Karibu Sana.

Cheka Unenepe

Monday, June 14, 2010

Kupokea simu

Wanaume kadhaa walikuwa kwenye chumba kimoja cha kubadilisha nguo za michezo ghafla simu ikaita. Mwanaume mmoja akawaambia wale wote wakae kimya akaipokea simu:
Mwanaume: Halo?
Mwanamke: Halo honey, upo club?
Mwanaume: Ndio.

Mwanamke: Nipo mlimani city nimeona suti ya laki 6 ni sawa nikiinunua?
Mwanaume: Ndio mpenzi inunue tu.
Mwana ke: Pia nimeona Lexus ya 2008 mpya kwa $ 55,000 nimeipenda sana.
Mwanaume: Oh! Kwa pesa hiyo bila shaka.

Mwanamke: La mwisho mpenzi kuna nyumba masaki kwa Milioni 150 ipo full loaded.
Mwanaume: Consider it done.

Baada ya maongezi kuisha jamaa akatabasamu na kuiweka simu pale alipoikuta na kuuliza
''yeyote anaemjua mwenye simu hii nani?''

No comments:

Post a Comment