Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Tuesday, November 30, 2010

Gari kutoa moshi

Mtoto mmoja aliporudi nyumbani toka shuleni akawa anamsimulia baba yake, ''baba leo tumepelekwa jumba la makumbusho tumejifunza mengi''

Baba akanena, ''safi sana mwanangu.''
Mtoto: Pia nimewaambia waje nyumbani kukuona.
Baba: Enh??!! Kuniona? Akina nani?
Mtoto: Si watu wa makumbusho:

Baba: Mimi wananifuata ili iweje.
Mtoto: Nimewaambia baba angu ana gari la zamani na linatoa sana moshi, na wao wanataka gari la zamani linalotoa moshi mwing kama lako.

Afrika kusini

Mama: Mume wangu safari bado haijaiva.
Baba: Najipanga mke wangu, South Africa maisha yapo juu kidogo.
Mtoto: Mhh! Baba, we si ulisema unaenda Afrika Kusini? Mbona mama unamdanganya unamuambia unaenda South Africa?

Maneno

Mwanaume mmoja alifuatwa na jirani mwema na kumuambia ''baba nanihi nimemuona mke wako yupo na mwanaume mwingine muda huu huu.''

Mwanaume aliefuatwa akajibu, ''ooh bora mwanaume maana nlishamkataza kukaa na wanawake umbea mwingi.''

Monday, November 29, 2010

Mke na mume

Mwanamke mmoja alikua amekaa sebuleni na mwanae, punde akachukua simu na kumpigia mumewe huku simu ikiwa katika sauti kubwa (loud speaker) ''mume wangu upo wapi? Mbona unachelewa kujibu''

Mume akawa anajibu kupitia simu, ''naja punde mke wangu nipo kwenye jam''
Kale katoto kakaenda jikoni na kurudi huku kakimuambia mama yake ''mama...mama... Baba muongo mbona hayupo humu kwenye chupa ya Jam'' (mithili ya siagi)

Unataka kusoma nini

Baba mmoja alikaa kibarazani na mwanae wa miaka minne akiongea nae, akamuuliza swali ''mwanangu ukikua mkubwa ungependa kusoma nini?''

Mtoto nae bila hiyana akamjibu Dad yake, ''mimi baba? Nikikua nataka nisome magazeti''

Mavituzi

Mwanamke mmoja wa kipemba alikuja Dar, siku moja akaopolewa na kidume. Alipewa malavidavi moto moto ikiwa kunyonywa kona zote.

Siku aliporudi kwa mumewe zanzibar wakati yupo na mumewe wakati wa malavidavi akamuambia ''mume wangu, Dar yaliwa hiyo''

Dogo

Dogo mmoja akimuambia ama kumuuliza baba yake, ''baba... nyumba ina dirisha, gari lina dirisha, ndege ina dirisha sasa mbona hamna dirisha kwenye baiskeli?''

Sunday, November 28, 2010

Chai time

Jamaa mmoja alikua anapita sehemu karibu na mgahawa, akaona mini-bus aina ya Coaster ina jeneza imepaki ikiashiria wasindikiza maiti wanapata kifungua kinywa.

Akamuita dereva wa ile bus na kumuuliza:
Jamaa: Samahani we ndi dereva?
Dereva: Ndio kaka, kulikoni?
Jamaa: Mbona mmesimama hapa?
Dereva: Mkuu tunapata chai kidogo safari ndefu.
Jamaa: Sasa mwenzenu kwenye jeneza mbona hamjamnunulia hata andazi?

Friday, November 26, 2010

Ajali kusimulia

Dogo mmoja akiwasimulia wenzake ''dah, baba angu si kapata ajali?''
Dogo wa pili, ''kagongwa na gari?''
Dogo wa kwanza, ''ndio! Yaani bora kagongwa na benz kuliko ingekuwa corolla''

Taratiibu

Jamaa mmoja alikua na mpenzi wake chumbani, alipotoka bafuni mchumba wake akamuambia ''ee chupi yako saafi''

Jamaa alipofika kitandani akawa anakaa taratiiiibu saaana, mpenziwe akamuuliza ''vipi misuli imekushika?''

Jamaa akajibu, ''naogopa ntaichafua chupi''

Mimba

Baba mmoja akifanya ishara kadha wa kadha mbele ya tumbo la mkewe ambae ni mjamzito.
Mkewe alimuangaliaa mwisho akashindwa vumilia akamuuliza ''kwani mbona sikuelewi mwenzangu?''

Mumewe bila hiyana akamjibu, ''we huoni kuwa namfundisha mwanangu tangu akiwa tumboni akitoka awe trafiki polisi?''

Kuonja

Mtoto: Mama hiyo unayotengeneza ni nini?
Mama: Natengeneza sumu nimuwekee baba yako ananiudhi sana.
Baada ya masaa kadhaa.
Mtoto: Mama nimeionja ile sumu taamu, baba atafaidi kweli leo.

Mtoto akisimulia jambo

Mtoto: Mama nikuambie kitu?
Mama: Niambie tu mwanangu.
Mtoto: Haya, kwani baba muoga eenhe?
Mama: Mh!! Kwa nini mwanangu?
Mtoto: Maana ukisafiri huwa anaogopa kulalia godoro anamlaliaga dada wa kazi tuuu.

Wednesday, November 24, 2010

TV

Mtoto mmoja alizoea kuona TV za kisasa tangu amezaliwa. Siku moja akaenda kutembelea ndugu zao alipofika akaona TV zile zenye kichogo nyuma akamuita baba yake na kumuuliza ''baba hii nini nyuma ya TV?''

Kwa dokta

Dokta mmoja wa kiume akimhudumia mama mjamzito.
Dokta: Hii ni mimba yako ya kwanza?
Mjamzito: Ndio, hivi huwa inauma wkati wa kujifungua?
Dokta akajibu, ''mimi mbona nlijifungua bila maumivu''

Bata

Kibosile mmoja alienda kuangalia sarakasi, mwanasakasi mmoja akawa amemuweka bata chini ya beseni amemfunika juu chini huku akiruka ruka na kucheza.

Yule kibosile akaongea na jamaa mpaka akamunua yule bata. Siku chache mbele akampigia simu yule aliemuuzia, ''halo... Mbona bata hachezi kama siku ile?

Jamaa akamjibu, ''ulikumbuka kumuwashia mshumaa?''

Tuesday, November 23, 2010

Hela iko wapi?

Mama akimuuliza mama yake.
Mama: Jesca mwanagu ile pesa yangu pale mezani ipo wapi?
Mtoto: Ooh! Nimeitumia mama ila niliitoa photocopy nimekuachia kopi.

Friday, November 19, 2010

Mtoto na mama yake

Mtoto mmoja akimuambia mama yake mjamzito alipomuona anakoroga chai. ''wee mama weewee! Shauri yako, utamuunguza mtoto tumboni''

Pesa bank

Jamaa mmoja alianza kuangua kiliobaada ya kusikia taharifa ya habari, kuulizwa kulikoni akajibu ''nimesikia kwenye taharifa ya habari bank ya cbn imeibiwa milioni mia tawi la mjini''

Jamaa akawa hajamuelewa, ''sasa wewe unalia nini?''
Anaelia akajibu, ''si jana tu nimeweka milioni mia tawi lile lilee'' (huku akifuta machozi)
Msimuliwaji alicheka mpaka akakaa chini na kumuambia ''hehehe imeibiwa bank au wewe? Hahahaha!''

Kituo cha polisi

Jamaa mmoja alienda mpaka kituo cha polisi akafika na kuuliza, ''nna tatizo nyumbani kwangu''
Polisi akamuuliza: Tatizo gani hilo lililokuleta?
Jamaa akajibu: Kuku wangu wawili wameibiwa na mbwa wenu.
Polisi: Mbwa wetu?
Jamaa: Si yule mbwa anaitwa polisi kwani sio wenu?

Wednesday, November 17, 2010

Siku ya kwanza shuleni

Mama alimuuliza mwanae baada ya kurudi kutoka shule siku ya kwanza, ''enhe mwanangu umejifunza nini leo shuleni?''
Mtoto akamjibu mama yake ''bado sijajifunza vya kutosha itabidi nirudi tena kesho''

Kojoleo

Mtoto mmoja wa kike alimuambia baba yake ''baba na mimi ninunulie kojoleo kama la dereva''

Tuesday, November 16, 2010

Dawa ya usingizi

Jamaa: Dokta zile dawa ulizonipa jana mbona ni za usingizi?
Dokta: Ndio, si ndio ulizotaka nikupatie?
Jamaa: aah mi nlitaka za kulala sio za usingizi.

Teja

Teja moja (bwia unga) alikuwa kituo cha daladala akiitia/piga debe daladala ''tandika tandika gari...'' huku anasinzia na ule ulevi wao wa kubwia unga.
Kuja kuhamaki ''kumbe daladala ishatimua kitaambo kama dakika tano zilizopita''

Sunday, November 14, 2010

Moto

Mtoto mmoja akimuambia baba yake kwenye simu wakati nyumba yao inaungua moto, ''baba... baba... Heee wahi uone nyumba yetu inaungua kaaama kwenye sinema ya James Bond vile gadi raha''

Mswaki

Jamaa mmoja alienda kwa rafiki yake na kumuambia nna bidhaa nauza ikiwemo miswaki!
Jamaa anae uziwa akanunua.

Kesho yake jamaa akapita tena ''aisee mswaki ulioniuzia mzuri nimeupenda sana.''
Jamaa akamjibu ''asante sana ipo mingine kama unataka yote used kama nliokuuzia''

Saturday, November 13, 2010

Maongezi ya vijana

Vijana watatu wa kiume na msichana mmoja wakiongea mara akapita msichana mrembo mmoja kati ya wale vijana akasema ''dah mrembo yule mtamu'' mwingine akasema ''si mchezo''

Ikafika muda wa yule dada kati ya vijana watatu akamuuliza kijana mmoja wa tatu ''Iddi wewe je?''
Iddi akajibu ''aanh mimi niko period''

Kipofu kwa daktari

Kipofu alipelekwa hospitali na ndugu yake kufika hospitali nesi akawaambia ''kumuona daktari ni shilingi elfu kumi''

Yule aliempeleka hospitali kipofu akajibu, ''tumekuelewa ila huyu mwenzangu ni kipofu hawezi kumuona daktari''

Friday, November 12, 2010

Mmassai na mzigo

Mmasai mmoja alipewa lifti kwenye kenta alikuwa amejibebesha mzigo kichwani. Alipopanda kwenye kenta akawa bado mzigo wake upo kichwani. Wakamuambia aushushe tu si yupo kwenye gari mmasai yule akakataa katu katu.

Thursday, November 11, 2010

Headphone

Jamaa mmoja alimuuliza mwenzake swali lifuatalo, ''kwani hizi headphones ni za kupitishia sauti?''
Mwenzake akamjibu ''ndio maana ake''
Akauliza tena ''hazichakachui unachokisikia kweli?''