Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Sunday, November 28, 2010

Chai time

Jamaa mmoja alikua anapita sehemu karibu na mgahawa, akaona mini-bus aina ya Coaster ina jeneza imepaki ikiashiria wasindikiza maiti wanapata kifungua kinywa.

Akamuita dereva wa ile bus na kumuuliza:
Jamaa: Samahani we ndi dereva?
Dereva: Ndio kaka, kulikoni?
Jamaa: Mbona mmesimama hapa?
Dereva: Mkuu tunapata chai kidogo safari ndefu.
Jamaa: Sasa mwenzenu kwenye jeneza mbona hamjamnunulia hata andazi?

No comments:

Post a Comment