akaona TV zile zenye kichogo nyuma akamuita baba yake na kumuuliza ''baba hii nini nyuma ya TV?''
Kwa dokta
Dokta mmoja wa kiume akimhudumia mama mjamzito.
Dokta: Hii ni mimba yako ya kwanza?
Mjamzito: Ndio, hivi huwa inauma wkati wa kujifungua?
Dokta akajibu, ''mimi mbona nlijifungua bila maumivu''
Dokta: Hii ni mimba yako ya kwanza?
Mjamzito: Ndio, hivi huwa inauma wkati wa kujifungua?
Dokta akajibu, ''mimi mbona nlijifungua bila maumivu''
Bata
Kibosile mmoja alienda kuangalia sarakasi, mwanasakasi mmoja akawa amemuweka bata chini ya beseni amemfunika juu chini huku akiruka ruka na kucheza.
Yule kibosile akaongea na jamaa mpaka akamunua yule bata. Siku chache mbele akampigia simu yule aliemuuzia, ''halo... Mbona bata hachezi kama siku ile?
Jamaa akamjibu, ''ulikumbuka kumuwashia mshumaa?''
Yule kibosile akaongea na jamaa mpaka akamunua yule bata. Siku chache mbele akampigia simu yule aliemuuzia, ''halo... Mbona bata hachezi kama siku ile?
Jamaa akamjibu, ''ulikumbuka kumuwashia mshumaa?''
Tuesday, November 23, 2010
Hela iko wapi?
Mama akimuuliza mama yake.
Mama: Jesca mwanagu ile pesa yangu pale mezani ipo wapi?
Mtoto: Ooh! Nimeitumia mama ila niliitoa photocopy nimekuachia kopi.
Mama: Jesca mwanagu ile pesa yangu pale mezani ipo wapi?
Mtoto: Ooh! Nimeitumia mama ila niliitoa photocopy nimekuachia kopi.
Friday, November 19, 2010
Mtoto na mama yake
Mtoto mmoja akimuambia mama yake mjamzito alipomuona anakoroga chai. ''wee mama weewee! Shauri yako, utamuunguza mtoto tumboni''
Pesa bank
Jamaa mmoja alianza kuangua kiliobaada ya kusikia taharifa ya habari, kuulizwa kulikoni akajibu ''nimesikia kwenye taharifa ya habari bank ya cbn imeibiwa milioni mia tawi la mjini''
Jamaa akawa hajamuelewa, ''sasa wewe unalia nini?''
Anaelia akajibu, ''si jana tu nimeweka milioni mia tawi lile lilee'' (huku akifuta machozi)
Msimuliwaji alicheka mpaka akakaa chini na kumuambia ''hehehe imeibiwa bank au wewe? Hahahaha!''
Jamaa akawa hajamuelewa, ''sasa wewe unalia nini?''
Anaelia akajibu, ''si jana tu nimeweka milioni mia tawi lile lilee'' (huku akifuta machozi)
Msimuliwaji alicheka mpaka akakaa chini na kumuambia ''hehehe imeibiwa bank au wewe? Hahahaha!''
Kituo cha polisi
Jamaa mmoja alienda mpaka kituo cha polisi akafika na kuuliza, ''nna tatizo nyumbani kwangu''
Polisi akamuuliza: Tatizo gani hilo lililokuleta?
Jamaa akajibu: Kuku wangu wawili wameibiwa na mbwa wenu.
Polisi: Mbwa wetu?
Jamaa: Si yule mbwa anaitwa polisi kwani sio wenu?
Polisi akamuuliza: Tatizo gani hilo lililokuleta?
Jamaa akajibu: Kuku wangu wawili wameibiwa na mbwa wenu.
Polisi: Mbwa wetu?
Jamaa: Si yule mbwa anaitwa polisi kwani sio wenu?
Wednesday, November 17, 2010
Siku ya kwanza shuleni
Mama alimuuliza mwanae baada ya kurudi kutoka shule siku ya kwanza, ''enhe mwanangu umejifunza nini leo shuleni?''
Mtoto akamjibu mama yake ''bado sijajifunza vya kutosha itabidi nirudi tena kesho''
Mtoto akamjibu mama yake ''bado sijajifunza vya kutosha itabidi nirudi tena kesho''
Tuesday, November 16, 2010
Dawa ya usingizi
Jamaa: Dokta zile dawa ulizonipa jana mbona ni za usingizi?
Dokta: Ndio, si ndio ulizotaka nikupatie?
Jamaa: aah mi nlitaka za kulala sio za usingizi.
Dokta: Ndio, si ndio ulizotaka nikupatie?
Jamaa: aah mi nlitaka za kulala sio za usingizi.
Teja
Teja moja (bwia unga) alikuwa kituo cha daladala akiitia/piga debe daladala ''tandika tandika gari...'' huku anasinzia na ule ulevi wao wa kubwia unga.
Kuja kuhamaki ''kumbe daladala ishatimua kitaambo kama dakika tano zilizopita''
Kuja kuhamaki ''kumbe daladala ishatimua kitaambo kama dakika tano zilizopita''
Sunday, November 14, 2010
Moto
Mtoto mmoja akimuambia baba yake kwenye simu wakati nyumba yao inaungua moto, ''baba... baba... Heee wahi uone nyumba yetu inaungua kaaama kwenye sinema ya James Bond vile gadi raha''
Mswaki
Jamaa mmoja alienda kwa rafiki yake na kumuambia nna bidhaa nauza ikiwemo miswaki!
Jamaa anae uziwa akanunua.
Kesho yake jamaa akapita tena ''aisee mswaki ulioniuzia mzuri nimeupenda sana.''
Jamaa akamjibu ''asante sana ipo mingine kama unataka yote used kama nliokuuzia''
Jamaa anae uziwa akanunua.
Kesho yake jamaa akapita tena ''aisee mswaki ulioniuzia mzuri nimeupenda sana.''
Jamaa akamjibu ''asante sana ipo mingine kama unataka yote used kama nliokuuzia''
Saturday, November 13, 2010
Maongezi ya vijana
Vijana watatu wa kiume na msichana mmoja wakiongea mara akapita msichana mrembo mmoja kati ya wale vijana akasema ''dah mrembo yule mtamu'' mwingine akasema ''si mchezo''
Ikafika muda wa yule dada kati ya vijana watatu akamuuliza kijana mmoja wa tatu ''Iddi wewe je?''
Iddi akajibu ''aanh mimi niko period''
Ikafika muda wa yule dada kati ya vijana watatu akamuuliza kijana mmoja wa tatu ''Iddi wewe je?''
Iddi akajibu ''aanh mimi niko period''
Kipofu kwa daktari
Kipofu alipelekwa hospitali na ndugu yake kufika hospitali nesi akawaambia ''kumuona daktari ni shilingi elfu kumi''
Yule aliempeleka hospitali kipofu akajibu, ''tumekuelewa ila huyu mwenzangu ni kipofu hawezi kumuona daktari''
Yule aliempeleka hospitali kipofu akajibu, ''tumekuelewa ila huyu mwenzangu ni kipofu hawezi kumuona daktari''
Friday, November 12, 2010
Mmassai na mzigo
Mmasai mmoja alipewa lifti kwenye kenta alikuwa amejibebesha mzigo kichwani. Alipopanda kwenye kenta akawa bado mzigo wake upo kichwani. Wakamuambia aushushe tu si yupo kwenye gari mmasai yule akakataa katu katu.
Thursday, November 11, 2010
Headphone
Jamaa mmoja alimuuliza mwenzake swali lifuatalo, ''kwani hizi headphones ni za kupitishia sauti?''
Mwenzake akamjibu ''ndio maana ake''
Akauliza tena ''hazichakachui unachokisikia kweli?''
Mwenzake akamjibu ''ndio maana ake''
Akauliza tena ''hazichakachui unachokisikia kweli?''
Subscribe to:
Posts (Atom)